Najua kuna watu wanafatilia sana na kushtuka na idadi ya watu wanaokufa huko Italy kutokana na ugonjwa wa korona. Vifo hivi vimeleta hofu kubwa kiasi kwamba watu kusitisha shughuli zote ili kuzuia maaambukizi.
Kwa muktadha huo nimependa watu hasa wa dunia ya tatu kufahamu magonjwa ya mafua na yenye kuathiri mfumo wa upumuaji yamekuwa yakisababisha vifo vingi sana sana. Simaanishi kuhafifisha kinachotokea sasa hasa vifo vya korona natoa picha kuwa ipo hofu ya ziada iliyotokea.
Katika utafiti uliofanywa na Rosano et al (2019) huko Italy wenye kichwa kinachosema ‘Investigating the impact of influenza on excess mortality in all ages in Italy (2013/14 – 2016/17)’ inaonyesha kati ya mwaka 2013/14 hadi mwaka 2016/17 huko Italy idadi ya watu waliokufa kutokana na magonjwa yahusianayo na mafua ni zaidi ya watu 68,000.
Mchanganuo wake ni 13/14 – 7,027, 14/15 – 20,259, 15/16 – 15,801 , 16/17 – 24,981. Utafiti huu unasema watu wengi wanaokufa ni wazee na Italia vifo vitokanavyo na mafua ni vingi sana kulinganisha na nchi nyingine Ulaya. Kwa utafiti huu na ukichukua namba kubwa Zaidi ya vifo ya mwaka 16/17, ni wastani wa vifo 2081 kila mwezi kwa mwaka mzima, na au 4163 kwa mwezi ndani ya miezi sita ambapo ni karibu ya wastani wa muda wa mlipuko wa mgonjwa haya ya mafua kila mwaka.
Sasa linganisha idadi hiyo kwa Italy ambapo hadi tarehe ya leo ni watu karibia 11,591 wamepoteza Maisha tangu vifo vya mwanzo kutangazwa tarehe 22 Feb 2020.
Je, idadi hiyo itafikia au kuzidi idadi ya watu walio kufa kwa magonjwa yahusianayo na mafua mwaka 16/17 ambayo ni 24,981?
Kwa upande wa nchi ya marekani angalia katika website ya www.cdc.gov/flue ‘burden of Influenza’, inaonyesha idadi ya vifo vinavyotokea huko America kila mwaka vinavyotokana na jamii ya mafua ambapo kwa wastani kati ya watu 12,000 hadi 61,000 hufa kwa magojwa ya jamii ya mafua kila mwaka. Hii ni wastani wa vifo 10,166 kwa mwezi ndani ya miezi sita au 5083 kwa mwezi ndani yam waka mzima.
Mchanganuo wake hadi 2017 ni;
2010-11: 37,000 , 2011-12: 12,000, 2012-13: 43,000 , 2013-14: 38,000, 2014-15: 51,000, 2015-16: 23,000, 2016-17: 38,000.
Hapo idadi kubwa Zaidi ya vifo ni watu 51,000 wa mwaka 14/15. Linganisha na idadi ya sasa takribani watu 2854 wamefariki huko Marekani kwa ugonjwa wa korona.
Kwa duniani, WHO wanasema kuwa kila mwaka hadi watu 650,000 hufa kila mwaka kwa magonjwa ya kupumua yanayohusiana na mafua kila mwaka. Angalia www.who.int/news up to 650,000 die of respiratory diseases linked to seasonal flue each year.
Hadi sasa kwa dunia nzima inakadiriwa kuwa na vifo 35,035 vitokanavyo na korona tangu mwezi disemba mwaka jana. Linganisha idadi hiyo na vifo vitokanavyo na influenza vya dunia nzima, hii kulingana na mtandao wa www.worldometers.info.
Kutoka katika website ya John Hopkins medicine www.hopkinsmedicine.org inaeleza kwa urefu tofauti kati ya ugonjwa wa korona na ugonjwa wa mafua (influenza). Kwa kifupi magonjwa haya yanafanana sana kwa dalili zake kwamba yanasababisha homa, kikohozi, kutapika n ahata kuharisha. Namna yanavyosambazwa inafanana tofauti ni (INAWEZEKANA) korona ikasambaa kupitia hewa (airborne route) na mwisho hata namna za kuzuia zinafanana mfano kuosha mikono, kukaa nyumbani n.k. Muhimu kuliko yote tunaambiwa watu wanapona kwa magonjwa yote haya.
Mwisho, wakati habari za vifo vingi zikitangazwa kila siku zimeongeza hofu. Yawezekana ni kwa sababu ya mitandao ya kijamii na vile habari zinasambaa kwa haraka tofauti na zamani. Nani ajuaye?? Yawezekana watu wengi hasa wazee ambao kinga zao zimeshuka pia wakiwa na misongo mingi wanakufa kwa sababu ya taarifa mbaya wanazosikia kila wakati. Kama mwandishi Jeff Wise wa Psychology today anavyosema katika Makala yake ya Aprili 2010 kuwa ndio hofu inaweza kukuua ‘Yes, Fear Can Kill You’
Rai: Viongozi wetu, muda wa zile siku 30 zikiisha tufungue shule na shughuli zote wakati tukiendelea kuchukua tahadhari nyingine zilizopo sasa.
