Vipepeo Weusi: Mkakati Namba 0034 (Simulizi)


VIPEPEO WEUSI: MKAKATI NAMBA 0034








EPISODE 13




Nikiwa bado nimefumba macho kwa uchungu na hasira iliyochanganyika na hofu, kitu pekee nilichokuwa nakiona katika ufahamu wangu ni giza lililotanda ambalo niliamini kuwa leo yaweza kuwa siku yangu ya mwisho duniani.

Lakini ghafla..!!! Nikasikia mtu anafoka..

"Ole wako umguse hata shati."

Nikashtuka kutoka katika hofu yangu na uchungu na kufumbua macho. Blaki naye nikagundua ameshtuka na kugeuka kuelekea upande sauti ilipotoke.
Kushoto mwa uwazi wa kuingilia kwenye uchochoro alikuwa amesimama Godi. Mkononi ameshika kipande cha karatasi.

"Narudia ole wako umguse hata shati" Godi akaongea kwa kujiamini huku anaingia kwa nguvu kumpita yule mahabusu mwingine aliye kaa pale kwenye uwazi wa kuingilia uchochoroni.

"Unasemaje wewe mseng*" blaki akafoka kwa hasira huku anamsogelea Godi kwa shari.

Godi akapiga hatua moja mbele kwa kujiamini huku anaongea.

"Kama unataka RCO Sweya ajue kuwa maiti ya askari wake imefukiwa nyumbani kwenu nyuma ya nyumba, basi mguse huyo au niguse mimi! Pia kama unataka taarifa za bunduki mlizoficha nyumbani kwa bimkubwa wako kihondo zimfikie RPC basi niguse au mguse huyo! Naamini kesi iliyokuleta humu ni kesi ya kijinga tu ya kukutwa na kiroba cha bangi! Sasa kama unataka kesi ya mauaji ya askari pamoja na ujambazi wa silaha zikukute basi jaribu kutugusa!! Naamini Bimkubwa wako pia hawezi kuwa Salama kwenye hizo kesi.. So kama unajiona wewe ndio kidume pekee mwenye pumb* basi tuguse."

Godi aliongea kwa kujiamini na kwa utulivu wa hali ya juu kana kwamba yuko juu ya kilele cha dunia.
Akasogea hatua nyingine mbele na kukaribiana kabisa na blaki, kisha akaendelea kuongea.

"Na usidhani nakutania, chukua hii karatasi ukajisomee ushaidi wa hiki nilichokueleza"

Godi akaongea huku anakunja karatasi aliyokuwa ameishika mkononi kisha akamuwekea Blaki kwenye mfuko wa suruali. Wakati anaikunja kunja karatasi niliitazama kwa makini na kugundua kuwa ilikuwa ni karatasi ile niliyopewa na Baba Bite ambayo ghafla nilikuwa siioni kwenye mfuko wangu wa suruali.

Blaki alikuwa amefura kwa hasira lakini ameganda kana kwamba ni sanamu ya barafu. Niliwatazama na wale 'wapambe' wake, nao macho yalikuwa tamewatoka kweli kweli na wamegubikwa na mshtuko usoni.

Ilikuwa kana kwamba ni mnyama swala amemulikwa na tochi kali usoni nyakati ya usiku. Licha ya ujanja wa swala uliotukuka muda wa mchana, lakini hakuna mnyama mjinga kama swala umshitukize usiku kwa kummulika na tochi kali usoni. Anabaki ameganda ameduwaa hajui afanye nini.

Ndicho kilichokuwa kimemkuta Blaki muda huu. Aliganda ameduwaa ingawa bado alikuwa amefura kwa hasira.

Walikuwa wamesogeleana na Godi kwa ukaribu bado kidogo pua zigusane na Godi wamekaziana macho wanaangaliana.
Wakaganda hivyo kwa takribani dakika moja nzima hakuna anayepepesa macho.

Ghafla Blaki akageuka na kuanza kuondoka kutoka kwenye uchochoro. Wapambe wake wakamfuata. Wakaondoka kuelekea yard namba moja.

"Oooooooooopppssss" Godi alihema kwa kutoa pumzi ndefu nje na kukaa chini.

"Wewe mseng* unajua leo tungekufa wote hapa??" Godi akaongea kwa akiwa ana hema na kukaa chini vizuri.

"https://jamii.app/JFUserGuide! Asante kwa kuiba karatasi yangu na asante kwa kuniokoa" nikaongea huku nahema kwa nguvu pia na kuingizia utani kwa mbali lakini bado paniki ilikuwa haijaisha ndani yangu.

"Sihitaji asante yako wala ujinga wowote! Ninachotaka unambie wewe ni nani na nini kinachoendelea" Godi akaongea huku ananyanyuka pale chini akijishikilia ukutani kana kwamba amechoka kwa kukimbia umbali mrefu.

