Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Hii app ya browser-based ni mtihani. Labda ni kwangu tu lakini picha zikiwekwa moja kwa moja zinakuwa hazionekani vizuri mpaka mtu abonyeze kama anataka ku-download...

View attachment 2927650

Ukitaka zionekane vizuri wakati wa kuposti ni lazima u-click Insert

View attachment 2927651

Halafu uchague full image ndiyo upost....

View attachment 2927652

Sijui kama na wengine mna tatizo hili au ni mimi peke yangu...

App ya zamani ilikuwa nzuri mtu unaweka tu picha mara moja badala ya hizi steps zote. Hovyo tu yaani!
App ya zamani ilikuwa nzuri mtu unaweka tu picha mara moja badala ya hizi steps zote.
 
1709859799046.png
 
Kufuatia mahojiano na pacha waliokuwa wakisoma Chuo Kikuu Ardhi wakieleza jinsi walivyoweza kufanyiana mtihani, uongozi wa chuo hicho umesema unafanya uchunguzi wa jambo hilo.

Katika mahojiano hayo ya Wasafi FM yaliyofanyika Machi 6 mwaka huu, pacha mmoja alikiri kumfanyia pacha mwenzake mtihani wa marudio (supplementary) wa Hydrolojia kwa kutumia kitambulisho cha mwenzake baada ya kufeli mtihani huo.

“Tulikuwa chuo sasa unajua chuo tunasoma kozi ambayo kuna masomo ambayo tunaendana kwahiyo sasa kuna somo moja ambalo linaitwa Hydrology tukawa tunaingia class moja lakini bahati mbaya mwenzangu akapata supp mimi nikawa nimetoboa, sasa nikamwambia hapo kwenye supp tulia nitafanya mimi [..] akanipa kitambulisho chake nikamaliza akatoboa supp na hawakuwahi kujua,” mmoja wa pacha alieleza.

Aidha, uongozi wa chuo hicho umesema baada ya kufanya utafiti na kubaini ukweli wa taarifa hizo, umma utajulishwa juu ya matokeo ya uchunguzi huo.
FB_IMG_1709872473776.jpg
 
Fadhila Thomas Kiria wa USA River, Arusha amepotea katika mazingira ya kutatanisha akiwa mjini Moshi, asubuhi ya tarehe 4/3/2024 na hadi leo hajulikani halipo. Tarehe tajwa hapo juu Fadhila alikua dukani anapofanya kazi, Moshi mjini. Akalalamika kichwa kumuuma, akaacha simu na pochi juu ya meza dukani, akatoka kwenda kununua dawa. Lakini hakurudi mpaka leo. Ameacha mtoto mchanga wa wa miezi 5 anayenyonya.

Juhudi za kumtafuta maeneo mbalimbali ya Moshi na Arusha hazijazaa matunda. Taarifa imetolewa Polisi lakini bado hajaonekana. Ndugu wamemtafuta hospitali zote za Moshi, ikiwa ni pamoja na vyumba vya kuhifadhia maiti (mochwari) lakini hawajampata. Haijulikani kama yu hai au amefariki, au labda alipata tatizo la afya ya akili kutokana na maumivu ya kichwa. Tunaomba yeyote atakayemuona awasiliane na mama yake kwa simu nambari; 0762122114 au dadaye Berha: +255765688085. Asanteni na Mungu awabariki
FB_IMG_1709872457351.jpg
 
Back
Top Bottom