Vifo vya Tembo: Tumuunge Mkono Kikwete

Vifo vya Tembo: Tumuunge Mkono Kikwete

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,367
Reaction score
100,408
Wapendwa tumuunge mkono JK katik,a kampeni yake ya kupunguza au kukomesha kabisa mauwaji ya Tembo wetu ambao wamebaki wachache sana (sina idadi kamili).

Hata hivyo kwakuwa Jk anaenda kuiwakilisha Tanzania ningeomba jambo hili moja lizingatiwe na ndilo ombi langu kuu kwamba, asiende kurusha vijembe dhidi ya Gazeti la Daily Mail bali akaweke na aishie hapo tu penye kuweka na kuuelezea Ulimwengu mikakati au chochote alichonacho dhidi ya ku-protect Tembo wetu.

Wenzetu wale walikuja na facts basi na sisi tuweke facts kama tunazo, ni ujinga na ushamba kusema Gazeti linamchafua Rais bali tuunyeshe ulimwengu basi sis kuwa sisi "tuwasafi". Zipo hadi video zenye ushahidi huo wa wauzaji wa meno ya tembo tena Dar suio Mkoani. Kwahio kwa namna yoyote ile KIikwete usiende kupinga wala kupiga vijembe eleza mikakati yetu tu (kama ipo).

Ukimaliza rudi nyumbani tuchome yale mabango yalioyoandaliwa kwa mabilioni, maana naamini Tembo wetu hawatalindwa kwa mabngo bali kwa kila mmoja wetu kuwa mwaminifu katika utendaji wake.
 
unatoa wito kwa majangili au kwetu sisi waungwana,

Ni vigumu sana kumuunga mkono kikwete wenu.
 
Huyo huyo mlisema tumuunge mkono kwenye vita ya madawa ya Kulevya baada ya kusema ana orodha ya wauza unga wakubwa na wadogo lakini hadi leo hii hajawataja wala kuchukuliwa hatua yeyote na biashara inazidi kushamili huku mateja wakialikwa Ikulu kula bata.

Kwa hiyo Tambua anachokiongea ni tofauti kabisa na atendacho.
 
Elli, is this U?
Nldhani umekuja na huo mkakati wa Jk ili tuunge mkono!

Sasa mpaka hapo tumuunge mkono kwa lipi?
 
tumemshauri amfukuze katibu mkuu akakataa,subiri wakamchane live.
 
Elli

Umeandika sawa sana, ukweli husimama wenyewe, na kama kweli wanaandika kukuchafu lazima pia ujiulize, inamaana bado kuna tatizo kubwa...hii inaonesha kunaunafiki mkubwa sana katika hii biashara ya ujangili... lakini kitu ninacho amini kwa dhati kama kweli serikali ingekuwa ina nia thabiti ya kupambana na ujangili ingekuwa imefanikia!
 
Last edited by a moderator:
Elli, is this U?
Nldhani umekuja na huo mkakati wa Jk ili tuunge mkono!

Sasa mpaka hapo tumuunge mkono kwa lipi?
 
Labda kama atajivika magwanda na kuingia porini kupambana na majangili,na baada ya hapo atueleze bila kificho wahusika wakuu wa hii biashara,hata mimi nitajiunga nae.
 
Tumuunge mkono kwa lipi kwa kumchagua katibu mkuu wa chama chake ambae ni kubwa la majangiri
 
Ngoja nami nitengeneze meli yangu maalumu ya kusafirisha sembe na meno nikitajirika nitamuunga mkono
 
Binafsi sioni jambo jipya kwa serikali yetu na wala sioni umakini wowote kwenye utokomezaji wa ujangili...

Zilipigwa kelele wakati huo faru wanauawa, serikali hii hii iliziba masikio na faru wote wakaisha...

Sasa hivi sijui tuna faru hata 15 hawafiki na hapo ni baada ya kuwawekea tracking system...

Hata hawa tembo naamini kabisa itafika wakati nao wataisha kabisa hata tufanye kampeni vipi...
 
Na mimi nasema na tumuunge Mkono katika Kuyasambaza yale Ma Bango.

Majangili lazima wata feel Guilty tu, ni binadamau na wao pia ujue...
 
Elli

Hivi wewe unaaamini Kikwete hawajui wanaoua tembo wetu? Ntiashangaa kama atakuwa haujui. Tatizo wanaoendesha hiyo biashara ni wale wale wanaomzunguka na kula naye. Kwani kuna siri gani kwamba Kinana anahusika na hii biashara (bila shaka hatatishia kunipeleka mahakamani kama alivyofanya kwa Mchungaji Msigwa) na huyo ndiye katibu mkuu wa chama tawala. Kwamba Kikwete hajui wakati ndege ya kijeshi kutoka ughaibuni ilikuja ikapata clearence ikatua KIA ikabeba Twiga walio hai na kuondoka.

Samahani lakini, sijui mleta mada unataka tumsaidie Kikwete kivipi?

Tiba
 
Kwenye huo mkutano angekwenda na KINANA naye akajieleze atasaidiaje kutokomeza majangili kupitia kampuni zake. Hata hivyo nani atamfunga kengele mwenzie kwenye serikali hii SIKIVU. Kama twiga alipanda ndege bila kuonekana itakuja kuwa majangili wanaojificha vichakani!!!
 
Hatuwezi kumuunga mkono kwa hili,

Kwa sababu Waharifu wanafahamika na Serikali inalijua hilo. Kinana ametajwa muda mrefu lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yake.

Hivyo huenda hata Rais ana mkono wake katika suala la mauaji haya ya Rasilimali za Taifa na ndio maana yupo kimya.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Back
Top Bottom