"Hapa sio mahala sahihi kuongea hayo mambo" nikamjibu na wote tukaanza kutembea haraka kutoka hapo uchochoroni.

Tukaelekea yard namba mbili na kutafuta sehemu ya peke yetu na kuketi.

"Tangu siku ya kwanza nilihisi kuna kitu unaficha! Unaongea uongo" Godi akafungua maongezi mara tu tulipoketi chini.

" Jana nilipokuwa nimekupokea humu gerezani na kukuonyesha mazingira unakumbuka baada ya hapo ni kitu gani cha kwanza uliniomba?" Akaniuliza.

"Kitu gani?"

"Uliomba kwenda chooni.!" Akaongea huku ana tabasamu.

"Kwahiyo ndio nini sasa?" Nikamjibu nikijifanya sielewi anachoongea.

"Skia kijana, nina uzoefu sana na jela.! Mahabusu akitoka huko nje alafu akirejea humu na kitu cha kwanza akielekea chooni, humu jela tunaita anaenda 'kudownload'! Yani kuna vitu amevificha nyuma huko labda hela, bangi au chochote so anataka kwenda kukitoa" akaongea huku anatoa tabasamu Fulani hivi la mzaha. "Sasa Jana uliniambia unaataka uende chooni na nikakufanyia kusidi tu kukwambia usubiri mpaka tukiingia selo ili nione utafanyaje na cha ajabu tulivyoingia tu selo kitu cha kwanza ukaenda chooni! So nikajua kuwa ulienda kudownload.. Tukipokuwa tumelala nikakusachi mifukoni nijue ulicho enda kudownload chooni ndio nikakuta karatasi. Sikuisoma wala nini na nikairudisha tena mfukoni mwako coz nilijua asubuhi ukiikuta haipo utajua ni mimi na ilipofika asubuhi kwenye wakati tumepanga mstari tunafunguliwa kutoka selo nikakuchomoa tena hiyo karatasi na nikaenda kuisoma na kukuta hayo niliyoyakuta. Sasa humu jela watu wanaingiza bangi, wanaingiza hela na vitu kama hivyo lakini wewe umeficha karatasi na ulikuwa na shauku ya kujua taarifa za Kaburu so moja kwa moja hii ina maana lazima wewe utakuwa mtu wa 'system' na humo humu kwa kazi maalumu!! Una swami lolote kwanza mpaka hapo"
Godi akaongea kwa madaha kabisa, ni dhahiri alikuwa anainjoi jinsi alivyonibananisha.

"Endelea!" Nikamjibu kwa kifupi tu kwa kukereka lakini niko makini.

"OK!" Akakaa vizuri na kuendelea, "baada ya mazoezi nikakuonyesha Kaburu alipo na nikafuatilia kwa mbali mlivyokuwa mnabishana, nikafuatilia ulivyorudi yard huku, nikafuatilia Sinyorita alivyokuja kukuita na nikakuona ulivyoelekea uchochoroni kuonana na kina Blaki, so ikanibidi nitumie uzoefu wangu wa kitaa na taarifa niliyosoma kwenye karatasi yako na nikajitoa kuwa 'Yesu mtoto'! Nikatoa maisha yangu ili niokoe maisha yako!!" Akaongea huku akimalizia na utani kama kawaida.

"Na kilichokufanya uhatarishe maisha yako kuokoa maisha yangu ni nini?" Nikamuuliza kwa shauku kwasababu ingawa nilimshukuru sana moyoni kwa kuniokoa lakini bado moyoni nilokuwa najiuliza kwanini alijihatarisha kiasi kile kuniokoa. Hatukuwa tumeshibana kiasi kwamba awe tayari kufanya 'chochote kwa ajili yangu'.

"Jibu lake simpo tu" akaongea huku ana tabasamu, "wanakwambia ukikaa karibu na waridi lazima unukie! Sikufichi Ray, hii kesi niliyonayo safari hii lazima itanifunga na nahisi nitafungwa namba ndefu sana.. So, nimekuokoa namna ile nadhani haitakuwa vibaya kama ukiongea na hao wenzako kwamba msinisahau katika ufalme wenu na kunisaidia niepuke kifungo! Hiyo ndiyo sababu na bila kusahau nimefanya vile kwa upendo pia hahahaha" akaongea hoja yake ya kweli kwanini ameniokoa kisha akamalizia kwa kuingiza utani tena.

"Wow! Una mikakati mizuri ila ulichokosea tu ni kwamba mimi sio mtu wa 'system'! Mimi raia kama wewe"

"Ucha ufala basi! Nimekuokoa sekunde chache zikizopita alafu unashindwa kuniheshimu kusema ukweli.. Acha mambo ya kiseng* aisee" Godi akafoka na mzaha ukaondoka kabisa usoni mwake.

