Farolito
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 14,982
- 35,103
Dogo alinisimulia wakiwa boarding waliamka kwenda kunywa ule uji wa saa 11asubuhi,wamekunywa fresh sasa ile wanamalizia kunywa wale wapishi nao ndio wanamalizia kugawia wanafunzi wengine uji wa chini kwenye yale mapipa ndio wanaona lipaka limefia humo halafu limechambuka chambuka ile mbayaVijijini huko enzi zile tunasoma unaamka asubuhi unakuta eti sisimizi kibao wamejichanganya wameingia kwenye maziwa ya mgando. Unaona wanakupotezea muda bure. Unawavurugiamo kwenye maziwa halafu unawanywa humo humo. Siku nzima unacheua vitamin tu yaani afya kede kede. Mamende siyapendi hasa yale makubwa ila hawawezi kunifanya nikatupa chakula changu - hasa kama ni ugali na nyama. Nevaaa !!!

Kilichofuata hapo ni kila mtu kufa kivyake




