Vijiji vingi vilivyopo nje ya Africa ni vizuri sana

Vijiji vingi vilivyopo nje ya Africa ni vizuri sana

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
5,895
Reaction score
11,788
Kwa hapa Africa maeneo mengi yenye muonekano mzuri ni maeneo ya mijini. Hapo kwenye miji yetu kidogo utakuta kuna mitaa ya kishua, kuna town centre iliyokaa unyama, yani miji yetu huwa na baadhi ya mitaa mizuri at least, ingawa bado inasumbuliwa na slums pia

Sasa ukija kwenye vijiji vyetu, ni ngumu sana kukuta kijiji kina muonekano wa kuvutia. Utakuta nyumba za udongo, au nyumba nzuri zipo ila moja moja, umeme wa shida, barabara za hovyo, shule chache tena zinafelisha hatari, yani unakuta kijijini vitu vizuri ni vile natural tu kama milima, mito, ziwa nk

Lakini ukiangalia vijiji vingi nje ya Africa vilivyo ni tofauti sana na vijiji vyetu. Kuna watu wanapenda maisha ya utulivu ya kijijini ila wakifikiria vijiji vyetu vilivyo nyuma kimaendeleo wanalazimika kubaki mijini tu

Angalia mfano vijiji hivi, ambavyo vipo nje ya Africa halafu fananisha na 80% ya vijiji vya hapa Africa



From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg
From fairytale streets to crystal-clear canals_ these 10 most beautiful villages in the world...jpeg

Pia kama kuna kijiji chochote kizuri hapa Tanzania naomba mnitajie nijaribu kufuatilia. Maana nimekesha Google maps kila nikiangalia vijiji vyetu pale sehemu ya photos naona hali ni mbaya
 
Hivyo sio vijiji Bali majiji ya sasa ama ya zamani, mfano wake kwa Tanzania ni kama Stone town Zanzibar, Bagamoyo, Pangani etc.

Ulaya kuna nchi nyingi Tu majiji Yao hayana maghorofa marefu.

Mfano hio Frigiliana ilijengwa na Moors Enzi za Andalusia ukiangalia architectural yake hazitofautiani Sana na stone town
images (1) (3).jpeg
 
Hivyo sio vijiji Bali majiji ya sasa ama ya zamani, mfano wake kwa Tanzania ni kama Stone town Zanzibar, Bagamoyo, Pangani etc.

Ulaya kuna nchi nyingi Tu majiji Yao hayana maghorofa marefu.

Mfano hio Frigiliana ilijengwa na Moors Enzi za Andalusia ukiangalia architectural yake hazitofautiani Sana na stone town
View attachment 3553139
Zanzibar hapo Stone Town kuna watu hadi laki 7
Frigiliana ina watu 3300 tu. Yani ni wachache kuliko wanafunzi wa karibia kila chuo Tanzania
Sehemu yenye watu 3300 sio jiji.

Hata tukitoa Frigiliana bado naweza kukuonesha mamia ya picha za vijiji vingine vizuri sana nje ya Africa
 
Zanzibar hapo Stone Town kuna watu hadi laki 7
Frigiliana ina watu 3300 tu. Yani ni wachache kuliko wanafunzi wa karibia kila chuo Tanzania
Sehemu yenye watu 3300 sio jiji.

Hata tukitoa Frigiliana bado naweza kukuonesha mamia ya picha za vijiji vingine vizuri sana nje ya Africa
Stone town haina watu laki 7, stone town ni kisehemu kidogo Tu kinaanzia Baharini mpaka darajani/Mlandege, stone town ni sehemu ndani ya Zanzibar, same to Frigiliana ipo ndani ya Jiji la Málaga.
 