"Ok ok ok! Labda niseme kwamba mimi ni raia kama wewe ila nashirikiana na 'system' kuhusu masula fulani"

"Masuala gani?"

"Siwezi kukwambia!"

"Sihitaji unambie nataka angalau unitoe tongo tongo usoni!"

Nikajifikiria kwa sekunde kadhaa nimueleze nini? Haitakuwa uungwana kwangu kumficha kabisa ukizingatia kuwa ameniokoa kutoka kwenye kifo dakika chache zilizopita. Lakini pia nikagundua kutokana na uzoefu wake wa jela, Godi anaweza kuwa 'asset' kwangu.

"Ooooops! Ok, ulisikia kuhusu kifo cha Waziri Josephat Kipanju?" Nikamuuliza.

"Kila mtu amesikia kuhusu hilo!"

"Ok! Ni kwamba tunaamini kuwa Kaburu anafahamu taarifa kuhusu muuaji wa Waziri Kipanju" nikamweleza kwa kifupi.

"Duuuuhh!" Akaguna, "na umesema wewe ni raia kama mimi sasa uchunguzi wa mauaji ya Viongozi wa serikali wewe unakuhusu nini?"

"Kwa kifupi tu labda niseme kuna mtu wangu wa karibu amesukumiwa fuko la mavi kuhusishwa na kifo hicho kwahiyo nisipozipata taarifa za muhusika halisi wa tukio like kutoka kwa Kaburu basi ndugu yangu nitampoteza!" Nikamfafanulia.

"Aiseeeee!! Una Bahati mbaya aisee, maana huyo Kaburj mwenyewe kwanza huwezi kumpata muda wa mchana na hata ukimpata sijui utamweleza nini ili atoe hizo siri" Godi akaongea huku anainuka.

Wote tukainuka, makalio yakianza kuuma kwa kukaa chini mda mrefu. Tukainuka na kuendeleza maongezi huku tunatembea tembea pale yard.

"Kaburu huwa ana shinda wapi mchana?" Nikamuiliza.

"Ofisini kwa mkuu wa gereza!" Akanijibu.

"Whaaaat?? Anafanya nini ofisini kwa mkuu wa gereza??"

"Humu jela kila mfungwa anapangiwa kazi ya kufanya! Ndio maana wengine unawaonaga huko nje wanapelekwa shamba, wengine wapishi humu ndani jikoni kule, wengine kutunza mifugo kwenye mazizi ya magereza na kadhalika.! Sasa Kaburu yeye kazi yake anazifanya ofisini kwa mkuu wa gereza!"

"Aisee! Ilikuwaje mpaka apangiwe kazi ya kibishoo hivyo? Na anafanya nini hasa uko ofisini?"

"Kuhusu alipataje hilo shavu la kushinda ofisini kwa mkuu wa gereza labda ukamuilize mkuu wa gereza mwenyewe.. Lakini kwa ninavyofahamu kazi anayoifanya huko ni kusidi kazi za kiofisi hasa nyaraka za wafungwa na mahabusu.!! Yani kwa mfano nyaraka za hukumu za wafungwa zikiletwa zinakuwa zimeandikw kingereza kwahiyo yeye anazichapa kwa kishwahili, au mahabusu wenye kesi kubwa wakiletewa mienendo ya kesi zao kutoka mahakama kuu pia inakuw kwa kibgereza na yeye anawasaidia kuzichapa kwa kiswahili au mfano wafungwa humu wakitaka kukata rufaa wanaandika rufaa zao na yeye anasaidia kuzichapa zikae kwenyw standard ya kiofisi! Hicho anachokifanya kila siku huko anakoshinda ofisini kwa mkuu wa Gereza" Godi akanifaanulia.

"Fuuuucck!! Kwa stahili hiyo inabidi nitafute namna ya kumfanya aisende huko ofisini kwa angalau hata siku tatu ili nipate mda mzuri wa kumshawishi aniambie ninachotaka"

"Na utafanyane hayo mazingaombwe kusafanya Kaburu asiende ofisini kwa siku zote Tatu hizo?"

"Inabidi kutafuta namna hakuna jinsi!"

"Sidhani kama……."

Nikamkatisha aisongee.

"Quite! I'm thinking!"

"Unazemaje?" Akaniukiza akiwa amekereka na kingereza changu kama kawaida.

