Nimechoshwa na mengi sana naanzia mazingira ya mtaani kwetu:
nimechoka hizi habar za kufuatiliana maisha mwache mtu aishi atakavyo sio utakavyo wewe.
nimechoka habar za kudharauriana kwa kile alichonacho mtu, wakati mwingne hata hujamkosea mtu anakudharau na kukutema mate hii sio tabia njema.
Nimechoka na sipendi kuona malumbano ya wanandugu na hizi extended family nimezichoka naomba mungu ktk maisha yangu yajayo yasitokee haya yanayotokea sasa.
Sipendi kunyooshewa vidole na ushirikina hasa ukimjua anayekuwekew uzibe ktk maisha yako daaa kwa kweli unaweza tenda dhambi (kuua).
Kwa upande wa humu JF.
Sipendi matusi wala malumbano ktk thread.
Sipendi kauli ya kueka picha maana saiv ishakuwa kero kila mtu anataka picha kama ni hivyo basi atafutwe camera man wa JF awe anazunguka kutafuta picha za matukio unayoyataka( sijui kama mtaweza kumlipa).
Nimechoka kuona dharau humu na kejeli ktk topic anayoanzisha mtu, wakati mwingne mtu anakuwa yuko seriously na tatizo lakin anapokea matusi badala ya ushauri.
Nimechoka topic hizi Natafuta mchumba, habar za punyeto,sijui zile za namna ya kumlidhisha mpenzi, mara habari za kuachwa, kufumaniwa na nyingne nyingi zinazochosha kwa kweli ktk topic tujirekebishe na kujitahidi kusearch topic ili kujifunza huko sio kurudiarudia na hili linachangiwa sana na wageni humu ndani.
Looo!!! Yapo mengi mengne ntaendelea badae kabla mwaka huu hujaisha.