Vilivyo chosha kuvisikia 2013...

Vilivyo chosha kuvisikia 2013...

Wengine tumechoshwa na ..
  • Foleni barabarani, hili ni moja ya majanga ya taifa, pamoja na
  • UZEMBE WA DAWASCO
  • UZEMBE TANESCO
  • SUMATRA
  • Customer Services kwenye mashirika na kwenye makampuni..
  • CHADEMA kujizoretesha na maugomvi yasiyo na mwanzo wala mwisho (CCM itapeta tena kiulaini)..
  • Kwetu CCM bado kuna uzembe, rushwa na kutokuwajibika...
  • Kila kitu kumlalamikia JK, kwanini lawama karibu zote hawabebi walio chini yake?!
  • Elimu duni bado kwa watoto wetu na vijana..
  • Huduma za afya duni kabisa, ebu tugangamae 2014..
  • Ustawi wa jamii uborereshwe kwa watoto wote, yatima na walio na wazazi, kwa kina mama na vikongwe..
  • Ukosefu wa ajira na kuwasaidia wasio na ajira...
  • Kutokua na msaada kabambe na wa ukweli kwenye ujasiriamala...
  • ----
 
pia nimechoka kulipwa mshahara nataka nipewe posho kila ninapoenda kazini kama posho za wabunge na si kusubiri mwisho wa mwezi, siku nisipokuja kazini nisipewe posho.
Hii njia ya kulipa posho hutumiwa na makampuni yanayokwepa kodi kwa srikali
 
yaani namaanisha kabisa, lazima nitoke na kampuni at any cost any how, kazi zimekuwa za majungu na mbaya zaidi mimi na wizi ni mbalimbali ambapo ninapoingia kazini (kazi mpya) it doesn't take a month kujikuta nina bunch ya maadui kisa sipigi au siruhusu watu kupiga.


You are not alone,trust me
 
me nimechoka upendeleo unaofanyika chitchat kiasi kwamba wageni hatupati nafasi

nimechoka kuona avatari za uongo na kweli natamani kila mtu aweke picha

nimechoka magari kuishia posta mpya badala ya feri

nimechoka makonda kutulipisha nauli ya buku watu wa kimara kila ifikapo jioni

nimechoshwa na maralia sugu

nimeshoshwa na ahadi ya mpenzi wangu kusema atanioa mpaka atakapokusanya mahari ya em tano
 
1.nimechoka kusikia radio ya wafu
2. nimechoka kusikia story za lowassa na urais
3. nimechoka kusikia harambee za lowassa.
 
me nimechoka upendeleo unaofanyika chitchat kiasi kwamba wageni hatupati nafasi

nimechoka kuona avatari za uongo na kweli natamani kila mtu aweke picha

nimechoka magari kuishia posta mpya badala ya feri

nimechoka makonda kutulipisha nauli ya buku watu wa kimara kila ifikapo jioni

nimechoshwa na maralia sugu

nimeshoshwa na ahadi ya mpenzi wangu kusema atanioa mpaka atakapokusanya mahari ya em tano


ya Feri we utakuwa unafanya kazi ardhi nahisi
pole sana
chit chat muone mwenyekiti Baba V ....
shida yako imeisha
 
Last edited by a moderator:
Diamond Penny na Wema nilichoka kuwasikia habari zao!!!!!

wanaume kuwaua wapenzi wao nadhan this year ilikuwa juu
hasa baada ya ishu ya Ufoo

Nimechoka na wewe maana unanilingia sana, naamia kwa King'asti 2014
 
ya Feri we utakuwa unafanya kazi ardhi nahisi
pole sana
chit chat muone mwenyekiti Baba V ....
shida yako imeisha

ok [\The Boss] nitamuona

kuhusu feri sio mimi ninaeteseka ila nawaonea huruma kina mama wachuuzi wa samaki wanatembea kutoka posta hadi feri tangu kituo kisimamishwe
 
Last edited by a moderator:
ok [\The Boss] nitamuona

kuhusu feri sio mimi ninaeteseka ila nawaonea huruma kina mama wachuuzi wa samaki wanatembea kutoka posta hadi feri tangu kituo kisimamishwe


hao wamama wachuuzi ungewajua walivyo na makusudu kwa wafanyaki njia hiyo
na kuwapaka wenzao shombo usingewaonea huruma
 
Nimechoka mwaka huu kupokelea mshahara dirishani nataka kila ya tarehe 25 iwe x-mas.
Nimechoka kuambiwa payrole toka hazina haijafika.
Nimechoshwa na mchina wangu asiyetoa LIKE JF.
Mungu nisimamie 2014 yote yaliyonikosesha Amani 2013 yasitokee tena.
 
nimechoka na kazi za kuajiriwa 2014 lazima nifungue kampuni yangu hata kama ni ya kuuza maji ya viroba
Natamani nikukumbatie.ahsante sana.kwa heshima yako nalog off jf.ili hii iwe comment yangu ya mwisho kuisoma jf kwa mwaka huu.
 
ha haaa, mdogo wangu snowhite, naona hata mimi karibu nitaacha kwenda harusini sababu ya kwaito...... nimeichoka mwili na moyo, lol!
nimechoka kuona watu wanateteana kwa mambo yasiyofaa kijamii, kisa tu eti kila mtu na maisha yake.....
 
Last edited by a moderator:
Hivi mtu anaweza kubuni jina jipya tumpatie PM? Na pia inawezekana tumfanyia cosmetic surgery ili hata sura iwe nyingine?

Na kuna yule waziri wa mambo ya MU badala ya MMU ambaye full time anachapa usingizi...Hivi tunaweza kum-export mahali?
 
Nimechoka kusikia ulalamishi wa wanaume juu ya wanawake na pesa.

Nimechoka kusikia hamasa za ufirauni

Ningefurahi kama watu wangechuja impact za mabandiko yao kwa younger generation hata kama ni ukweli.

Ningependa kuona habari zaidi za uchunguzi kuliko upambe wa magwanda vs magamba

Ningependezwa na umakini zaidi na uneutral wa moderators na jf owners.

Ile kauli ya 'where we dare to speak' ingekuwa reflected kama zamani.

Nitarudi na mengine zaidi.
Thanks The Boss for this useful post.
 
Last edited by a moderator:
Mie nimechokakuchezewa sharubu na vibinti vya hapa JF hususan vile vinavyokesha MMU na Chit Chat, nawatangazia hali ya hatari mwaka 2014, nitaanza kufanya kweli............. Nitavicharaza na henzerani!
 
hao wamama wachuuzi ungewajua walivyo na makusudu kwa wafanyaki njia hiyo
na kuwapaka wenzao shombo usingewaonea huruma

hahahahahahahahaha tatizo wafanyakazi wengine wana nyodo mno kujiona wako juu ndo mana yanawakuta
 
Back
Top Bottom