"Nyamaza kidogo niwaze nini cha kufanya"

Hakusema chochote akakaa kimya tu. Yukawa tunatembea tembea pale yard tuko kimya kama mabubu.
Huu ndio ulikuwa wakati wa mimi kutumia akili zangu zote nilizojaaliwa tangu nazaliwa. Nikawaza na kuwaza kwa dakika kibao. Hatimae nikapata wazo.

"Yeeeesss! I got it.. Nahisi najua cha kufanya" nikamuambia kwa msisimko baada ya kuhisi nina wazo la kufanikisha kumuondoa Kaburu ofisini kwa mkuu wa gereza.

"Kitu gani" Godi akaniuliza kwa shauku.

"Subiri utaona! Hivi Sinyorita ana kesi gani humu?" Sikumjibu swali lake badala yake nikamtwanga swali langu.

"Ana kesi ya robbery!" Akanijibu

"Robbery?? Hivi Sinyorita anaweza kumtosha hata nzi??" Nikashangaa.

"Stori ndefu sana! Hebu nidokeze hicho unachokiwaza" Godi bado alikuwa na shauku kujua ninachokipanga kichwani.

"Relax! Utaona.. Unafahamu askari anayewapangia zamu za ulinzi maaskari magereza wenzake humu?" Nikamuuliza tena bila kumjibu swali lake.

"Askari flani hivi bishoo tunamuitaga Obama"

"Ndio yupi huyo" nikamuuliza.

"Ulipokuja naamini kuna chumba cha ofisi ulipelekwa kuandikisha taarifa zao? Ndio huyo jamaa mwenyewe!" Akanijibu.

Nikamkumbuka. Ni yule askari magereza mstaarabu aliyeniokoa na kipigo kutoka kwa askari mwenzake wakati nasachiwa kabla sijaingia humu.

"Ok ok! That's , gud.. Nisubiri hapa nakuja" nikamjibu huku naanza kuondoka.

"Unaenda wapi?" Godi akaniuliza kwa mshangao.

"Kuna jambo nataka kwenda kuongea na Obama!"

"Umechanganyikiwa au??" Godi akauliza kwa mshangao mkubwa sasa hivi.

"Nipe dakika chache narudi.! And hakikisha umemtafuta Sinyorita nikirudi nataka niongee naye" nikamjibu na kuondoka yard.

Godi akabaki ameduwaa tu ananiangalia ninavyoondoka. Nilitamani nimueleze nikichokipanga kichwani lakini ili nitekeleze kwa uzuri hiki nilichokipanga ni bora tukifanye akiwa haelewi ninacholenga aje kujua mwishoni baada ya kuona mtokeo ya mpango wangu kama ukifanikiwa.

Nikaelekea uoande ule wenye jiko amabo umeungana na ofisi.



EPISODE 14 NDANI YA DAKIKA CHACHE ZIJAZO..
 

VIPEPEO WEUSI: MKAKATI NAMBA 0034





EPISODE 14

(Mara ya kwana kupost hii Episodes kwenye group whatsapp baadhi walidhani kuna sehemu nimeruka au nimekosea.. Mzigo haujarukwa wala kukosewa.. endelea kusoma na kufuatilia utaelewa)







GEREZA KUU LA MOROGORO




SIKU YA PILI


Kengere ya kuashiria muda wa chakula cha mchana Ilikuwa imepigwa tayari na wafungwa na mahabusu walikuwa wanaondoka yard kuelekea upande wa gereza wenye jiko.

Wakati wenzetu wanaelekea jikoni kuchukua chakula mimi na Godi tulibakia yard namba mbili.

Tukasubiri kama dakika tano tukiwa peke yetu kabisa yard yote, kisha ndio tukamuona Obama, yule askari magereza mstaarabu akija pale tuliposimama.

"I really hope unajua unachokifanya la sivyo wote tutaongia kwenye matatizo" Obama akaongea huku ananikabidhu funguo.

"Usijali mkuu, kila kitu kitaenda sawa!" Nikamjibu huku napokea funguo kwa kuificha kiganjani na kuiweka mfukoni. "Msauzi umempanga lindo pale nilipokueleza?" Nikamuuliza.

Obama akaitikia kwa kichwa kisha akageuka haraka na kuondoka.

"Ray, ungenidokeza japo kidogo huu mpango wako labda inaweza kusaidia! Usisahaunkuwa nina uzoefu mkubwa wa jela kuliko wew" Godi akaniuliza kwa shauku huku tunatembea kuelekea yard namba moja.

"Tatizo ni kwamba nikikwambia hauwezi kukubaliana nao" nikamjibu huku natembea kwa haraka.

"Unasemaje????" Godi akahamaki. "Kama una uhakika siwezi kukubaliana nao maana yake huo mpango wa wa hovyo"

"Ni kweli ni mpango wa hovyo lakini Nina hakika utafanikiwa, na bora kuwa na mpango wa hovyo kuliko kutokuwa na mpango wowote" nikamjibu.

