Wabunge ndio wawakilishi wa wananchi wa Tanzania serikalini. Kila mtanzania ana mahitaji yake au sauti yake anayotamani serikali isikie na itoe support au muongozo.
Ili kuwa na serikali ya watu tunahitaji kuwa na wawakilishi wa watu toka kila nyanja ili kuweza kuboresha na kuharakisha maendeleo ya nchi na watu wake
Sijawahi kusikia formula ya kwamba ratio muwakilishi au mbunge kwa wananchi inatakiwa kuwaje ila kwa kujifunza toka nchi tofauti na kwa kuangalia idadi yetu na uhitaji wetu wa maendeleo kama nchi bado hatuna idadi kubwa sana ya wawakilishi.
Tanzania tupo zaidi ya watu 60million na wote tunahitaji kuifikia serikali na kujadili mustakabali wa maisha yetu na taifa letu kupitia hawa watu.
Kikubwa kwenye viti maalumu ni kuchagua wawakilishi ambao watakuwa wanawawakilisha wananchi walio wengi, wenye uelewa mkubwa wa jamii ya mtanzania, changamoto na uhitaji pamoja na suluhu tarajiwa ili kuweza kufanikisha maendeleo ya wa mwananchi na taifa kwa ujumla