Viongozi wa kiislaam Dar, walaani kuuawa kwa Gaddafi

mshikachuma

JF-Expert Member
Dec 2, 2010
2,853
626
Viongozi wa dini ya kiislaam mkoa wa DSM wamelaani mauaji ya canar Ghadaffi.
Wamesema Ghadaffi amejanga misikiti mingi sana barani Africa ikiwamo Tanzania.
Pia wamesema pale Dodoma Ghadaffi amejenga msikiti mkubwa sana wa kiistoria.
Na mwisho wamesema Ghadaffi alikuwa mbioni kujenga chuo cha kiislamu ndani ya Tanzania.

Source - Channel ten...taharifa ya habari ya saa moja leo jioni
 
kwani maendeleo ni MISIKITI TU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Kwa watanzania ni lazima tukumbuke na ubazazi aliotufanyia kwa ndugu zetu kule KAGERA kwa kumsupport IDD AMIN. Amevuna alichopanda, miaka 42 madarakani kwani hiyo Libya ni mali ya Walibya na sio Gaddafi, wenye nchi wameichukua, aliwadharau kwa kuwaita mende na panya, sasa mende na panya wamemshughulikia. FUNZO KWETU NI KUWA USITUKANE WANANCHI
 
kwani maendeleo ni MISIKITI TU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Kwa watanzania ni lazima tukumbuke na ubazazi aliotufanyia kwa ndugu zetu kule KAGERA kwa kumsupport IDD AMIN. Amevuna alichopanda, miaka 42 madarkani kwani hiyo Libya nimali ya Walibya na sio Gaddafi, aliwadharau kwa kuwaita mende na panya, sasa mende na panya wamemshughulikia
Kwahiyo unataka kuniambia mende wamedondosha kabati la nguo?
 
Pia katika tamko lao kuna sheikh mmoja alimnukuu Ghadaffi kwa kusema....tafadhalini wanangu msiniuwe,tafadharini watoto
wangu msiniue....lakini watoto wale wakamuua baba yao kwa ukatili sana! kwahiyo kwa kauli ile ya Ghadaffi yaonyesha Ghadaffi
alikuwa ni mtu wa mungu! 'mwisho wa kumnukuu sheikh'
 
si tanzania tu viongozi afrika hawakipenda pamoja na membe,25 asilimia ya budget ya african union ni gadaffi si waislam tu walosikitika.tatizo wengi tunachukia waarabi na kupenda wazungu.biashara ya utumwa waatabu walikuwa middle man wanunuzi wazungu.pesa alizoleta gadafi afrika zinahamia ulaya
 
punguzeni kuhubiri dini, just send a fair and brilliant comment. Plz ila kiukweli kisa kajenga msikiti! Lets defend GADDAFI kwa mengi sana though as a humanbeing lazima alikuwa na mapungufu.

Angalizo;

Kifo cha G Kisichukuliwe kidini zaidi though inaruhusiwa kumkumbuka marehemu ila kiafrika zaidi jamaa ni waukweli, wapi mwingine tutampata ataekataa kuwapa gesi, mafuta, uranium, gold na precious metals like nickel Na bila kusahau TANZANITE.

Apumzike kanali wa afrika. Angalizo; ubaya wa marehemu hauongelewi wakati wa msiba. Nadhani hata mlioko ughaibuni mtakubaliana na hilo. Rip G.
 
Kwa nini hawakulaani wakati watu wa Benghazi walipokuwa wanauliwa? Au hawakuwa waislam?

Hawa viongozi wanatakiwa watambue kuwa hela zilizotumika kuwajengea misikiti sio za Ghadaffi wala baba yake Ghadaffi, ni hela za watu wa Libya wakiwepo wale waliokuwa wanakejeliwa na kuitwa 'rats' na Ghadafi mwenyewe. Ni aibu kwa kiongozi yeyote kulaani mauaji ya Ghadafi kwa sababu alijenga misikiti! Hawa viongozi walitakiwa watoe sababu nyingine ya 'muhimu' na sio kuongelea 'material gain' tena zilizotoka kwa wananchi waliokuwa wananyanyasika kwa miaka 42!