"Na Obama umefanikiwaje kumshawishi hicho ulichoenda kumshawishi mpaka amekubali kukuletea funguo!!"

"Nitakuambia usijali" nikamjibu kwa mkato huku bado tunatembea kwa haraka na tahadhari kuelekea yard namba moja.

"Unaonaje ukiniambia sasa?" Akaniukiza huku ananishika bega nipunguze mwendo.

"Shiiiittt!! Una mpango mwingine wowote wa namna gani tunaweza kumfanya Kaburu asitishe kwenda ofisini kwa mkuu wa gereza???" Nikamuuliza kwa kufoka huku namtazama usoni. Godi hakujibu chochote. Nikaendlea kuongea, "sasa kama huna plani yoyote, unaonaje ukiacha kubwabwaja na kuniuliza maswali na badala yake ufanye kile ninachokueleza?" Nikaongea kwa kufoka.

"Ok! Poa.." Akajibu kwa kifupi.

Tulikuwa tumeshafika yard namba moja, ambapo napo yard yote tulikuwa peke yetu, wafungwa wote na mahabusu wameenda kula.

"Ok! Selo ya Blaki iko wapi?" Nikamuuliza Godi.

"Selo namba 46, ile kule mwishoni" akanijibu huku tunatembea kuifuata selo ilipo.

"Una uhakika bangianazowauzia wafungwa anaziweka humu ndani??" Nikamuuliza tukiwa tayari tumefika nje ya selo namba 46.

"Nisingekuwa na uhakika nisinge kwambia! Blaki ni kama kiwanda humu ndani unaweza kukuta ana kete hata mia tano humo ndani" Godi akaongea.

"Ok!!" Nikajibu kwa kifupi huku nafungua kufuli kubwa la Chuma lilikuwa linaning'inia selo namba 46.

Nikalifungua haraka haraka kisha tukaingia wote wawili. Ndani ya selo kulikuwa na magoro matatu yamepangwa pembeni na upande mwingine kulikuwa na mabegi ya mgongoni kama matatu hivi na yote kwa muonekano wa haraka haraka yalionekana yalikuwa na nguo ndani.
Nikang'amua kwamba begi mojawapo kati ya hayo atakuwa ameficha misokoto yake ya bangi anayouza humu jela ila amechanganya na Nguo ili isionekane kwa urahisi. Hatukuwa na muda wa kusachi kwa hiyo tukayabeba mabegi yote matatu na kuondoka nayo.

Tukatoka nje na kuanza kuondoka.

"Umesahau kufunga mlango!" Godi akageuka na kunionyesha mlango ambao niliuacha wazi.

"Sijasahau! Nataka ubaki hivyo" nikaongea huku natembea kwa haraka.

Tukarudi tena yard namba mbili na mabegi yetu.

"Ok! Selo ya Bokela iko wapi?" Nikamuuliza huku napepesa macho huku na huku.

"Ile kule nayo iko mwoshoni namba 75" akanijibu kwa haraka na tukaanza kutembea haraka haraka kuifuata.

"Kwa hiyo hawa ndio madoni wa kuuza bangi humu jela" nikamuiliza tukiwa tunaikaribia selo namba 75.

"Ndio hawa! Wote ndio madoni wa bangi humu lakini Blaki ndio nyoko zaidi, ana wapambe karibia ishirini humu ambao ni kama misukule yake akiwaambia chochote wanatekeleza bila kuuliza! Bokela yeye kwa hesabu ya haraka haraka wapambe wake hawavuki kumi" Godi akaongea tukiwa tumefika nje ya sell namba 75.

"Ok naomba kibiriti!" nikaongea huku naweka mabegi chini nje ya selo namba 75.

"Nimepata kibiriti ila ujue kwamba kibiriti ni bidhaa adimu humu, so nilicbofanikiwa kupata ni hiki" Godi akaongwa huku ananikabidhi njiti moja ya kibiriti na kipande cha karatasi cha kibiriti ile sehemu ya kahawia ya kuwashia.

"Itatosha! Good job" nikavipokea

Tukaangaza macho huku na kule pale yard kuhakikisha hakuna aliyerudi kuona na kutubamba tukifanya hiki tunachokifanya.

Nikaanza kuiwasha ile njiti kwa umakini sana huku Godi amezungusha mikono kuzuia upepo usiizime pindi ikiwaka.

Hatimaye ikawaka na nikachukua karatasi kidogo pembeni na kuiwasha pia ili kupata moto mkubwa kisha nikaanza kuyaunguza yale mabegi kwa chini moja baada ya jingine.

Tulipoona mabegi yameanza kushika moto, tukainuka kwa haraka na kuondoka yard na kuyaacha mabegi pale pale nje selo namba 75.

Tukaelekea upande wa mbele wa gereza kule jikoni na kupanga foleni ya chakula.

Kwakuwa tulikuwa tumechelewa kuja huku kwahiyo tukajikuta tuko mwisho kabisa foleni. Lakini kitu kilichomshangaza Godi ni kwamba tuliyemkuta nyuma kabisa ya mstati kabla yetu alikuwa ni Sinyorita.
Godi akageuka kwa mshangao na kuninong'oneza.

"We mseng* umepanga nini kitokee?? Na huyu choko uliongea naye nini jana nilipokuitia?" Akauniliza kwa kuninong'oneza ili Sinyorita asisikie.

"Utaona ndani ya dakika chache! Relax" nikaongea huku natabasamu kwa wasi wasi.

Magereza mengi ya Tanzania hayana 'mesi' ya kulia chakula. Hivyo gereza hili la Morogoro walikuwa na utaratibu kwamba ukishachukua chakula unasubiri mpaka watu waishe kwenye foleni au kubakia kidogo kisha mnaeuhusiwa mrudi yard na vyakula vyenu mkale.

Wakati tunafika kwenye foleni kulikuwa na kama watu thelathini hivi, lakini sasa tulikuwa tumebaki kama kumi hivi.

Afande Msauzi akafungua geti na kuruhusu watu waanze kurudi yard wakalw chakula.

Dakika kama tatu baadae baada ya watu kuruhusiwa kurudi yard ambapo kwenye foleni tulikuwa tumebaki kama watu watano hivi, ghafla tukaanza kusikia kelele kubwa za kishindo zinasikika kutoka yard.

Zilikuwa kelele kubwa hasa kama vile watu wanashangilia au kama wako kwenye uwanja wa vita wanapambana. Kelele zilizidi kila sekunde zilivhokuwa zinasonga,n ghafla tukasikia askari magereza aliyepo yard anapiga filimbi ya kuashiria hatari. Kadiri filimbi ilivyokuwa inapigwa na kelele zilizidi kuwa kubwa zaidi.

Wale wenzetu tuliokuwa nao kwenye foleni wakasahau ghafla hata swala la chakula wakakimbilia yard kwenda kushuhudia kinachoendelea.
Kwahiyo kwenye eneo hili tulibaki mimi, Godi, Sinyorita, Msauzi na wapishi jikoni.

Filimbi ya hatari ilipulizwa kwa nguvu zaidi na kishindo cha kelele kilizidi kuwa kikubwa.

Ghafla akatokea askari magereza kutoka kwenye ule mlango wa kwenda maofisini alikuwa anakimbia huku amebeba bunduki begani anaelekea yard.

Alipopita tu pale mlangoni kunakoelekea yard, Msauzi akaniangalia. Nikampa ishara kwa kumuitikia kwa kichwa. Akafunga geti kisha na yeye akakimbia kwenda yard.
Kwa hiyo katika eneo hili kwa sasa tulibaki mimi, Godi, Sinyorita na wapishi wa jikoni.

Kama sekunde kumi baada ya yule askari mwenye bunduki kupita na Msauzi kumfuata, tukasikia mlio mkali wa risasi. Mlio huo mkali ulisikika kwa kishindo mara tatu. Risasi tatu zilikuwa zimepigwa hewani. Wote kwa haraka tukajirusha na kulala chini mikono kichwani.

Hiyo ndiyo ilikuwa protokali ya magereza Tanzania. Kukitokea hatari askari anaoiga filimbi ili mlale chini, kama msipotii basi zinapigwa risasi hewani.
Baada ya hapo askari anaruhusiwa kumpiga risasi mgungwa yeyote ambaye atakuwa bado amesimama.

Kwahiyo kwa haraka sana tukalala chini, mpaka wapishi kule jikoni nikawaona nao wamejirusha kulala sakafuni.

Nikaangaliana na Sinyorita na kumpa ishara kwa kichwa.

Sinyorita akainuka kwa haraka na kukimbia kwa kunyata kuelekea kule kwenye mlango wa kuingia kwenye maofisi ya magereza. Akapita mlangoni ambao ulikuwa umeachwa wazi na yule askari mwenye bunduki na akatokomea huko ndani kwenye maofisi.

Tukiwa tumelala chini pale pale Godi akanigeukia na kuniangalia kwa mshangao.

"Kumanina zako! Nishaelewa ulichokilenga" akaongea na kutabasamu.

Kama dakika tatu baadae Msauzi akarejea kwenye eneo hili lenye jiko na akaongea kwa mamlaka na kwa kufoka.

"Wafungwa, mahabusu wote kwenda yard namba moja!! Wote yard namba moja" akaongea huku anatembea.

