Vipi kuishi na mume mkali kupitiliza?

zoooozy

New Member
Sep 24, 2017
3
7
Natumai ni wazima..

Lengo la kuanzisha uzi humu ni kutaka msaada wetu wa mawazo jinsi ya kuishi na mume mkali.

Nina miaka minne kwenye ndoa na watoto wawili.

Kwa kweli nampenda mume wangu na yeye najua ananipenda lakini napata mawazo ya kuomba talaka sababu tokea niolewe hajabadilika kabisa anaweza nifokea hata mbele ya wazee wake kisa mtoto kaumia bahati mbaya. Yaani hata mtoto akiamka usiku akalia anatoka sana anasema namfanyia fujo makusudi!

Nikisahau kitu kama chupa ya maji kwenye gari yake anafoka hadi kuishia kuniita ukuta na kutaka kunipiga.

Naumia sana ndugu zangu naombeni ushauri.
 
Huyo ulipaswa kumuonyesha msimamo mapema, hata hivyo hujachelewa. Mueleze kuwa unakerwa na tabia ya kukufokea kama mtoto mdogo, na kwamba unahitaji akuheshimu kama mke kama wewe unavyo muheshimu kama mume baas. Ukimlegezea mwisho atakuja kukutia makofi.
 
Hongera sana kwa kueza kuistahimili hiyo miaka yote.jaribu kuongea nae akishindwa badilika lifikishe kwa wazazi wake pasina kusahau kumshirikisha Muumba wake.

Akishindwa kabsa msisitize tu akiwa anakugombeza ajitahidi kukuita majina km honey, sweety,laaziz,mahbuba,Mke wng,m
ama watoto otherwise akikuita tu ukuta usiitike wala ongea chochote maana sikumbuki km ukuta unasikiaga ama kuongea
 
Tafuta muda anaraha,kaa zungumza nae na umwambie hiyo tabia hupendi inakuumiza na kukudhalilisha pia...

Tambua km ni tabia yake anaona ni sawa tu na hakosei kitu mana kazoea.....hivyo bas kubadilika kwake itachukua muda, talaka si suluhisho.... aso hili analile
 
Ukali ni tabia,
Ukali ni udhaifu.
Mimi mwenyewe ni mkali hadi najiogopa japo siyo rahisi kuniona nikifoka hovyo.
Lakini akiniudhi mtu kupitiliza naweza kumkemea na akimbie kuelekee kusikojulikana.
Nilipogundua mimi ni mkali na huumiza wengine, kwasasa nina mabadiliko makubwa sana.
Hii hali huwezi kuamua kuwa mkali bali ni udhaifu.
LAKINI USISAHAU WATU WAKALI wana huruma sana hasa ukimweleza tatizo huwa anaguswa haraka kukusaidia.
Tumia muda mnapokuwa na furaha mweleze kwa hisia za ndani kuonyesha jinsi anavyokuumiza.
 
Ukali ni tabia,
Ukali ni udhaifu.
Mimi mwenyewe ni mkali hadi najiogopa japo siyo rahisi kuniona nikifoka hovyo.
Lakini akiniudhi mtu kupitiliza naweza kukemea na skimbie aelekee kusikojulikana.
Nilipogundua mimi ni mkali na huumiza wengine, kwasasa nina mabadiliko makubwa sana.
Hii hali huwezi kuamua kuwa mkali bali ni udhaifu.
LAKINI USISAHAU WATU WAKALI wana huruma sana hasa ukimweleza tatizo huwa anaguswa haraka kukusaidia.
Tumia muda mnapokuwa na furaha mweleze kwa hisia za ndani kuonyesha jinsi anavyokuumiza.
There u are. Me pia ni miongoni mwa hao. Hua najikuta nafoka sana mpaka najua kabisa nimemuumiza mtu ila akitulia tu aje muda aniambie huwa nakuwa mpole na kama kuna kitu anahitaj on the namtimizia tena kwa upole kabisa. Labda tuna mapepo..
 
There u are. Me pia ni miongoni mwa hao. Hua najikuta nafoka sana mpaka najua kabisa nimemuumiza mtu ila akitulia tu aje muda aniambie huwa nakuwa mpole na kama kuna kitu anahitaj on the namtimizia tena kwa upole kabisa. Labda tuna mapepo..
Siyo mapepo ni udhaifu flani, ukichunguza vizuri watu wakali hawana asili ya utani wa kijinga, ni watu siriaz kwa kila jambo na wachapa kazi, wanaamini ktk kazi, so udhaufu wetu ni hako ka ukali but all ni all nimefanya utafiti nakujiridhisha 90% ya watu wakali siyo katili, siyo wachoyo na wengi ni wakarimu kupitiliza but 10% yao ni kinyume chake. Mtu akiweza kumvumilia mtu mkali na kumwezea AMEPATA CHOMBO CHEMA
 
There u are. Me pia ni miongoni mwa hao. Hua najikuta nafoka sana mpaka najua kabisa nimemuumiza mtu ila akitulia tu aje muda aniambie huwa nakuwa mpole na kama kuna kitu anahitaj on the namtimizia tena kwa upole kabisa. Labda tuna mapepo..
Usisahau kuwa hatuna vinyongo hata mkizipiga within 5 mins hasira hakuna tena na mambo yanasonga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom