Vibaka kuzunguka Ikulu, Usalama upo?

Vibaka kuzunguka Ikulu, Usalama upo?

Ni mita ngapi kutoka ikulu ya nchi!?
Polisi labda wako kwenye maandalizi ya kusimamia uchaguzi nadhani wakimaliza hilo watahamia hilo eneo kudhibiti hali ya mambo. Sina uhakika hadi wakati huo watakuwa wameathirika raia wema wangapi!


Kaka Lukindo. Waathirika wa Ocean Road wanazidi mia tano. Pale huna cha kujitetea wakikuweka kwenye 18. Ni pori tupu na ufukwe. Wanakufanya wanalolitaka
 
ndio wanapaita Lebanon huko....
hatari sana...
ukitaka kupita usiku basi pita kama kibaka tu au teja wala hawakuzingui
 
Binafsi walitaka kunikata mapanga.Nilikuwa nafanya jogging majira ya saa moja usiku.Nilipofika karibu na viwanja vya basketball wakatokea jamaa wanne na mapanga.Ni bahati tu niko fit na waliponikimbiza niliwaaacha mbali.

Ni aibu kwa eneo hili kuwa na majambazi.Hili ni eneo karibu na ikulu na polisi wa doria wanapita kila mara.

Hivi ni kwa nini polisi wasiyawekee mtego majambazi haya wakayanasa.?

Mtego wenyewe rahisi tu...askari wachukue gari aina ya noah na waende muda huo wa uharamia wakiwa wengi na silaha za moto. Dereva awe mwanamke na akifika hapo ajifanye gari limemharibikia najua watatokeza kichwakichwa. Kitakachofuatia ni kufumua fumua ubongo kwa risasi, baasi.
 
Hapo nyuma ya huo mtaa mbona kuna wakubwa zao ila wao ni wavaa suti! Ni sehemu tu ya kugawana majukumu! Nyie kaben hapa sie tukabe huku

Una maana Polisi wetu hushirikiana nao, au ulimaanisha Usalama wa Taifa?
 
Una maana Polisi wetu hushirikiana nao, au ulimaanisha Usalama wa Taifa?

yote ni majibu sahihi kwani haiingii akilini kusema kamera za ulinzi za ikulu zinaona mwisho getin tu na hao polisi kujibu ni matukio ya kawaida bila kuongeza nguvu ni kudhihirisha ushiriki wao. Hivi vyombo viwili yafaa kuacha kutegeana kwa kusema swala la vibaka ni la polisi ilihali hapo ni usoni na machoni pa nchi. Hebu wajibikeni kwa pamoja ili kuuondoa uchafu huo hapo.
 
yote ni majibu sahihi kwani haiingii akilini kusema kamera za ulinzi za ikulu zinaona mwisho getin tu na hao polisi kujibu ni matukio ya kawaida bila kuongeza nguvu ni kudhihirisha ushiriki wao. Hivi vyombo viwili yafaa kuacha kutegeana kwa kusema swala la vibaka ni la polisi ilihali hapo ni usoni na machoni pa nchi. Hebu wajibikeni kwa pamoja ili kuuondoa uchafu huo hapo.

Kwa mfano wananchi wakienda na kuua jambazi moja, itasaidia?
 
Hao wanakaa NCHI YA LEBANON najua wa Mkoani hawaijui nchi ya Lebanon iko wapi hapo ferry
 
Pole sn kwa unyanyasaji uliofanyiwa!

Limefika mezani kwa wadau wa usalama watalifanyia kazi
 
USIGUSE WAZUNGU WA MELI WANA KANCHI KAO HATA SEMBE,WIDA,GONGO KWAO NI HALALI.....
Tena hata wewe unabahati sana yaani uliwakimbiza?
 
Hello wana JF,

Nimeshuhudia matukio ya vibaka kuvamia wapita njia (Ocean Road) kwenye mpaka wa IKULU mara mbili.

Tukio la kwanza lilitokea majira ya jioni baada ya wanawake wawili kuegesha gari yao pembeni kwa dharura, walivamiwa na vibaka wakanyang'anywa simu na mikoba yao na niliposimama kutoa msaada, vibaka hao walikimbia wakiwa na mali walizopora.

Pili imetokea juma lililopita saa sita mchana baada ya kijana mmoja mtembea kwa miguu kusimamishwa na vibaka, kumpiga makonde mazito baada ya kupinga amri yao huku wengine wakimpekua mifukoni wakachukua simu pesa na viatu kisha kutimkia ufukweni.

Tukio hilo lilitolewa taarifa kituo cha polisi Kivukoni na polisi walikiri ni matukio ya kawaida pale hivyo watafuatilia!

Wadau, Nini kifanyike?

kama ndani ya ikulu kuna vibaka ,unashangaa nini kuwaona wengine wapo nje
 
Hello wana JF,

Nimeshuhudia matukio ya vibaka kuvamia wapita njia (Ocean Road) kwenye mpaka wa IKULU mara mbili.

Tukio la kwanza lilitokea majira ya jioni baada ya wanawake wawili kuegesha gari yao pembeni kwa dharura, walivamiwa na vibaka wakanyang'anywa simu na mikoba yao na niliposimama kutoa msaada, vibaka hao walikimbia wakiwa na mali walizopora.

Pili imetokea juma lililopita saa sita mchana baada ya kijana mmoja mtembea kwa miguu kusimamishwa na vibaka, kumpiga makonde mazito baada ya kupinga amri yao huku wengine wakimpekua mifukoni wakachukua simu pesa na viatu kisha kutimkia ufukweni.

Tukio hilo lilitolewa taarifa kituo cha polisi Kivukoni na polisi walikiri ni matukio ya kawaida pale hivyo watafuatilia!

Wadau, Nini kifanyike?

Mkuu Unasemea Jioni ya saa ngapi? Tua nzie hapo
 
Back
Top Bottom