Pili, kama hawa viongozi wa dini wamekuwa wafuatiliaje wazuri watakuwa wamewasikia watu wa Libya wakisema 'categorically' kuwa vita yao si kama wanataka nyongeza ya mishahara, allowance za nyumba na posho zingine, wanachopigia ni 'freedom'. Na wamepata freedom (in whatever form) kwa damu maana wamekufa watu kwa maelfu wakipigania haki ya msingi kabisa kwa kila mwanadamu ya kuwa huru.

Ujumbe muhimu naonpata toka kwa hawa viongozi watu wanaolaani mauaji ya Ghadafi ni kuwa hawako huru "kifikra". Akili zao zimeganda kwenye kwenye material gains. Kumpenda mtu kwa sababu tu kakujengea nyumba ni utumwa wa hali ya juu, na hiki ndicho watu wa Libya (tena waislam) wamekataa kwa gharama kubwa (life). Waige mfano wa watu wa Libya na kutambua kuwa utu wa mtu hautokani na mali au majengo bali uhuru wake wa kuishi maisha anayotaka na kutimiza ndoto zake kulingana na talanta aliyopewa na mwenyezi mungu.

Hawa viongozi wanatia doa. Yes, kifo cha Ghadafi kama binadamu yeyote ni huzuni, lakini Ghadafi alikuwa na every opportunity ya kuachia ngazi na kuepusha hii kadhia.
 
Pia katika tamko lao kuna sheikh mmoja alimnukuu Ghadaffi kwa kusema....tafadhalini wanangu msiniuwe,tafadharini watoto
wangu msiniue....lakini watoto wale wakamuua baba yao kwa ukatili sana! kwahiyo kwa kauli ile ya Ghadaffi yaonyesha Ghadaffi
alikuwa ni mtu wa mungu! 'mwisho wa kumnukuu sheikh'
Hizo ni mbwembwe tu za mashehe ubwabwa kwani yeye kaua wangapi zile silaha alizokuwa anagawa mitaani kama njugu alifikiri anagawa mishumaa.
 
Kama Mungu atamlaza pema Gaddafi basi hakuna atakayekwenda motoni labda Hitler.
Duuh! mkuu unamajibu ya kukata maini wewe!!!!....na kama Gadaffi ataingia peponi,na kwanini Hitler asiingie? wote si binadamu?
 
Unajua nyie hamjui kuwa yesu ni Muislamu..

Sasa tunampapatikia nini wakati ni mwenzetu..

Kuhusu Qadafi watazaliwa wengi mkuu..hata yesu aliua na roman empire kwa kushirikiana na wayahudi (walitaka kumuua)

Yesu ni mwislam? hayo maneno ungeyasema saudi arabia kichwa chako ni halali yao, muulize yule mcheza mpira aliyemchora Yesu kwenye mkono wake au mtu yeyote aliejaribu kuingia saudi arabia na bilblia kwenye begi lake.

Huko ni rahisi kuingia na cocaine au bangi lakini siyo bilblia mkuu, sasa kama huyu Yesu ni mwislam kwa nini hakuna ruksa nchi za kiislam kutaja jina lake wala kusoma biblia au kujenga kanisa au kuvaa alama ya msalaba?

Ilikuwaje kule Turkey TV ya kikiristo ikavamiwa na watangazaji kuuwawa? Au pakistan vipi wale wanaomwamini huyu Yesu mwislamu wanauawawa hata waziri wa serkali aliyetoa hoja za kuwatetea pia akauawa na sasa umma wa kiislam unataka muuaji aachiwe huru ?

Vipi kule iran yule mchungaji anaetakiwa kuuwawa kwa kuwa mkristo. Bila kusahau misri ambapo mauaji ya wakiristo yanafanywa waziwazi na waislam, umewahi kuona nigeria jinsi waislam wanavyo chinja wafuasi wa huyu Yesu mwislam au Somalia ambapo alshaabab wana landa landa kila mahali kumbaini mfuasi yeyote wa Yesu mwislam ili achinjwe kwa ncha ya upanga? Yapo mengi tu yanayoonyesha kuwa Yesu ni adui namba moja wa uislam na kamwe yeye mwenyewe hawezi kuwa mwislam.

Mkuu uislam ni hadaa tangu mwanzo wake hadi mwisho wake, jaribu kuangalia mwenendo mzima wa dunia hivi sasa, shetani anaua bali Mungu anaokoa, utapata jibu. Hujachelewa bado jipe moyo Yesu yu hai na anakuita, ukifungua mlango wa moyo wako yeye ataingia na atakula pamoja nawe.
 
Back
Top Bottom