Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 183,582
- 1,105,378
Ujana kweli kaa la moto. Yaani kabisa nikapanda ndege. Safari ya masaa matatu. Halafu sasa tunakaribia kutua ndege inayumba huku na huko, mvua inanyesha balaa, upepo unavuma hali tete hatari. Nikiangalia nje kwenye dirisha giza tupu radi zinapiga chini maji ya bahari mpaka nikawa najiuliza sasa hii ndege ikianguka nitakwenda kusema nini mbinguni jamani mimi? Ila Mungu si Athumani tukatua salama aisee. Na mjidada wa kizungu nikaukuta hapo airport unanisubiri...heka heka zote zikasahaulika 