Stone town haina watu laki 7, stone town ni kisehemu kidogo Tu kinaanzia Baharini mpaka darajani/Mlandege, stone town ni sehemu ndani ya Zanzibar, same to Frigiliana ipo ndani ya Jiji la Málaga.
Now you have it
Stone Town ni part ya jiji so ni the same, ni eneo la mjini lililojengeka vizuri
Lakini Frigiliana sio part ya jiji la Málaga
Screenshot_20260305-204851.png
 
📍Marangu, Kilimanjaro
📍Lushoto, Tanga
📍Mahenge, Morogoro
Lushoto si ndo pako hivi?
lushoto-town.jpg

Kwa level ya vijiji vya Tanzania imejitahidi ila bado sana, mabati yenye kutu yanaharibu mwonekano. Pia barabara sio nyeusi

Ila kwa vijiji vyote Tz labda Ndanda (Mtwara) ndio naona pako vizuri, kuna lile eneo la wamisionari. Wazungu wamelijenga vizuri sana. Hili hapa
Abasia-yote.jpg
 
Lushoto si ndo pako hivi?
View attachment 3553145
Kwa level ya vijiji Tanzania imejitahidi

Ila kwa vijiji vyote Tz labda Ndanda (Mtwara) ndio naona pako vizuri, kuna lile eneo la wamisionari. Wazungu wamelijenga vizuri sana. Hili hapa
View attachment 3553147
You don't get the point, lushoto sio ancient city, ni mji wa karibuni Tu, Bagamoyo na Pangani zote zina fit hizo criteria kama unataka km kadhaa toka kwenye jiji,

na kama nilivyokuambia huko juu ni mji wa zamani huo na upo Málaga, usiiamini Chatgpt ama Gemini Asilimia Mia itakuingiza chaka, mfano wake ni kama Dar es salaam sasa hivi watu waondoke baada ya miaka 100 kuwe kunaishi watu Tu kawaida kwenye nyumba za mjini then tujisifie vijiji vyetu ni vizuri.

Pia north Africa na West Africa ndio wamejenga hio miji mingi kwao pia kuko hivyo hivyo
 
You don't get the point, lushoto sio ancient city, ni mji wa karibuni Tu, Bagamoyo na Pangani zote zina fit hizo criteria kama unataka km kadhaa toka kwenye jiji,

na kama nilivyokuambia huko juu ni mji wa zamani huo na upo Málaga, usiiamini Chatgpt ama Gemini Asilimia Mia itakuingiza chaka, mfano wake ni kama Dar es salaam sasa hivi watu waondoke baada ya miaka 100 kuwe kunaishi watu Tu kawaida kwenye nyumba za mjini then tujisifie vijiji vyetu ni vizuri.

Pia north Africa na West Africa ndio wamejenga hio miji mingi kwao pia kuko hivyo hivyo
Basi AI ya Google inadanganya. Twende Wikipedia. Still Frigiliana haipo ndani ya jiji la Málaga. Ipo 70km from Malaga, kumbuka sio kila sehemu ndani ya Málaga province ni city. Ni sawa na uende Tukuyu useme ni part ya Mbeya city kitu ambacho sio kweli
AI is right, Frigiliana is not part of any city
Screenshot_20260305-211753.png

.
.
Okay, Frigiliana ni old town. Lakini bado vijiji vya Ulaya ni vizuri tu tena bila hata much effort vinapendeza
Vipo vingi ambavyo havikuanza kama old towns na ni vizuri
Sisi hata hiyo Bagamoyo sidhani kama inafanana na Frigiliana. Bagamoyo ni town kabisa yenye watu 80,000 tofauti na Frigiliana yenye watu 3300 hadi 3500

Kuna hivi vijiji ambavyo sidhani kama vilikuwa old towns navyo
wengen-village.jpg
Wengen-small.jpg
 
Kwa hapa Africa maeneo mengi yenye muonekano mzuri ni maeneo ya mijini. Hapo kwenye miji yetu kidogo utakuta kuna mitaa ya kishua, kuna town centre iliyokaa unyama, yani miji yetu huwa na baadhi ya mitaa mizuri at least, ingawa bado inasumbuliwa na slums pia

Sasa ukija kwenye vijiji vyetu, ni ngumu sana kukuta kijiji kina muonekano wa kuvutia. Utakuta nyumba za udongo, au nyumba nzuri zipo ila moja moja, umeme wa shida, barabara za hovyo, shule chache tena zinafelisha hatari, yani unakuta kijijini vitu vizuri ni vile natural tu kama milima, mito, ziwa nk

