Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Nimechagua vitasa kwa sababu Vitasa ndiyo balaa kama pale Muhimbili vitasa vinashikwa na wagonjwa na wazima wangapi kabla ya wewe kukishika. Lakini pia kuna nguzo za kwenye usafiri wa Umma kama vile treni au mabasi ambazo zinashikwa na watu wengi. Inakuwaje katika kueneza magonjwa kwenye jamii? Ukiteremka kutoka kwenye basi huwa unakumbuka kwamba ulishika nguzo ya basi ambayo hapo kabla ilishikwa na mtu mwingine ambaye hujui alikuwa ni msafi kiasi gani?