Sniper
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 2,008
- 949
Ndoa ni taasisi yenye nguvu kubwa kijamii na kiroho. Lakini pale panapojitokeza kutokuelewana, mara nyingi matokeo yake huwa ni migawanyiko na hatimaye talaka. Katika mazingira mengi, talaka haimalizii tatizo pekee, bali huibua hali mpya ya maumivu, visasi na mara nyingine mashambulizi ya kiroho.
Baadhi ya wake, baada ya kutalakana, huchukua hatua za kichawi kumfunga mume wao kimaendeleo. Vifungo hivi huonekana katika sura mbalimbali: mume kushindwa kupata mafanikio ya kifedha, kuzuiwa kupata kazi nzuri, biashara kufa ghafla, au hata kukosa amani ya kimaisha. Hii inatafsirika kama “kifungo cha talaka” ambacho hutokana na hasira, wivu au hamu ya kulipiza kisasi.
Wakati ndoa na talaka zinapaswa kuwa mchakato wa kuamua njia bora za maisha ya baadaye, uchawi unaotumika kama kifungo unageuza talaka kikwazo kwa maendeleo.
Ni bahati mbaya sana baadhi ya wanaume wengi hawajalijua hili. Nawasanua, unapoona sintofahamu baada ya talaka, jikague, chukueni hatua.
Hii sio ramri chonganishi. Yapo kwenye jamii zetu na tunaishi nayo. Na vibinti vya sikuizi vimekuwa vichawi kuliko bibi zao!
Baadhi ya wake, baada ya kutalakana, huchukua hatua za kichawi kumfunga mume wao kimaendeleo. Vifungo hivi huonekana katika sura mbalimbali: mume kushindwa kupata mafanikio ya kifedha, kuzuiwa kupata kazi nzuri, biashara kufa ghafla, au hata kukosa amani ya kimaisha. Hii inatafsirika kama “kifungo cha talaka” ambacho hutokana na hasira, wivu au hamu ya kulipiza kisasi.
Wakati ndoa na talaka zinapaswa kuwa mchakato wa kuamua njia bora za maisha ya baadaye, uchawi unaotumika kama kifungo unageuza talaka kikwazo kwa maendeleo.
Ni bahati mbaya sana baadhi ya wanaume wengi hawajalijua hili. Nawasanua, unapoona sintofahamu baada ya talaka, jikague, chukueni hatua.
Hii sio ramri chonganishi. Yapo kwenye jamii zetu na tunaishi nayo. Na vibinti vya sikuizi vimekuwa vichawi kuliko bibi zao!