VIDEO: Mwigulu aonya, Arusha wakiikataa CCM watakufa

VIDEO: Mwigulu aonya, Arusha wakiikataa CCM watakufa

Mchumi kageuka chinjachinja, Hayo magwanda na Midevu anaonekana ni mtu hatari ambaye anaweza kuwadhuru CCM pindi wakimtema. Jamaa kachanganyikiwa na wanamlea, lakini majuto mjukuu

Kwa jinsi alivyo, ukiongeza na tabia yake; yote yanamfanya afanane kabisa na Jonas Savimbi
 
Kwa jinsi alivyo, ukiongeza na tabia yake; yote yanamfanya afanane kabisa na Jonas Savimbi
CCM, Usalama waTaifa pamoja na Ikulu wanaipeleka Tanzania pabaya kwa kumuachia Mwigulu kuunda majeshi kwa mgongo wa CCM. Hayo magwanda anayovaa, tayari anajionyesha ni jemedari wao mkuu. Now, he is getting respect, but later will turn to be Royalty ambayo wafuasi wanakuwa brain washed
 
Mbona Mwigulu ni gamba ambalo kwetu hapa Arsha hatudanganyiki? bali tyuko tayari kwa kunyofolewa kucha kwa pispisi. OOOOhhh CCM KWISHINEY
 
Huna lolote mtoa mada mipovu tu. Et namdharau au unaishi hewani bwana mkubwa?
 
Mi huyu jamaa nilisoma nae pale Mazengo huwa ana tabia ya kutafuta umaarufu bila kutumia akili. Pale shuleni wiki chache sana kabla ya necta alikuwa akitembea anapungia watu vidole vitatu akimaanisha atapata div 1 ya point tatu kwenye EGM yake. Pamoja na kumeza Mzumbe project yote maswali na majibu yake aliambulia div 3 ya mwisho...mchumi 1st class huyo. Vijana kama akina Nashon Andrew walikuwa wanamshangaa tu kisha necta ikasoma div 1 kali tu kwa akina Andrew. Yeye oohh nakata rufaa..mara nimeonewa...mara nilipaniki...hovyooo...midevu yake anataka sifa tu. Siye huyu alimshambulia Maalim Seif kwamba baada ya kuupata u VP sasa kanyoa timberland...mie Mwigulu huwa namdharau sana.

Pangu Pakavu.
sasa aliingiaje udsm akiwa div.3??
 
Napata shaka na uchambuzi wako, sababu hana muda mrefu kwenye siasa za ccm.watu walianza kumfahamu kwenye uchaguzi mdogo wa Igunga ambapo,hata hivyo alikuwa anaropoka sana na kubebwa na rushwa ya maji ya maboza, chakula cha msaada, na pia akatoka na kashfa ya kufumaniwa na mke wa mtu.katika siasa za igunga watu wengi walihoji umakini na umadhubuti wake.lakini, sababu ccm inaendeshwa kwa makundi na kukomoana , bado alionekana kijana mchapa kazi na mwanasiasa mahili upande wa kundi lake,kuwa," anajibu wapinzani."Lakini si kweli wana ccm wapatao mil 6 wanamkubali.wapo vijana wasomi , makini ,wachapa kazi na weledi kimisingi ya kusaidia umma hata kutetea itikadi ya ccm ya kutetea wanyonge.lakini hawapewi nafasi.Hivyo kachwa kutetea kundi la wana ccm mafisadi kiasi, kwamba anashindwa kuhimili mabadiliko na kuwa msanii wa kuropoka maneno yake na si sera za kutetea wanyonge.Ki msingi NCHEMBA si mwana siasa mweledi wa si mahili , na wal hakuwa mvuto muda mrefu.ila kwa wanaccm wa kundi lake wanaosaidiwa na Riz mtoto wa kaya , wakitetewa na usalama wa taifa , mwache naye apige karata yake .ndo maisha ya watanzania tumezoe ghiriba, hili, hadaa, na unyonge ulikithiri bila kuwa na mtetezi.sasa kama anasema maneno hayo ya kutowasaidia wananchi wa Arusha , je wana arusha si walipa kodi?je hakuna rasilimali mkoa wa arusha taifa linafaidika nazo ambazo wanaArusha wanasitahiki kupelekewa maendeleo bila kujali itikadi za kichama? wana Arusha je ,si watanzania wanaositahiki maisha bora bila siasa za vyema?kama kweli kasema hivyo hata ndani ya ccm hafai.

