Vita ya Gazeti la Mwananchi na Joshua Nassari- Limekosa hoja

Kwa kweli chadema tunaanza kuharibu nimejc kia vibaxa dah! Kucn tutajickia vip hii ni krediti kwa magamba kwa. Cio vzuri nasari umekosa kabsa.
 
It makes me sick kuona watu wanaotakiwa kuwa na akili wanatete upuuzi! So sick. Huyu kijana anahitaji kufunzwa, nilimsikia toka kwenye kampeni akitoa kauli kadhaa tata. Kauli hizi zisiposita hazitamgarimu yeye tu bali na chama pia. Mimi nilikuwepo kwenye mkutano na pale pale niliwaambia watu niliokuwa nao ile kauli si sahihi na si msimamo wa CDM. Elewa fika ule ni mkutano wa CDM, kauli inayotolewa pale inachukuliwa ni msimamo wa chama especially ikitolewa na kiongo wa chama ambaye ni mbuge. Dogo amechemka na kama tunataka kumsaidia awe kiongozi bora hatuna budi kumwambia wazi wazi.

Sir Winston Churchill aliyeiongoza Uingereza wakati wa vita kuu ya kwanza aliwahi kutengeneza kitengo kwa ajili tu ya kumkosoa. He was keen to know what he was not doing right! I usually call upuuzi upuuzi, dogo kakosea ajirekebishe, awe makini na kauli zake asilewe akipigiwa kelele za kushangiliwa na watu. Kauli ile haina tija kwake wala kwa CDM.
 
Nawaombeni sana kama mnampenda nasari kwa moyo wa dhati mwambieni ukweli, kwa kufanya hivy mtakuwa mmemjenga na mmemsaidia. siwezi kukubali kumpamba nasari ilihali ni kweli kachemka!!ni kweli alikurupuka kuzungumza kauli ile.anachotakiwa kuelewa ni kila atakachoongea Nassari kinayo impact kwa jamii, hivyo basi wote waliomkosoa naungana nao weather wawe wanayo nia njema au mbaya mimi ninawaunga mkono kwani kauli aliyoitoa hakuipima, ni vizuri Nasari akawa makini kwa kauli yoyote atakayoitoa ajue inauzito kwa jamii kama kiongozi na asikurupuke kuufurahisha umma kwani ataaibika na hii itaweza kuharibu sura na taswira nzuri ya chama chetu hivyo kwa wapenda haki wote tuungane kwa hili tumrekebishe Nasari kwa nia Nzuri kabisa.
 
Tusipende kusifiwa tu,tukubali na kukosolewa pia. Challenge is the better practice to reach the gentleman stage.
 
.....hayo ni maoni ya MUHARIRI na sio habari. Kwakua sie tuna AKILI na BUSARA Tusiya BEZE tuya heshimu. Huwezi fananisha gazeti la MWANANCH na magazeti megine hapa !
 
Bado ni tetesi, kwamba gazeti la mwananchi itatumiwa kuchafua chadema kwa kuandika habari ambazo itawafanya wananchi kuwa na hisia mbaya na chadema,tangu wakati wa uchaguzi wa arumeru mwandishi wao mmoja alikuwa anatumia jina la bandia kwa taarifa zake,na inapangwa baada ya kuona mwananchi inawasomaji wengi......lakini mwanachi kuwa katika siasa kwa upande mmoja,inatia shaka kwa wasomaji wao hao wengi
 
Bado ni tetesi, kwamba gazeti la mwananchi itatumiwa kuchafua chadema kwa kuandika habari ambazo itawafanya wananchi kuwa na hisia mbaya na chadema,tangu wakati wa uchaguzi wa arumeru mwandishi wao mmoja alikuwa anatumia jina la bandia kwa taarifa zake,na inapangwa baada ya kuona mwananchi inawasomaji wengi......lakini mwanachi kuwa katika siasa kwa upande mmoja,inatia shaka kwa wasomaji wao hao wengi

Sasa mhariri amejitosa mzima mzima kutaka kuangamiza chama!
 
Na ndiyo maana sasa hivi gazeti mwananchi linajikomba kwa watawala kwa kutenga kurasa za gazeti lake kutukana wapinzani.

4Sure wata cheki mapicha picha, kitu wanachofanya ni sawa sawa na kupiga sarakasi sebleni huku umevaa taulo mbele za watoto.
 
Nataka nitofautiane kwa mbali na mashambulizi aliyofanya mhariri wa gazeti la Mwananchi dhidi ya Mbunge wa Arumeru Mh. Joshua Nassari. Kauli aliyotoa Nassari siyo kauli mbaya kuliko zote kutolewa na kiongozi wa kisiasa kiasi cha Mhariri kutumia maelezo mengi kumdhalilisha mbunge huyu eti "alikuwa hajajipanga kuwa Mbunge". Huu ni unafiki mkubwa na chuki binafsi kwani the same gazeti kwa kipindi chote karibu mwenzi mzima wa Kampeni za ubunge huko Arumeru liliweza kusikiliza na kuripoti kampeni za Nassari vizuri kabisa na wakati mwingi kumsifia. Mwezi huo ulikuwa unatosha kueleza wanayoeleza leo kwani si rahisi kama mtu hana busara au zimtoshi kuweza kuzificha kwa mwenzi mzima. Mfano mzuri ni Livingistone Lusinde alivyodhihirisha utaalam wa matusi na utomvu wa nidhamu kwa muda mfupi alioshiriki katika kampeni. Leo hii Joshua anateleza kidogo Gazeti la mwananchi linamshambulia eti anatakiwa afundwe, na alikuwa hajajipanga kuwa mbunge. Hili gazeti nasema limetumwa na inawezekana ndio mwanzo wa kupoteza dira na heshima iliyojijengea.

Hivi ni mara ngapi mkuu wa nchi anatoa kauli mbaya na hata za iabu kuliko Nassari na hamsemi anahitaji kufundwa au hajajiandaa kuwa rais?

"Ni mara ngapi Mawaziri wanatoa kauli ambazo zinatia kichefuchefu na aibu kwa taifa na humuandiki?"

Iweje leo mtumie karibu ukurasa mzima kumshambulia Mbunge wa Arumeru.

GAZETI LA MWANANCHI LIMEKWENDA MBALI SANA KWANI MAJUMUISHO YA MHARIRI YANATAKA KUAMINISHA WASOMAJI KWAMBA NASSARI HAJUI AFANYALO, HAJATULIA, HAJAKOMAA NA HANA UWEZO WA KUONGEA MAJUKWAANI.
Mimi natofautiana nanyi kutokana na chuki binafsi mliyoonyesha kuicheza ngoma msiyoijua sawasawa.

wewe acha unazi usio na maana mhariri ana kosa gani hapo? kila siku unataka usikie positive information kuhusu wanachama na chama cha chadema,waandishi wakijaribu kutoa mtazamo negative kwa chama chenu mnaanza kulalamika bila mpango. mimi nakwambia kitu kimoja dogo pale kateleza aombe radhi kwa umma aache ujanja usio kuwa na tija kwa wananchi. yeye nimbunge lazima ajue wananchi wanamtegemea kama kioo cha jamii.
 
Mwananchi ni sehemu ya Nation Media Group na wako Kenya hata Uganda.Wamiliki ni wazito wa Dunia hii akiwemo The Aga Khan na hapa nyumbani hata KING MAKER ROSTOM AZIZ anaweza kuwa mwanahisa.
Kama wewe ni msomaji kuna siku waliandika tahariri iliyoweza kutafsirika kama maudhi kwa Usalama wa Taifa na kuna raia mwema au mtanzania wa hivyo ambaye aliibuka kuwatishia wahariri.Yaonekana walizibwa mdomo kiaina na sasa ili kudumisha biashara zao wahariri wa Mwananchi wamepotea hatua wakamshambulia Nassari ili walau kujikomba kwa dola lililowatishia maisha.
Hawa wako kibiashara zaiiidi na maneno ya unabii wa waziwazi ya Waziiri Mkuu Mstaafu Frederick T.Sumaye kuwa kama unataka biashara yako ikunyookee njoo CCM yanathibitishwa QED
 
Tido Mhando bosi wa Mwananchi alikuwa mtumishi mtiifu wa magamba kwa muda mrefu kwa hiyo gamba halijavuka vizuri kwa hiyo usishangae gazeti kupoteza muelekeo. Mbona alichoongea Nassary ni kidogo mno ukilinganishwa na yanayozungumzwa na RADIO IMAAN kila siku. Hii Radio inaongelea kuwabagua watanzania na kuwagawa mchana kweupe lakini si gazeti la Mwananchi au polisisiem waliolaani hiyo radio

Na alikuwa rafiki mzuri wa EL. Mara nyingi alihakikisha safari za EL ziko well covered na hata yeye mwenyewe binafsi alikuwa anachukua nafasi ya kumhoji EL (wakati akiwa PM) ili aweke mambo sawa.
 
Mbona JK kamteua Mbatia kutimiza yale waliyokubaliana na Cameroun kuhusu haki za "Makundi mengine" ndani ya jamii lakini hawasemi kwamba amekosea!

HUENDA AISEE, HAHAHAAAH watu wadadisi sana, watu wanafikiri kwa kina
 
kwa maoni yale....mwananchi linaanza kupoteza mwelekeo

Kama iliwalazimu kumwandika Joshua kwa sababu za kuwa neutral je ingekuwa aliyekosea ni Tido Mhando mkurugenzi wa Mwananchi wangemweka kwenye tahariri kwa kina namna ile? Hebu Mhariri wa mwananchi try to be fair. Kwa kuandika vile ni ujumbe gani unataka kuwapa watu wa Arumeru waliomchagua Nassari?
 
