Virtual Private Network (VPN) imenirudisha JF

Unajidanganya na VPN yako, wewe jiulize kwanini mitandao yote ilifungiwa ikabaki JF.

Huu ni mtandao wa serikali, hata censorship ya thread inakupa hilo jibu.

VPN ni sawa na kuingia motoni na rain jacket.

Usalama wako ni kusoma tu usiandike chochote JF kama mimi, hahaha.
 
Mimi nlikuepo kipindi chote ccm walipizima internet,wengine vpn tunayo kitambo
 
Acha kumdanganya mwenzako.
 
Kesho tarehe 2/11/2020 ndio mwanzo wa maandamano ya kitaifa. Tunasisitiza kwa wafuasi wetu: maandamano lazima yawe ya amani. Tuna wasiwasi juu ya tabia ya mamlaka (polisi, ujasusi na jeshi) ambao wanaweza kuua watu wetu. Wauaji watawajibika mmoja mmoja
 
Mimi VPN niliipata mapema sana siku ile ile ya uchaguzii asubuhi , tatizo la kusumbua mtandao lilianza siku kabla ya uchaguzi nililigundua kwenye saa 11 hivi nilihisi mtandao wamefunga lkn sikuwa na uhakika ..nilikuja kuthibitisha asubuh ya uchaguzi baada ya kuona watu wanalalamka nikajua tayari huko, lkn ndugu yangu mwa DIT akanifanyia mambo mapema nikarudi hewani , niliipata vpn kupitia gugo ilikua haisumbui kasoro social network tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…