Haya yote uliyoyasema ni ya kweli ila kuna jambo moja tu ambalo haujaliweka wazi....katika zama hizi za uwepo wa CCM kwanza kabisa bila nguvu ya dola haiwezekani CCM kuwepo....na kila aliye kwenye nafasi ya kuchaguliwa ndani ya CCM ni MSAIDIWA wa dola .... kuanguka au kutobebwa kwake kunamaana ya wafanyakazi wa dola kupata adhabu mbali mbali....Wanaohodhi nyadhifa mbalimbali ndani ya CCM huchukuliwa ndio waendesha nchi na hakuna mkato pindi watakapo litaka jambo lazima dola ihusike kuhakikisha linafanyika....kwa bahati mbaya kuna kundi la wadhalimu lililotambua nguvu ya kuwa mwanaCCM likaingia kwanguvu sana kupata nyadhifa nakuitawala CCM bila hata kuijua...Kauli mbalimbali za hao wanaohodhi hizo nyadhifa kwa sasa hazina tofauti na za Mwigulu....kauli ya kawaida sana tena kila wakati ya Mh. Magufuli kuwa "serikali ya CCM inapitisha barabara hata walipo wabunge wa upinzani" ... nakushangiliwa sana na wabunge wote waliopo Bungeni wa CCM....inaashiria mambo mawili kwamba waziri na wabunge wa CCM hawana habari kuwa Waasisi wa CCM walitofautisha serikali na Chama kwamba, Chama hakina hadhi ya kuwa Serikali ila kitaomba ridhaa ya kuendesha serikali....("ukiwa dereva wa Buldoza haina maana wewe ni Buldoza"...! )... serikali haiachi kuwa serikali kwakuwa CCM wako madarakani, ukiona hilo linaaminika basi tambua ni ishara ya serikali dhalimu....kwamba pengine wananchi wa Tanzania ya leo hata misingi ya CCM hawaikumbuki tena na ndio maana udhalimu umekuwa sifa ya kiongozi wa kitanzani...."mwaache naye akale" ndivyo wananchi wajuavyo juu ya uongozi, pili ... ni dhahiri viongozi hawa wa CCM wanajua watanzania hawakumbuki tena sifa za uongozi ...kwa upungufu huu wa Watanzania CCM ya wadhalimu wameendelea kuuacha ufikiri huu kukua ndani ya vichwa vya watanzania na kuutumia kujikita madarakani....utasikia kiongozi anajinadi eti amejenga hospitali au shule kwa fedha zake mfukoni na wananchi wanashangilia kuwa ndiye anaestahili kuwaongoza kisa anauwezo wa hayo maendeleo....wamesahau imani ya CCM kuwa maendeleo ni WATU, ARDHI, SIASA SAFI na UONGOZI BORA na vigezo vya hayo maendeleo ni uwezo wa WATU wenyewe (Siyo mtu-kiongozi) kupambana na UMASKINI, MARADHI, NJAA na UJINGA kwamba kazi ndiyo msingi wa maendeleo na si mtu....kwahiyo wajibu wa kiongozi ni kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na kazi ili waondokane na hayo manne...iwe kilimo, iwe biashara ya mazao iwe ni ajira katika ujenzi wa barabara, majengo n.k. pia wajibu wa siasa safi ni pamoja na kuhakikisha mikataba na wawekezaji wa nje WAFAIDIKA WAKUU ni WANANCHI na siyo baadi ya WADHALIMU walioihodhi dola... CCM.

UMASIKINI kwa tafsiri ya CCM pia unaainisha kuwa kukosa MALAZI, CHAKULA na MAVAZI ndio viashiria vya umasikini ... hivyo basi UONGOZI BORA utalenga katika kupata vyanzo vya mapato ili WATU waondokane na hayo mfano sera sahihi za ufanyaji biashara nchini nk. Lakini leo Mwigulu anaamini ktk Ilani ya Uchaguzi ya CCM yaani kinyume kabisa na imani ya chama....ambacho kwa sasa kinamilikiwa na wadhalimu eti kitawaondolea wananchi haya yote ilahali Viongozi wanaCCM wanashindana ni nani mwenye uwezo wa kuwa tajiri akiwa madarakani zaidi ya mwenzie ni lini huo utajiri utawafikia hao wananchi?
 
Akiwa anahutubia viwanja wa Kijenge Chini hapa Arusha Mwigulu nchemba alisema tukiikataa CCM na kuichagua CHADEMA TUtakufa!!!! Na baada ya kukaa Arusha na utafiti kumwonyesha CCM haina Chake AMETIMIZA aliyosema.
Mungu atasimama katika hili tukio.
 
Jamaa ana roho mbaya zaidi ya Hitler

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mungu atawalipizia wote waliohusika mchana kweupe mara saba sabini!
 
Bunge la magamba litasema nini juu ya hili Ngoja tuone watakavyojibebe kuja kushuhudia maiti zao
 
Kila anapopita lazima iwe mbaya. Iko day tu
 
hawa jamaa wanavichwa vigumu sana,jamani muda wa mabadiliko ukefika hakuna wakuzuia,na hivyo vifo ndo vinachochea zaidi mabadiliko.Nakumbuka THE GREAN OF WHEAT ya Ngugi W. Ilikua ni busara kuheshimu wimbi la mabadiliko na siyo kuwatisha wananchi kwa mauaji.The Hague watu lazima wapelekwe.
 
Nafikiri amejiandaa kuingia msituni ndio maana ameanza kwa kuachia ndevu ili atishe watu. Nchemba amejaribu kumpoteza Lwakatare imeshindikana na sasa wamekuja na mbinu ya kuua
 
Nyie watu wa Arusha mmekuwa waoga sana. Kama ingekuwa ni mkoa wa Mara TATA huyo Mwigulu saizi angekuwa anacheka na fashist mwenzie Idd Amini huko kuzimu. Cha kushangaza kafanya mauaji Arumeru ya Mbwambo mmemuangalia na sasa kafanya mauaji mengine na atalala hapo hapo Arusha na kesho atawadhihaki mitaani. Uanaume wenu uko wapi???
 
Mkubwa nakwambia 100% anahusika kama kauliye ilivyosema!


Akiwa anahutubia viwanja wa Kijenge Chini hapa Arusha Mwigulu nchemba alisema tukiikataa CCM na kuichagua CHADEMA TUtakufa!!!! Na baada ya kukaa Arusha na utafiti kumwonyesha CCM haina Chake AMETIMIZA aliyosema.
Mungu atasimama katika hili tukio.
 
Nahisi wamechoka amani. Damu ya mtu.haiendi bure malipo ni hapahapa
 
Back
Top Bottom