Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Habari hii ni ya kweli kabisa. Sio chai wala udaku.
Taharuki imetanda katika mji mmoja baada ya tukio la kutisha lililowahusisha vijana zaidi ya 40 walioshambuliwa na wanyama wakali wa porini.
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo karibu na eneo la tukio, kundi la vijana zaidi ya 40 lilijikuta katika hali ya hatari baada ya kumcheka na kumdhihaki Mtumishi wa Mungu aliyekuwa akipita njiani. Walimzodoa kwa maneno ya dhihaka kuhusu kichwa chake chenye upara. Vijana hao walimzomea kwa sauti na kejeli na kumwambia: "Paa wewe, mzee Kipara!"
Muda mfupi baada ya dhihaka hizo, dubu wawili wa porini(wild bears) walitokea ghafla na kuanza kuwashambulia vijana hao bila huruma, wakasababisha vifo vya vijana 42!
Tukio hili limechochea mjadala mkubwa, wengi wakisema ni somo kali kwa kizazi kinachopenda mzaha na kukosa heshima kwa wakubwa. Na wengine wakihusisha tukio hilo na laana.
Endelea kufuatilia uzi huu kwa taarifa/ufafanuzi zaidi kuhusu tukio hili la kushangaza.
Taharuki imetanda katika mji mmoja baada ya tukio la kutisha lililowahusisha vijana zaidi ya 40 walioshambuliwa na wanyama wakali wa porini.
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo karibu na eneo la tukio, kundi la vijana zaidi ya 40 lilijikuta katika hali ya hatari baada ya kumcheka na kumdhihaki Mtumishi wa Mungu aliyekuwa akipita njiani. Walimzodoa kwa maneno ya dhihaka kuhusu kichwa chake chenye upara. Vijana hao walimzomea kwa sauti na kejeli na kumwambia: "Paa wewe, mzee Kipara!"
Muda mfupi baada ya dhihaka hizo, dubu wawili wa porini(wild bears) walitokea ghafla na kuanza kuwashambulia vijana hao bila huruma, wakasababisha vifo vya vijana 42!
Tukio hili limechochea mjadala mkubwa, wengi wakisema ni somo kali kwa kizazi kinachopenda mzaha na kukosa heshima kwa wakubwa. Na wengine wakihusisha tukio hilo na laana.
Endelea kufuatilia uzi huu kwa taarifa/ufafanuzi zaidi kuhusu tukio hili la kushangaza.