R-K-O
JF-Expert Member
- Jun 27, 2023
- 482
- 2,138
Habari zenu wakuu,
Mimi ni kijana muajiriwa na pia ni mfanya biashara
Katika biashara yangu huwa napenda sana kuiendesha kwa kuongezea vitu vya darasani, kuna hii system nataka niitumie ya kutenganisha pesa za mauzo mfano ya kwa siku, baada ya siku kadhaa, kwa wanaolipa madeni, kulingana na wateja, n.k..
Sasa nilipata wazo ninunue vikontena na vimfuko vigumu vya plastiki nikajaribu ila napata wakati mgumu kuziingiza pesa kwa mpigo
Shida kwenye hivi vikontena na vifuko nikijaribu sana inaingia milioni 2 tu, mbaya zaidi unakuta jioni kuna milioni 3 hadi 6 kwahio inakuwa changamoto kweli kweli
Ni wapi naweza kupata contena ama vifuko vigumu kwa saizi nayaotaka mimi ili pesa ikiingia iwe inabaa vizuri na kusiwe na nafasi ya ziada, makontena ya vyakula nimejaribu ila yanaacha nafasi.