Kusikiliza mazungumzo ya watu kwa hila ni tabia mbaya.
sorry kweli nimefanya tabia mbaya nilijitahidi kujizuia nikiwa nimekonsentreti na kitabu changu lakini kadiri walivyokuwa wakiongea ndipo masikio yangu yakawa wazi kwao kuwasikiliza, ingekuwa macho ningefumba.........sasa maskio hayana kifunikio........
Nauliza tuu wanajamvi pengine kunawanajamvi wanapitia tatizo kama hili je ni sawa kuflash ukimaliza haja zako flash uziache kwa anayekuja aone mmeng'enyo wa vyakula ulioushusha?
Sasa ukutane na mie, nimekulia Sangabuye, hatukuwa na choo ni mwendo wa kukata gogo porini afu unaji-'shenena chini'
Unaniambia nikisaidia haja ndogo ni-flush? si nitakushangaa? Ila ukinifundisha taratibu nitaelewa tu, kuwa mkojo unaleta harufu mbaya chumbani.
Kiranga umechangia vizuri sana kwenye 1 na 2 ila hapo nilipoweka green umeniacha hoooiii kwa kucheka hahahahahaaaaa, usishangae inawezakuwa havichekeshi ila mie napenda kucheka kuliko kula loooh. Thanks.Yeah,
Hilo ni jambo la jakamoyo lenye kizungumkuti, kwani si kama umetaka kuingilia ila mambo yametokea yenyewe, kwa kadiri ya maelezo.
Sasa basi, maadam yameshatokea na wewe mshawasha wako haukuishia kusikiza tu, bali kama binadamu mwenye utashi umetaka kuwasilisha, na mimi kama binadamu mwenye utashi nawasilisha.
1. Mashoga mnapendana sana, lakini mambo mengine ya ndoa kuwasilisha kwa mashoga mwiko. Mume ni mwandani na msiri wako. Kama mna matatizo kuna namna za kuyamaliza na vikao vyake, na watu maalum wa kuwashirikisha. Kutoa habari za ndani kwa mashoga sijui mume wangu ha flashi choo kunamshusha hadhi mumeo. Mumeo akishuka hadhi na wewe mwanamke umeshuka hadhi kwani mume ni luba la maisha. Hata mkiachana atabaki "alikuwa mume wako". Utamuhadithia shoga mapungufu ya mumeo mangapi? Kesho keshokutwa ukikwaruzana na shoga akaenda kukutolea siri zako za ndani "mumeo mchafu hajui hata ku flashi" utasemaje?
2. Sijaona maelezo yoyote kama mke kamuuliza mume. Na kwa kweli umesema kwamba kwa kadiri ya habari ilivyo mke hajamwambia mume kuhusu kero hii. Hapa kuna tatizo kubwa kuliko ku flush vyoo na lisipotatuliwa ndoa hii haina mustakabali mzuri. Kwa nini mke ajisikie huru kumueleza habari shoga yake na asijisikie huru kumueleza mume wake? Nani kala viapo vya ndoa hapa? Shoga au mume? Kwa nini mke hamuamini mume? Mana hili ni suala la kuaminiana. Ina maana mke akimuambia mume kwamba "Bwana, umesahau kuflush". Halafu aangalie kama atasahau tena itakuwa tusi? Kuna tatizo la mawasiliano? Mke anamuogopa mume? Mke anajishtukia kwamba yule mume aliyemchagua wakati wa uchumba si huyu wa wakati wa ndoa?
Ni muhimu kuwa wazi. Mke asipokuwa muwazi atajulikana. Na hatimaye mwanamme anaweza kuona kitu hakiko sawa akafikiri mke kapata bwana nje tatizo likawa kubwa zaidi.
Kumbe kisa ku flashi choo tu!
Wakati hatujui hata kwa nini mume ha flashi choo. Inawezekana ni mwanamazingira kama Hugo Chavez au "mashikolo mageni" tu!
Kuna wengine kutokana na shida ya maji, wanaflash tuu pale wanapokitumia choo kwa haja kubwa. Unajua flash moja inatumia lita ngapi za maji?
Halafu kuna mtindo wa baadhi ya akina dada wanajifanya eti wanaenda chooni kumbe anaenda kujiangalia tuu kwenye kioo au kusoma message kwenye simu yake, halafu anaflash choo as if amekitumia.
Bora nibaki na choo changu mie. Mkija kwangu haja ndogo mkajisadie kwenye shina la mgomba.
![]()
Unaweza ukaikuta kwenye choo sasa hii ni mara moja lbda kwa muuuda, but hii ya mtu ndio tabia yake na ndio unaishi naye 7 days a week, 12 months a year x miaka utakayoishi naye mh! si unyanyasaji wa kisaikologia huu !
wenzio tulifanikiwa..siyo kila mtu kafika saa 12 kama wewe hadi huoni
Maamuzi ya busara ni kwenda kumpima akili, wajua tunatembea na vichaa halisi. Note "Kila binadamu ni kichaa ila aliyezidi ukichaa ndie tunaemwona tofauti na sisi" Ukitaka kuamini angalia watu wakimpiga mwizi hadi kufa, kuna akili timamu hapo?
Mimi nilishasema ukipata mchumba pima ukimwi, malizia na kupima akili
Ha ha we Tamatheo sasa unataka kuanzisha mandamano ya wababa hapa nchini, yaani katiba itamke wazi kuwa wa baba wapimwe akili kabla ya ndoaTena wakati huu wa vuguvugu la katiba mpya ndio wakati muafaka ili tuliweke kisheria kabisa, ili huyu jamaa yetu awe sample baada ya katiba kupitishwa.
Yaaaani, Hakuna USIRI wa NDOA!! siku hizi , kila kitu wanawake tunahadithiana, kwani angesafisha halafu akamwambia kuwa kitendo hicho alichofanya hakipendi ingekuwaje? na akumbuke huyo amwambiaye ataenda kuyasambaza mtaa wooote , so itajulikana kuwa mumewe ni mchafu huwa akisha PUU " haflash. KIFUA Mungu alikiumba kusitiri vitu vikubwa vya ndani ya NDOA na si upambo! TUWE NA USIRI WA NDOA ZETU JAMANI!!!! Loh!nyumba kuta nne jamani lol!na bati lake juu!