Tusisambaze hofu….
Kwa muktadha huo nimependa watu hasa wa dunia ya tatu kufahamu magonjwa ya mafua na yenye kuathiri mfumo wa upumuaji yamekuwa yakisababisha vifo vingi sana sana. Simaanishi kuhafifisha kinachotokea sasa hasa vifo vya korona natoa picha kuwa ipo hofu ya ziada iliyotokea.
Katika utafiti uliofanywa na Rosano et al (2019) huko Italy wenye kichwa kinachosema ‘Investigating the impact of influenza on excess mortality in all ages in Italy (2013/14 – 2016/17)’ inaonyesha kati ya mwaka 2013/14 hadi mwaka 2016/17 huko Italy idadi ya watu waliokufa kutokana na magonjwa yahusianayo na mafua ni zaidi ya watu 68,000.
Mchanganuo wake ni 13/14 – 7,027, 14/15 – 20,259, 15/16 – 15,801 , 16/17 – 24,981. Utafiti huu unasema watu wengi wanaokufa ni wazee na Italia vifo vitokanavyo na mafua ni vingi sana kulinganisha na nchi nyingine Ulaya. Kwa utafiti huu na ukichukua namba kubwa Zaidi ya vifo ya mwaka 16/17, ni wastani wa vifo 2081 kila mwezi kwa mwaka mzima, na au 4163 kwa mwezi ndani ya miezi sita ambapo ni karibu ya wastani wa muda wa mlipuko wa mgonjwa haya ya mafua kila mwaka.
Sasa linganisha idadi hiyo kwa Italy ambapo hadi tarehe ya leo ni watu karibia 11,591 wamepoteza Maisha tangu vifo vya mwanzo kutangazwa tarehe 22 Feb 2020.
Je, idadi hiyo itafikia au kuzidi idadi ya watu walio kufa kwa magonjwa yahusianayo na mafua mwaka 16/17 ambayo ni 24,981?
Kwa upande wa nchi ya marekani angalia katika website ya www.cdc.gov/flue ‘burden of Influenza’, inaonyesha idadi ya vifo vinavyotokea huko America kila mwaka vinavyotokana na jamii ya mafua ambapo kwa wastani kati ya watu 12,000 hadi 61,000 hufa kwa magojwa ya jamii ya mafua kila mwaka. Hii ni wastani wa vifo 10,166 kwa mwezi ndani ya miezi sita au 5083 kwa mwezi ndani yam waka mzima.
Mchanganuo wake hadi 2017 ni;
2010-11: 37,000 , 2011-12: 12,000, 2012-13: 43,000 , 2013-14: 38,000, 2014-15: 51,000, 2015-16: 23,000, 2016-17: 38,000.
Hapo idadi kubwa Zaidi ya vifo ni watu 51,000 wa mwaka 14/15. Linganisha na idadi ya sasa takribani watu 2854 wamefariki huko Marekani kwa ugonjwa wa korona.
Kwa duniani, WHO wanasema kuwa kila mwaka hadi watu 650,000 hufa kila mwaka kwa magonjwa ya kupumua yanayohusiana na mafua kila mwaka. Angalia www.who.int/news up to 650,000 die of respiratory diseases linked to seasonal flue each year.
Hadi sasa kwa dunia nzima inakadiriwa kuwa na vifo 35,035 vitokanavyo na korona tangu mwezi disemba mwaka jana. Linganisha idadi hiyo na vifo vitokanavyo na influenza vya dunia nzima, hii kulingana na mtandao wa www.worldometers.info.
Kutoka katika website ya John Hopkins medicine www.hopkinsmedicine.org inaeleza kwa urefu tofauti kati ya ugonjwa wa korona na ugonjwa wa mafua (influenza). Kwa kifupi magonjwa haya yanafanana sana kwa dalili zake kwamba yanasababisha homa, kikohozi, kutapika n ahata kuharisha. Namna yanavyosambazwa inafanana tofauti ni (INAWEZEKANA) korona ikasambaa kupitia hewa (airborne route) na mwisho hata namna za kuzuia zinafanana mfano kuosha mikono, kukaa nyumbani n.k. Muhimu kuliko yote tunaambiwa watu wanapona kwa magonjwa yote haya.
Mwisho, wakati habari za vifo vingi zikitangazwa kila siku zimeongeza hofu. Yawezekana ni kwa sababu ya mitandao ya kijamii na vile habari zinasambaa kwa haraka tofauti na zamani. Nani ajuaye?? Yawezekana watu wengi hasa wazee ambao kinga zao zimeshuka pia wakiwa na misongo mingi wanakufa kwa sababu ya taarifa mbaya wanazosikia kila wakati. Kama mwandishi Jeff Wise wa Psychology today anavyosema katika Makala yake ya Aprili 2010 kuwa ndio hofu inaweza kukuua ‘Yes, Fear Can Kill You’
Rai: Viongozi wetu, muda wa zile siku 30 zikiisha tufungue shule na shughuli zote wakati tukiendelea kuchukua tahadhari nyingine zilizopo sasa.
Tusisambaze hofu….