Duh Yajayo.....!!!!SEHEMU YA 45
Ulionekana kuwa uzembe mkubwa, ilikuwaje nyumbani kwa bilionea mkubwa kama Cassian kutokee na mfanyakazi kufanya jambo kama hilo, utekaji uliokuwa umefanyika ulikuwa ni wa kizembe sana ambao hawakuamini kama ungeweza kutokea sehemu yoyote ile.
“Inawezekana vipi?” aliuliza polisi mmoja, maelezo ya mlinzi yalionyesha tukio hilo lilikuwa la kizembe.
Kila mmoja alishangaa, walihisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea. Walianza na mlinzi, walihisi kwamba alikuwa akijua mambo mengi kuhusu tukio hilo lililokuwa limetokea.
Alijitetea kwa upande wake kwamba hakuwa akifahamu kitu chochote kile na kwa sababu Cassian na Naseku walikuwa wakimwamini sana Sikujua, hakuwa na la kuuliza lolote lile kwa kuamini kwamba kwa kila kitu alichokuwa akikifanya kilikuwa sahihi.
“Nitamwambia nini mke wangu? Huu ni mtihani mkubwa sana kwangu!” alisema Cassian huku akionekana kuumia mno.
Simu zikapigwa, polisi wa kila kituo wakapewa taarifa juu ya kilichokuwa kimetokea. Kitu cha kwanza kabisa ambacho kwao kilionekana kuwa na uhakika wa kujua mahali watoto walipokuwa kilikuwa ni kulitafuta gari lake.
Polisi walikimbizana, kutekwa kwa watoto wa Cassian, bilionea mkubwa ilikuwa ni sawa na kutekwa kwa watoto wa rais. Polisi wakaondoka katika vituo vyao na kuingia mitaani, wakasaidiana na trafki kulitafuta gari hilo.
Hawakutaka watu wengine wafahamu kilichokuwa kimetokea, ulikuwa ni msako wa kimyakimya ambao waliamini kwamba usingeweza kuwashtua watu wengi.
Ilipofika saa 10:15 jioni, gari la Naseku likaanza kuingia mahali hapo. Kwanza hali aliyokutana nayo nyumbani ilimshtua, hakukuwa na mlinzi, geti alifunguliwa na mume wake, alibaki akijiuliza maswali mengi pasipo majibu yoyote yale.
Alimfahamu Cassian, alikuwa mwanaume mwenye furaha tele lakini kwa siku hiyo alivyokuwa akimwangalia alionekana kabisa kuwa na kitu kilichokuwa kikimtatiza moyoni mwake kwani hata tabasamu ambalo alijitahidi kumuonyeshea lilionekana kutokutoka moyoni mwake.
“Mume wangu! Kuna nini?” aliuliza Naseku huku akionekana kuwa na hofu kubwa.
“Hakuna kitu!” alijibu Cassian
Mbona hatare hii sasa!!SEHEMU YA 48
Evelyne alikuwa chumbani kwake, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria Cassian ambaye bado aliendelea kuumiza moyo wake kupita kawaida.
Maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake hayakuisha na ndiyo maana kitu pekee alichokuwa akikihitaji kwa kipindi hicho ni kuwaua watoto wa mwanaume huyo.
Aliwatuma watu ambao walimwambia kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kufanikisha kile alichokuwa kikihitaji. Hilo halikuwa tatizo kwani baada ya siku kadhaa, akapewa taarifa kwamba tayari watoto walikuwa waekwishatekwa.
Moyo wake ukawa na furaha tele, akamwambia Mwajuma kwamba tayari kazi aliyokuwa akitaka kwa kipindi kirefu ilikuwa imekamilika, watoto aliokuwa akiwataka walikuwa mikononi mwake.
Mwajuma akafurahia, akaona kwamba mtihani mgumu waliokuwa nao kipindi chote ukawa umekamilika na kwa kuwa alihitaji rafiki yake awe na furaha tele siku zote, akamwambia kwamba kwamba bado alikuwa naye bega kwa bega.
“Wapo wapi tukawaue?” aliuliza Mwajuma huku akionekana kuwa na hasira kali hata zaidi ya alizokuwa nazo Evelyn.
“Subiri! Wanasema wapo njiani!” alisema Evelyne.
Alichukua simu yake na kuwapigia watu wake kwa lengo la kuwaambia kwamba hawakutakiwa kuwaua watoto hao wao bali walitakiwa kumsubiria kwani yeye ndiye aliyekuwa na jukumu la kuwamaliza kwa mkono wake.
Kila alipokuwa akipiga simu, haikuwa ikipokelewa, moyo wake ulikuwa na presha kubwa, alikuwa na kimuemue ambacho hakuwa nacho kabla. Hakuacha, muda wote alikuwa akiwapigia simu lakini majibu yalikuwa yaleyale kwamba simu haikuwa ikipatikana.
Akahisi kulikuwa na tatizo, akahisi kwamba inawezekana watu hao walikuwa wamemgeuka na ndiyo maana walizima simu zao na hawakutaka kuziwasha kwa ajili yake.
Alihuzunika, ilipofika majira ya saa sita mchana akawapigia tena, wakati huo simu ilikuwa ikiita kuonyesha kwamba iliwasha, alisubiri, haikupokelewa kwa wakakati, alikuwa na hamu kubwa, baada ya sekunde kadhaa, simu ikapokelewa na sauti ya upande wa pili kusikika.
“Samahani simu iliisha chaji,” alisema mwanaume aliyesikika upande wa pili.
“Usijali! Imekuwaje huko?” aliuliza Evelyne.