Wote tuliokuwa hapa, mimi, Godi na wapishi tukainuka na kuanza kukimbia kuelekea Yard namba moja.

Zaidi ya mimi na Godi, hakuna mwingine aliyekuwa anajua kuwa Sinyorita ameingia kule kwenye maofisi.

Tulipofika yard namba moja tukawakuta wafungwa wote na mahabusu wamejaza kwenye eneo hili.

Kwa kawaida wafungwa wakiwa wametapakaa yard ya kwanza na ya pili unaweza kuhisi gereza lina watu wachache sana. Lakini tulipokuwa tumekusanywa hapa na kujazana ndio nikapata picha halisi jinsi tulivyo kuwa wengi.

Watu wote walikuwa wamekalishwa chini kitako.
Mbele kabisa ya yard walisimama maaskari kama watano hivi na yule mmoja mwenye silaha. Pembeni yao kulikuwa na watu kama kumi na tano wamepigishwa magoti na karibia wanane kati yao walikuwa wanavuja damu kutokana na majeraha kichwani. Hawa walikuwa ni Blaki, Kobelo na wapambe wao.

"It's namba kuanzia mwisho huko" askari mmoja akafoka.

Wafungwa wakaanza kuhesabu namba kwa kutamka kwa sauti.

Ilichukua karibia dakika kumi nzima zoezi hili la kuhesabu namba kukamilika.
Baada ya kukamilika yule askari akafoka tena.

"Haya anzia hapa mbele kwenda nyuma"

Tukaanza tena kuhesabu namba safari hii kuanzia sisi tuliokaa mbele na kushia kwa wale waliokaa nyuma.

Mara zote mbili hesabu iliyopatikana ilikuwa ni 314.

"Bado wafungwa wawili hawapo" afande mwingine aliyekuwa ameshika daftari na kalamu akaongea.

"Umejumlisha vizuri walioko nje shambani"

"Nimefanya hivyo mkuu, walioko shamba ni 22 nikiwajumlisha hapa bado watu wawili hawapo hapa" akaongea yule mwenye peni na karatasi.

"Nani hayupo hapa" yule askari mwingine akajliza kitemi kwa sauti ya juu.

Watu wakaanza kugeuka geuka kuangaliana usoni.

"Kaburu hayupo!!" Kuna mfungwa akaongea kwa sauti..

"Yes mjumlishe na Kaburu yuko ofisini" yule askari akaongea akiwa kama amekumbuka kitu cha wazi kabis walichokisahau Kumjumlisha Kaburu aliyeko ofisini.

"Nani mwingine" akauliza tena.

Watu wakaanza kugeukiana na kuaangaliana.

"Daudi hayupo" kuna mfungwa akapayuka.

"Daudi yupi?" Yule askari akauliza kwa shauku.

"Sinyorita" Yule mfungwa akapayuka tena.

Wale maaskari wakashtuka kidogo na kuangaliana.

"Kwahiyo Kaburu na Sinyorita hawapo hapa" yule askari akaongea kwa hasira.

Wakaangaliana tena na maaskari wenzake. Kisha maaskari wawili wakaondoka kutoka pale yard na kuelekea kule eneo la jiko.

Yard ilikuwa kimya kabisa. Godi alikuwa anageuka na kuniangalia kisha anatabasamu kichini chini.

Tulikaa tukiwa tumetulia vile karibia robo saa nzima.

Mara tukaona watu kadhaa wameongozana wanaingia Yard.

Mbele alikuwa ametangulia mkuu wa gereza na pembeni yake kulikwa na maaskari wawili. Nyuma yao walikuwa ni Kaburu na Sinyorita ambao nyuma yao nao kulikuwa na maaskari wengine wawili.

Walipoingia pale yard wafungwa wote na mahabusu tukashikwa na mshangao mkubwa hatukuamini tulichokuwa tunakiona.
Au niseme wengine wote isipokuwa mimi walishikwa na mshangao.

Sinyorita alikuwa ameletwa yuko uchi wa mnyama ameshikilia nguo mkononi.

Walipofika pale mbele maaskari wote wakapiga saluti, kisha wakasogea pembeni kumpa nafasi mkuu wa gereza azungumze.

Kaburu na Sinyorita wakapiga magoti baada ya kukuta wenzao wengine akina Blaki waliokuwa pale mbele wamepiga magoti.

"Simameni hivyo hivyo msipige magoti nataka wenzenu wote wawaone mashetani nyinyi" Mkuu wa gereza akaongea kwa hasira.

"Naona mmeanza kutupanda kichwani sasa!" Akaongea mkuu wa gereza huku anatuangalia wafungwa wote na mahabusu.