Nimeisoma hiyo habari binafsi sijaona tatizo na makala hiyo zaidi ya ushauri tena uliotolewa wakati muafaka.

Chadema ni chama kinachotarajia kuchukuwa dola na kimekuwa na mvuto hivyo watu wanakichukulia kwa uzito ndiyomàna kauli za viongozi wake zinapaswa kuwa makini sana màna watu wanazichukulia kwa uzito wake laiti kauli kama hiyo angeitoa mtu wa ccm wala isingekuwa hoja maàna wamezoea.
 
Nimeisoma hiyo habari binafsi sijaona tatizo na makala hiyo zaidi ya ushauri tena uliotolewa wakati muafaka.

Chadema ni chama kinachotarajia kuchukuwa dola na kimekuwa na mvuto hivyo watu wanakichukulia kwa uzito ndiyomàna kauli za viongozi wake zinapaswa kuwa makini sana màna watu wanazichukulia kwa uzito wake laiti kauli kama hiyo angeitoa mtu wa ccm wala isingekuwa hoja maàna wamezoea.

Kurunzi, kwa nini Mwananchi haikuoa such comments wakati wa kampeni? kuwa ndg. Nasari hafai, mbona kuna mbuge mmoja wa alishasema kwa hali inavyotokea North Mara, is better Tarime iwe kivyake, na hakuna kilichosemwa na hata hao magamba? kwa nini aonekane kuwa hafai kuwa mbuge?
 
Kama iliwalazimu kumwandika Joshua kwa sababu za kuwa neutral je ingekuwa aliyekosea ni Tido Mhando mkurugenzi wa Mwananchi wangemweka kwenye tahariri kwa kina namna ile? Hebu Mhariri wa mwananchi try to be fair. Kwa kuandika vile ni ujumbe gani unataka kuwapa watu wa Arumeru waliomchagua Nassari?

Huyu mhariri tunamjua siku nyingi na agenda yake chafu ya kuiteketeza CDM.Tunamuuliza alikuwa wapi kuandika uchochezi wa namna hii Lusinde alipotukana matusi ya nguoni? Hawa mwananchi waache unafiki wao.Wasaliti wakubwa hawa!
 
Nataka nitofautiane kwa mbali na mashambulizi aliyofanya mhariri wa gazeti la Mwananchi dhidi ya Mbunge wa Arumeru Mh. Joshua Nassari. Kauli aliyotoa Nassari siyo kauli mbaya kuliko zote kutolewa na kiongozi wa kisiasa kiasi cha Mhariri kutumia maelezo mengi kumdhalilisha mbunge huyu eti "alikuwa hajajipanga kuwa Mbunge". Huu ni unafiki mkubwa na chuki binafsi kwani the same gazeti kwa kipindi chote karibu mwenzi mzima wa Kampeni za ubunge huko Arumeru liliweza kusikiliza na kuripoti kampeni za Nassari vizuri kabisa na wakati mwingi kumsifia. Mwezi huo ulikuwa unatosha kueleza wanayoeleza leo kwani si rahisi kama mtu hana busara au zimtoshi kuweza kuzificha kwa mwenzi mzima. Mfano mzuri ni Livingistone Lusinde alivyodhihirisha utaalam wa matusi na utomvu wa nidhamu kwa muda mfupi alioshiriki katika kampeni. Leo hii Joshua anateleza kidogo Gazeti la mwananchi linamshambulia eti anatakiwa afundwe, na alikuwa hajajipanga kuwa mbunge. Hili gazeti nasema limetumwa na inawezekana ndio mwanzo wa kupoteza dira na heshima iliyojijengea.

Hivi ni mara ngapi mkuu wa nchi anatoa kauli mbaya na hata za iabu kuliko Nassari na hamsemi anahitaji kufundwa au hajajiandaa kuwa rais?

"Ni mara ngapi Mawaziri wanatoa kauli ambazo zinatia kichefuchefu na aibu kwa taifa na humuandiki?"

Iweje leo mtumie karibu ukurasa mzima kumshambulia Mbunge wa Arumeru.

GAZETI LA MWANANCHI LIMEKWENDA MBALI SANA KWANI MAJUMUISHO YA MHARIRI YANATAKA KUAMINISHA WASOMAJI KWAMBA NASSARI HAJUI AFANYALO, HAJATULIA, HAJAKOMAA NA HANA UWEZO WA KUONGEA MAJUKWAANI.
Mimi natofautiana nanyi kutokana na chuki binafsi mliyoonyesha kuicheza ngoma msiyoijua sawasawa.

Nadhani hapo gazeti halijakosea

Babu yangu hapo zamani za utoto wangu huniambia "Mtoto anayependwa sana hugombezwa sana"
 
Back
Top Bottom