Polisi nchini Kenya wanamshikilia Mwanamke aitwaye Virginia Wangui Thiga kwa tuhuma za kumchanganyia dawa za kulevya kwenye kinywaji Mwanaume na kisha kumuibia Ksh. Milioni 1 (Tsh. Milioni 20.5)
"Mwanaume aliyeibiwa alikwenda Embakasi Club na Rafiki yake wa kiume wakakutana na huyu Virginia akiwa na Rafiki yake wa kike na wakawaomba wajumuike nao wakawa wanne wanakunywa pamoja"
"Baadaye yule Mwanaume (Rafiki wa Mtu ambaye pesa zake zimeibwa) akaondoka zake na kumuacha huyu Kijana akiwa na Wanawake wawili wakiendelea kunywa ghafla akazima (kupoteza kumbukumbu) amekuja kushtuka kajikuta ameibiwa simu, ATM Card na vitambulisho vingine, na akabaini kuwa Ksh. Milioni 1 imetolewa kwenye akaunti yake"
"Tumemkamata Virginia tunaendelea kumuhoji na upepelezi mwingine bado unaendelea kama kuna wengine watakaopaswa kuhojiwa pia tutawahoji" ——— DCI
#MillardAyoUPDATES
View attachment 2005104