Vijana acheni pombe na Energy drinks, mwifwa

Watoe maelezo kitaalamu hizo energy drink zina chemical zipi ndani yake zinaopelekea kuharibu figo, sio kusema tu energy drinks zinaharibu figo.
Hii itasaidia sana watu wapate uelewa kwa upana zaidi.
Mkuu fegi tu yenyewe imeandikwa uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya yako na watu bado wanakula mwenge vibaya sana.

Sidhani kama wakiandika itasaidia chochote, solution wapige stop za kwenye chupa ya plastic waweke kwenye aluminium automatically na bei lazima ibadilike itapunguza sana matumizi yake.
 
Nimesoma gazeti la Mwananchi jana lenye kichwa cha Habari ukurasa wa mbele kisemacho
Pombe, 'energy drinks' zinavyomaliza vijana

Kwa mujibu wa hili gazeti wakinukuu wataalamu wa afya wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma ni kwamba:-

1. Vijana Wanne hadi Tisa hufika Hospital hiyo kila wiki Figo zikishindwa kufanya kazi.

2. Watanzania 10 kati ya 100 wana tatizo la Figo

3. Wahanga ni vijana umri kati ya 24-40

4. Gharama za kusafisha Figo kwa mwaka ni wastani wa TZS 31,200,000 Hadi 46,800,000 bila kuweka gharama nyingine kama usafiri

5. Energy drinks ni disaster kwenye moyo kwa mujibu daktari bingwa wa JKCI.

6. Matumizi ya vinywaji hivi yanaathiri pakubwa viungo vitatu ambavyo ni
-Ini,
- Figo na
- Moyo.

7. Wahanga wakubwa ni vijana wa kiume.

MY TAKE:

Vijana acheni pombe, taifa linawategemea. Linda afya yako. Afya ni mtaji.
Kwenye list Yako,toa nguluwe
 
Aisee Mimi bila Energy drinks sijisikii vizuri kabisaaa, 2014 nilikuwa nakunywa mpaka 6 per day lakini Sasa hivi asubuhi kabla sijala chochote lazima ninywe moja baridiii sana ndio nitafute chai Sasa. 🤣🤣🤣
Wewe ni mnjanja saaana ongeza idadi
 
Energy nakubaluana kabisa,nilikuwa mlevi wa Energy tena nilikuwa napenda lile la Mo kwakuwa kubwa,aisee nikaanza kidalili cha moyo kulipuka,wala sikuenda hospital nikasema hii ni energy tu,nilivyoacha nikawa safi kabisa.Nakaa mwaka hata Energy siitumi,kwa sababu haina faida yeyote
 
Serikali ipige marufuku hizi energy drinks hasa za kwenye chupa za plastic maana zinauzwa mno bei rahisi.

Kama kuna ulazima ziwepo basi ziwepacked kwenye kopo za Alluminium na moja iuzwe 6,000 ili kuthibiti unywaji holela.

Kama pombe za karatasi za viroba zilipigwa marufuku, Serikali inashindwa nini kupiga marufuku huu ulevi wa energy drink ili kuokoa nguvu kazi ya nchi na kupunguza mzigo mkubwa kwa sekta ya afya?
Sikuizi hizo pombe wanapima kwa vizibo.
Tabu iko palepale.
 
Back
Top Bottom