Na mbona yeye hataki kujitanabaisha yeye kama yeye badala yake anajificha kwenye wingi na si umoja ""eti tumeumba mbingu na ardhi na vilivyomo"
Ngoja nikukumbushe jambo:
Huko juu nimeandika kuwa"namna ambavyo wanapinga wasio waislamu wa sasa ni sawasawa na wale ambao ni makafiri wa zamani wakati wa zama za Nabii Mussa:[emoji116]
Mfn:
MUNGU anasema,hauji muujiza lazima adhabu itafata mbele yake.
Sasa basi,Musa alipotumwa aende kwa firauni nae pia alipewa muujiza wa.
Fimbo kuwa nyoka.
Mkono kuwa mweupe kama mwezi nk.
Lakini watu wake ambao alitumwa akawaongoe wengi wao walimwita mchawi.
Na walimkubali wachache mno.
Hata hapa wewe unaganda kwenye neno sisi[emoji116]
Hata hapo MUNGU angetumia neno Mimi pia ungehoji,hukumbuki Musa nae walimuhoji?
Naamini Mimi naandika hapa ila hamtafakari hata kidogo haya niyaandikayo.[emoji116]
MUNGU anasema tena,hao wasioamini hutafuta katika Qur'an maneno yenye utata kupotosha maneno ili wabaki tu kwenye imani zao.
Narudia:
Qur'an imeshuka kwa lugha ya kiarabu ili iwe nyepesi kusomeka...katika fasili za lugha MUNGU hutumia neno sisi kama kuonyesha ukubwa na utawala wake mbinguni...kuenea kwa nguvu zake.