Mbinu hizi zinapunguza utapeli sio full proof guarantee, kila muda zinagunduliwa mpya
Hapa niameorodhesha baadhi ya tahadhari za kuchukua ili kuliepuka hilo:-
01. Usiwe na haraka kwenye kufanya muamala, haijalishi mteja atakuwa na haraka gani. Mruhusu aondoke kama anaonekana ana haraka, kwa sababu katika namna nyingi watu wengi wametapeliwa kwa sababu matapeli wengi wanaonekana wana haraka.
02. Usitoe hela kabla ya kuona meseji kwako, na Usiweke hela kabla ya kupewa hela na kuzihakiki.
03. Kama ukimrudishia mteja hela, akakurudishia zihakiki hela tena, uhakiki ina maana ya kuzikagua idadi na thamani yake.
04. Usimfanyie mteja muamala kwenye simu yake, muamala wa mteja hufanywa na mteja.
05. Kwa namna yoyote ile usimpe simu ya wakala mtu yeyote aidha kuweka namba au kuhakiki meseji kama imerudi. Utampa mwanya wa kupigwa.
06. Usihudumie wateja zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Weka utaratibu wa kuhudumia mteja mmoja baada ya mwingine.
07. Kwa mawakala wa AIRTEL, hakiki meseji kwenye simu ya mteja, kwa sababu kuna wakati huchukua namba na kuwatumia watu walioko mbali na eno lako, kisha wanaripoti kukosea muamala.
08. Kama kuna watu zaidi ya mmoja wametoa pesa kwa wakati mmoja, usiulize nani katoa shingapi! Muulize jina, kisha omba simu yake angalia kiasi alichotoa kama kinaendana na jina lake. Hapa kuna mchezo, wanakuja wawili wanatoa, halafu mmoja anajifanya anaongea na simu, yule mwingine anachukua hela ya huyu anayeongea na simu, akishaondoka huyu wa simu anakuja kuchukua hela na ana meseji kamili utafanyaje?
09. Usimuamini mtu yeyote, usitume pesa kwa boss wako kwa sababu amekutumia meseji! Mpigie kuhakiki kama ni yeye au lah!
10. Mtoa huduma wa simu atakupigia kukuliza kama muamala unaoombwa kurudishwa ni halali na kwamba haukumhudumia, hawatakuuliza salio, wala ni nani kafanya muamala wa shingapi! Kuwa makini na hawa watu! Mtoa huduma atakupigia kwa namba 100 TU.
Ukipokea simu yoyote mbali na 100 ikidai ni mtoa huduma, hao ni matapeli.
11. Ikiwa huna uhakika na muamala kama umeufanya au lah, unaweza kumuomba mtoa huduma akupe muda kidogo kuhakiki kama umefanya muamala huo au lah! Na utakapojiridhisha unaweza kuruhusu au kukataa.
12. Usitumie namba ya wakala kwa mawasiliano binafsi ni HATARI.
13. Usimtajie mteja float/cash uliyonayo endapo kiasi anachotaka hauko nacho. Kuna wateja wanafika wanataja hela kubwa wakitaka kujua unashingapi! Sasa mtu amekwambia anaweka milioni 1, halafu unamwambia hauna, anakuuliza una shingapi! Inahusu nini wakati hata ukimtajia haitafika milioni moja.
14. Tunza vizuri simu za uwakala, na fedha zako. USIRI NI MUHIMU.
Ahsante..
15. USIWE NA HARAKA KUFANYA MIAMALA, NI VIZURI KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA LAKINI WAKIJA NA HARAKA WARUHUSU WAENDE.
Unaweza kuongezea mbinu nyingine................
Hapa niameorodhesha baadhi ya tahadhari za kuchukua ili kuliepuka hilo:-
01. Usiwe na haraka kwenye kufanya muamala, haijalishi mteja atakuwa na haraka gani. Mruhusu aondoke kama anaonekana ana haraka, kwa sababu katika namna nyingi watu wengi wametapeliwa kwa sababu matapeli wengi wanaonekana wana haraka.
02. Usitoe hela kabla ya kuona meseji kwako, na Usiweke hela kabla ya kupewa hela na kuzihakiki.
03. Kama ukimrudishia mteja hela, akakurudishia zihakiki hela tena, uhakiki ina maana ya kuzikagua idadi na thamani yake.
04. Usimfanyie mteja muamala kwenye simu yake, muamala wa mteja hufanywa na mteja.
05. Kwa namna yoyote ile usimpe simu ya wakala mtu yeyote aidha kuweka namba au kuhakiki meseji kama imerudi. Utampa mwanya wa kupigwa.
06. Usihudumie wateja zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Weka utaratibu wa kuhudumia mteja mmoja baada ya mwingine.
07. Kwa mawakala wa AIRTEL, hakiki meseji kwenye simu ya mteja, kwa sababu kuna wakati huchukua namba na kuwatumia watu walioko mbali na eno lako, kisha wanaripoti kukosea muamala.
08. Kama kuna watu zaidi ya mmoja wametoa pesa kwa wakati mmoja, usiulize nani katoa shingapi! Muulize jina, kisha omba simu yake angalia kiasi alichotoa kama kinaendana na jina lake. Hapa kuna mchezo, wanakuja wawili wanatoa, halafu mmoja anajifanya anaongea na simu, yule mwingine anachukua hela ya huyu anayeongea na simu, akishaondoka huyu wa simu anakuja kuchukua hela na ana meseji kamili utafanyaje?
09. Usimuamini mtu yeyote, usitume pesa kwa boss wako kwa sababu amekutumia meseji! Mpigie kuhakiki kama ni yeye au lah!
10. Mtoa huduma wa simu atakupigia kukuliza kama muamala unaoombwa kurudishwa ni halali na kwamba haukumhudumia, hawatakuuliza salio, wala ni nani kafanya muamala wa shingapi! Kuwa makini na hawa watu! Mtoa huduma atakupigia kwa namba 100 TU.
Ukipokea simu yoyote mbali na 100 ikidai ni mtoa huduma, hao ni matapeli.
11. Ikiwa huna uhakika na muamala kama umeufanya au lah, unaweza kumuomba mtoa huduma akupe muda kidogo kuhakiki kama umefanya muamala huo au lah! Na utakapojiridhisha unaweza kuruhusu au kukataa.
12. Usitumie namba ya wakala kwa mawasiliano binafsi ni HATARI.
13. Usimtajie mteja float/cash uliyonayo endapo kiasi anachotaka hauko nacho. Kuna wateja wanafika wanataja hela kubwa wakitaka kujua unashingapi! Sasa mtu amekwambia anaweka milioni 1, halafu unamwambia hauna, anakuuliza una shingapi! Inahusu nini wakati hata ukimtajia haitafika milioni moja.
14. Tunza vizuri simu za uwakala, na fedha zako. USIRI NI MUHIMU.
Ahsante..
15. USIWE NA HARAKA KUFANYA MIAMALA, NI VIZURI KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA LAKINI WAKIJA NA HARAKA WARUHUSU WAENDE.
Unaweza kuongezea mbinu nyingine................