Lakini ukiangalia vijiji vingi nje ya Africa vilivyo ni tofauti sana na vijiji vyetu. Kuna watu wanapenda maisha ya utulivu ya kijijini ila wakifikiria vijiji vyetu vilivyo nyuma kimaendeleo wanalazimika kubaki mijini tu

Angalia mfano vijiji hivi, ambavyo vipo nje ya Africa halafu fananisha na 80% ya vijiji vya hapa Africa



View attachment 3553123View attachment 3553124View attachment 3553125View attachment 3553126View attachment 3553127View attachment 3553128View attachment 3553129View attachment 3553130View attachment 3553131View attachment 3553132
Pia kama kuna kijiji chochote kizuri hapa Tanzania naomba mnitajie nijaribu kufuatilia. Maana nimekesha Google maps kila nikiangalia vijiji vyetu pale sehemu ya photos naona hali ni mbaya
Kupaulia bati la chuma nadhani marufuku kwa wenzetu majuu huko!

Emb wajuzi wa mambo, tuelezeni hili limekaaje?

Maana yasijekuwa kuna madhara katika mambo yetu yalee, tukawa hatujui huku tukilemaa tusijue kisababishi.

Iweje wao hatu tu kule kukosea hata kupaulia banda la kuku, hakuna, kila nchi ni vigae kwa kwenda mbele!
 
Kiukweli mimi kati ya vitu huwa natumia kupima uwezo wa akili na ustaarabu wa jamii fulani kwanza huwa naangalia namna wanavyojali na kutunza mazingira yao kwanza.
 
Kiukweli mimi kati ya vitu huwa natumia kupima uwezo wa akili na ustaarabu wa jamii fulani kwanza huwa naangalia namna wanavyojali na kutunza mazingira yao kwanza.
Hakika mkuu. Halafu hata ukitoa tu utunzaji wa mazingira jamii za Kiafrika naona uzalendo bado sana.
Unaweza kunotice jinsi serikali zetu zinavyojivutavuta kuendeleza vijiji. Umeme na maji tu vinachukua muda mrefu sana hadi leo vijiji vingi hali ni mbaya
Watu wengi hata kupangiwa kazi vijijini wanaogopa maana wanajua huko wanaenda kuwa disconnected from the world kwa jinsi maendeleo yalivyo nyuma
 
Kupaulia bati la chuma nadhani marufuku kwa wenzetu mjauu huko!

Emb wajuzi wa mambo, tuelezeni hili limekaaje?

Maana yasijekuwa kuna madhara katika mambo yetu yalee, tukawa hatujui huku tukilemaa tusijue kisababishi.

Iweje wao hatu tu kule kukosea hata kupaulia banda ka kuku, hakuna, kila nchi ni vigae kwa kwenda mbele!
Huoneshwi Tu kwenye TV Ila kuna nchi kibao Ulaya Choka mbaya kuna slums ukioneshwa za Marekani ama Ulaya hazina tofauti na Vingunguti ama msimgazi bondeni/Jangwani.

EteMlWdXEAkWhYk.jpg


Umeona hapo ukimuuliza MTU yoyote mtaani atakwambia ni Africa ama India etc ila ni Ulaya napo hapo.
 
Hakika mkuu. Halafu hata ukitoa tu utunzaji wa mazingira jamii za Kiafrika naona uzalendo bado sana.
Unaweza kunotice jinsi serikali zetu zinavyojivutavuta kuendeleza vijiji. Umeme na maji tu vinachukua muda mrefu sana hadi leo vijiji vingi hali ni mbaya
Watu wengi hata kupangiwa kazi vijijini wanaogopa maana wanajua huko wanaenda kuwa disconnected from the world kwa jinsi maendeleo yalivyo nyuma
Mkuu bado tuna safari ndefu sana. Kwanzia serikali zetu hadi wananchi ni mtihani. Africa tuna maeneo mazuri sana lakini tunashindwa kuyatunza na kuwa wabunifu. Unaweza kukosa uchumi lakini ukiwa una ustaarabu wa kutunza ulichonacho kukijali na kupangilia mbona tungekuwa na mazingira ya kuvutia lakini sasa ni kinyume kabisa ni ovyo ovyo.
 
Back
Top Bottom