Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,104
- 2,345
Courtesy: Ansbert Ngurumo with SK Media Online TV
====================================================
Kwa muhitasari:
✍️Ansbert Ngurumo anasema, Paul Makonda anakwepa kutoa dira na nini atakifanya kwa kuzingatia majukumu yake ya kikatiba Kwa mujibu wa katiba ya Chama Cha Mapinduzi - CCM na badala yake anahangaika na u - demagogi..
✍️Kwa wasiojua, majukumu ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM kwa mujibu wa katiba ya chama chao yaani CCM ni:
1. Kushughulika na masuala muhimu ya Itikadi ya CCM..
2. Kueleza na kufafanua Itikadi, Sera na Mipango ya CCM..
3. Kupanga na kuandaa mafunzo ya makada na wanachama wa CCM.
4. Kuyatangaza mambo haya (Sera, Itikadi na Mipango) na kuyafanyia uenezi kwa umma..
5. Kuongoza maandalizi ya Sera, Mipango na Ilani ya chama chao..
6. Kusimamia utafiti, kumbukumbu na kulinda maktaba ya chama chao..
=================================================
Hivi huyo mhuni anayeonekana kwenye kipande Cha video hiyo anamsaidia Makonda na CCM kutekeleza jukumu gani la Paul Makonda katika hayo yaliyoorodheshwa hapo☝️☝️ juu?
Haa haa. Ni u - demagogi tu mbele kwa mbele!
Je, atamjenga Rais Samia na CCM yake au anampeleka kaburini pia?