Vipi update za mazungumzo na Accacia

Vipi update za mazungumzo na Accacia

Mie sielewi. Wanajadili nini kati ya noah au kwenda jela kwasababu ya wizi wao? Hili la wizi linatajwa humu na madai ya kodi pia.
Najishangaa tena, hivi nani anadaiwa hapa kati ya Acacia na barric? Au wote ni watuhumiwa wa wizi na kodi?
Tuibieni hata agenda moja nyinyi wagawa chai!
 
Bado sijakata tamaa kabisa! Ila kukosekana kwa "Tweet" kama kawaida ya Jumba jeupe kunanipa mashaka sana!!
 
Nipo hapa nasubiri Noah yangu kwa hamu yote ila cha kuhudhunisha hata mrejesho wa stori wakati wanakunywa chai sijasikia
Nahisi zile Noah zetu zimeota mbawa. Kwa ukimya huu, nimeondoa matumaini ya kupata hata boda boda. Mimi nimesha amua naenda zangu Zimbambwe.
 
Kupitia Uzi Huu Naomba Kujua Vp Yule Aliekua Anaiba Mil 7 Kwa Dakika Aliishia Wap , Pia Yule Mwenye Nyumba 73 Ndo Vp Tena Kaludi Kumilik Nyumba Zake Au Imekuwaje,,
 
Sina chanzo chochote cha taarifa za ndani kati ya serikali na acacia . Ila nadiriki kusema mazungumzo hayo yalishakwisha kitambo kwa kutumia akili za kuzaliwa tu. Hebu tujiulize machache haya harafu tuamue mazungumzo yanaendelea au yashakwisha kitambo.

Tangu mazungumzo hayo yaanze ni takribani mwezi sasa. Je mtanzania mwenzangu una amini unaweza kukaa na mzungu mwezi mzima kujadili jambo moja kama hili la mchanga??? Kwa ninavyowafaham wazungu wanajali sana muda kuliko chochote kile . Siamin hata kidogo kwamba bado wanazungumza na serikali yetu. Kwan hayo mazungumzo ni ya kuuziana nchi ? Mazunguzo ya nani yuko sahihi kati ya ACACIA na serikali ndio ichukue muda wote huo?? Thubutu!! Mazungumzo yalisha isha, ila naona tumepigwa za usso sasa tunajipanga tutatokaje mbele za wananchi.!! Mzungu kwake masaa 24 ya kuacha kaz moja harafu afanye kaz ya ziada jua kaz ya siku tatu itafanywa kwa siku moja. Tukae bongo na wazungu wale mwez et kujadiliana nani yuko sahihi?? Mnipige mniue hakuna kitu kama hicho.

Kinachoweza kutokea ni labda walikaa siku mbili tatu kila mmoja akaenda zake kuandaa maamuz ya oficce yake than wamepanga kuja kukutana siku ya kutoa taarifa. Lakn hili la kusema mazungumzo yanaendelea tutakua tunaota.

Kingine cha kutia shaka. Iweje ACACIA wapeleke notice ya kukusudia kutushitak kama mazungumzo yanaendelea?? Si watakua wanafanya maamuz wakati kikao kinaendelea jambo ambalo litatia litahatarisha mazungumzo kukatika?? Kuna uwezekano mkubwa tumeshindana nao kwa kukaa meza moja kwa zile jeuri zetu . Sasa wameamua kutuonyesha njia sahihi ya kutuonyesha hawatanii kwamba hawatoi hata mia isipokua wao ndio wanatudai.

Mwisho;

je wewe mdanganyika mwenzangu una amini mazunguzo yanaendelea???
 
Mimi pia nasubiri kwa hamu kuambiwa kile tulichokubaliana.

Japo naona ndoto ya kumiliki Noah inazidi kufifia.

Hisia pia zinanituma kuamini kuwa tupo ICU. Maana ninavyomjua Baba Jesca na misifa yake, kama mambo yangekuwa poa tungeshajua kitambo sana.

MUDA NI MWALIMU MZURI.
 
Hahaha yule professor alietoa ripoti kwa mbwembwe bila kujua kama atakabidhiwa kazi ya kurejesha mpunga sijui anapumulia mashine gani. Ukitaka sifa kutoa ripoti taka sifa pia kurejesha mpunga[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]


Tik tok tik tok.
sent from my iPhone 7s using JamiiForum mobile app.
 
Hapa Sirikali inakuwa bubu, Ila siku Tundu Lissu aki- release press utaona jinsi Sirikali itakavyokuja resi na matamko ya hapa na pale.

Mara utasikia wapinzani ndio wamesababisha tusilipwe, Mara hawa sio wazalendo, sijui nani katoa siri.....

Time will tell
 
Back
Top Bottom