"Yani mnaingiza taharuki kwenye gereza langu kwa kugombea misokoto ya bangi??" Akaongea kwa hasira na kutoa macho.

"Naona mmejisahau kuwa mko gerezani labda tumewapa Uhuru sana ndio maana. Sasa kesho asubuhi hakutakuwa na mazoezi badala yake tutafanya msako wa selo kwa sell, ole wako tukukuta na bangi, ole wako tukukute na sigara, ole wako tukukute na ugoro, ole wako tukukute na kisu, ole wako tukukute na begi limejaa Nguo!! Nasema ole wako tukukute na kitu chochote tulichokikataza." Mkuu wa gereza akahutubia kwa hasira.

"Na wewe Blaki umeshakuwa kero humu gerezani, kuanzia kesho akuweka solo mpaka utakapobadilika" akaongea huku anamuangalia Blaki na wapambe wake.

Baadae nilikuja kuelewa kuwa aliposema anamuweka 'Solo' alimaanisha kuwa atamuweka kwenye "solitary confinement". Ni ile sehemu yenye selo zilizojitenga ambazo Godi alinieleza kuwa huwa wanawekwa mahabusu na wafungwa 'maalum'.

"Sasa kwa kuwa nyinyi mnajifanya vidume, mimi nitawaonyesha ni kidume zaidi yenu wapumbavu nyinyi" akaongea huku anatuangalia wafungwa wote na mahabusu.

"Kaburu nilikupa heshima sana ndio maana nikakupangia kazi ofisini mwangu! Lakini unathubutu kuingiza mashetank wenzako ofisini kwangu ili mfirane!! Ofisi yangu mimi, ofisi yangu mnatumia kufirana, ofisi yangu mimi.!!" Mkuu wa gereza akaongea kwa hasira na hisia huku anapiga piga kifua.

"Afande nataka hawa mashetani wote! Kuanzia hawa waliokuwa wanafirana, na hawa waliokuwa wanagombea bangi.. Nataka muwapeleke ofisini kule mpige virungu mpaka wajute kuzaliwa! Mkimaliza hawa mbwa Blaki na wenzake wafungieni 'solo' kule na huyu firauni Kaburu nataka kuanzia jumatatu aanze kwenda shamba simuhitaji tena ofisini kwangu" akaendelea kuongea kwa hasira.

Nikajikuta natabasamu niliposikia maneno "simuhitaji tena ofisini kwangu"!! Nikajipongeza, 'goal achieved' nikajisemea kimoyo moyo.

"Saa ngapi hapo" akamuuliza askari wa pembeni yake.

"Saa nane na robo Mzee" askari akajibu kwa heshima.

"Sasa nadhani mlikuwa mnakula, lakini kutokana na ujinga huu mlio ufanya nahairisha kila mlichokuwa mnakifanya na mtafungiwa selo sasa hivi saa nane mlale badala ya saa kumi" akaongea kwa hasira kubwa na kumalizia, "vijana msitake kunijaribu, mimi sijaribiwi! Mtaiona jela chungu"

Akamaliza na kuanza kuondoka.

"Kaba seloooo" askari mmoja akapayuka kitemi.

Wote tukaanza kuinuka kwa unyonge tumelowa kama tumemwagiwa maji ya barafu.

Tukaongozana na Godi kuelekea selo yetu namba mbili kubwa.

"Kumamae wewe msenge ni kichwa!! Saluti" akaninongoneza kwa kufurahi.
"Kwahiyo nini kifuatacho ITV??" Akaniliza kwa shauku.

"Well, tumeshafanikiwa kumuondoa ofisini kwa mkuu wa gereza! Lakini umesikia pale ameamuru kuwa jumatatu aanze kupelekwa shamba. Maana yake ni kwamba tuna siku ya kesho ijumaa, jumamosi na jumapili!! Tuna siku tatu tu kuhakikisha tumeongea nae na ametupatia taarifa tunayohitaji" nikaongea kwa sauti ya chini huku tunatembea kuelekea selo.

"Woooww!! Daaahh nilikuwa nakuchukulia poa sana.. Kumbeee daaahh! Sakuti aisee!" Akaongea kwa utani huku ananipigia saluti.

Nikatabasamu tu. Sikusema chochote.
Siku hii ya pili imeisha kwa mafanikio. Nina siku tatu mbele yangu kuhakikisha nakamilisha 'mission' iliyonileta humu.
Nikajipa moyo. 'Inyeshe mvua, au liwake jua' lazima kieleweke.


TUKUTANE IJUMAA KWENYE EPISODE 15..


The Bold
 
NEW EPISODES (EPISODE 13 & 14) POST # 3310 & 3311





Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu Charmie DON SINYORI mij adden
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom