Vibaka kuzunguka Ikulu, Usalama upo?

Vibaka kuzunguka Ikulu, Usalama upo?

lebabu11

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2010
Posts
3,971
Reaction score
3,948
Hello wana JF,

Nimeshuhudia matukio ya vibaka kuvamia wapita njia (Ocean Road) kwenye mpaka wa IKULU mara mbili.

Tukio la kwanza lilitokea majira ya jioni baada ya wanawake wawili kuegesha gari yao pembeni kwa dharura, walivamiwa na vibaka wakanyang'anywa simu na mikoba yao na niliposimama kutoa msaada, vibaka hao walikimbia wakiwa na mali walizopora.

Pili imetokea juma lililopita saa sita mchana baada ya kijana mmoja mtembea kwa miguu kusimamishwa na vibaka, kumpiga makonde mazito baada ya kupinga amri yao huku wengine wakimpekua mifukoni wakachukua simu pesa na viatu kisha kutimkia ufukweni.

Tukio hilo lilitolewa taarifa kituo cha polisi Kivukoni na polisi walikiri ni matukio ya kawaida pale hivyo watafuatilia!

Wadau, Nini kifanyike?

attachment.php


Vijana 6 wamekamatwa usiku huu baada ya kuhusika na wizi kwa kumtishia muuza sigara na karanga maeneo ya Ocean Road kuelekea BOT.

Vijana hawa walimtishia huyu muuzaji sigara akiwa na pakiti kumi za sigara na karanga zisizozidi za sh5000! Baada ya kuoneshwa panga na kisu aliwakabidhi mzigo na kutishiwa kuuawa kama atapiga kelele!

Kijana akajificha sehemu alipoona pikpiki akaomba msaada wakaenda kuwasubiria maeneo ya KFC!

Hapo ndipo kijana akishirikiana na walinzi wengine waliokuwa wakiwasubiri kwa hamu wakapiga ukunga wa wezi! Wazee wa CRDB wakamaliza kazi yao huku waungwana wanawarushia mawe vichwani.

Nimeacha wanasubiri defender kuwachukua! Samahani dini yangu hairuhusu kupiga picha za wenye damu, ningewawekea!

Muwe makini area hiyo usiku kuanzia saa moja!

attachment.php


Ndugu nakushauri kuanzia saa moja jioni usipite njia ile ya ocean road au sasa hivi inaitwa Barrack Obama drive nyuma ya Hotel ya Kimataifa ya Serena, uwe na gari au hata kwa miguu.

Kuna majambazi balaa watakuua kabisa uteketee duniani. Ukipita na gari hakikisha halitakuharibikia maeneo yale wala kupata pancha. Na ikipata pancha we tembea hivyo hivyo la sivyo mwisho wa dunia utakuwa umepiga hodi kwako. Ukisimama tu hutajua wametokea wapi na si zaidi ya mmoja.

Yamemtokea ndugu yangu aliyekuwa anatokea Hospitali ya Kansa Ocean Road saa mbili kasoro akasimamisha gari jirani na hospitali ya Aghakhan ili apate haja ndogo... Daaaaahh walitokea majambazi na mapanga na kilichotokea ni bas tu.

Nasikitika sana. Matukio ni mengi mno ya ocean road. Na urefu wa lile pori la viwanja vya Golf na Cricket ni mrefu sana kuanzia hospitali ya Aghakhan had kwenye uwanja wa basketball..Usipite usiku njia ile iwe kwa gari au kwa miguu.

NARUDIA TENA.. KWA UHAI WAKO KUENDELEA KUDUMU USIPITE OCEAN ROAD (BARRACK OBAMA DRIVE) IKIFIKA SAA MOJA USIKU UWE NA GARI AU HATA KWA MIGUU.

KULE NI JEHANAMU WATAKUUA...

Polisi tusaidieni!
Waheshimiwa,

Jana usiku wa saa mbili na nusu katika eneo la daraja la Selander, nilishuhudia mwanaume mwenye asili ya kizungu akiwa kang'ang'aniwa na vijana wa kibongo kama sita hivi kwa nia ya 'kumsachi' na kumpora

Matukio kama haya yalivuma sana miezi kadhaa ya nyuma kisha kukawa shwari, na wengi wetu labda tulidhani sasa hakuna hatari tena (mimi nikiwemo)

kwa nililoshuhudia jana ni wazi kwamba bado tunapaswa kuwa makini sana tupitapo maeneo yale.

Cha kushangaza hili lilitokea almost right infront of the police station, mwanzo kabisa wa daraja ukiwa unatokea mjini.

Usalama hakuna kwa eneo la kituo cha polisi , je huko vichochoroni kwetu??

Anyways it was just a word to alert you all, msijiachie mkipita pale kwenye gari na simu zenu na 'pochi' zitadakwa kama mwanzo.

TEKEA PEOPLE

Kwa tahadhari zaidi soma;

Jihadhari unapokuwa maeneo haya Dar es Salaam


Daktari Mgiriki auwawa Tanzania..

 

Attachments

  • aga khan.png
    aga khan.png
    66.8 KB · Views: 3,159
  • aga khan1.png
    aga khan1.png
    289.8 KB · Views: 3,221
Waheshimiwa,

Jana usiku wa saa mbili na nusu katika eneo la daraja la Selander, nilishuhudia mwanaume mwenye asili ya kizungu akiwa kang'ang'aniwa na vijana wa kibongo kama sita hivi kwa nia ya 'kumsachi' na kumpora

Matukio kama haya yalivuma sana miezi kadhaa ya nyuma kisha kukawa shwari, na wengi wetu labda tulidhani sasa hakuna hatari tena (mimi nikiwemo)

kwa nililoshuhudia jana ni wazi kwamba bado tunapaswa kuwa makini sana tupitapo maeneo yale.

Cha kushangaza hili lilitokea almost right infront of the police station, mwanzo kabisa wa daraja ukiwa unatokea mjini.

Usalama hakuna kwa eneo la kituo cha polisi , je huko vichochoroni kwetu??

Anyways it was just a word to alert you all, msijiachie mkipita pale kwenye gari na simu zenu na 'pochi' zitadakwa kama mwanzo.

TEKEA PEOPLE
 
POA MPWA!
tatizo wazungu wanajiachia sana wakati vijana wetu wana njaa
 
dah mzungu aliweza kuvumilia roba ya mbao kweli? naamini akirudi kwao ataenda kuandika kitabu kinachohusu kabari za kiafrika,

Sina shaka kwamba hao vibaka wakishamaliza kukusanya hesabu za siku lazima wapitie hapo polisi salenda kulipia bili yao maana inaonesha hao polisi wanawalinda vibaka wasiibiwe wala hawawalindi raia wema.
 
Tatizo sio wazungu.
Tatizo ni polisi walioshindwa kudhibiti uhalifu.
Je kutoka kituoni hadi darajani panahitaji petroli ya kuweka kwenye gari?
 
POA MPWA!
tatizo wazungu wanajiachia sana wakati vijana wetu wana njaa

yeah wajifanyaga kupita pale waki jogi mzee wanakutana na vijana kazini

ila Selander panataka kuwa kama jangwani, ukiharibikiwa na gari jnagwani uikimbie mwenyewe uwaachie......
 
dah mzungu aliweza kuvumilia roba ya mbao kweli? naamini akirudi kwao ataenda kuandika kitabu kinachohusu kabari za kiafrika,

Sina shaka kwamba hao vibaka wakishamaliza kukusanya hesabu za siku lazima wapitie hapo polisi salenda kulipia bili yao maana inaonesha hao polisi wanawalinda vibaka wasiibiwe wala hawawalindi raia wema.

jamaaa was tall enough kwa hiyo vibaka walimdandia kama wanarukia mapera vile
polisi wa pale wanajua 'wat goes on'.....sasa sijui kwa nini hawachukui hatua madhubuti!!!

hiyo kweli inaweza kutufanya tuhisi kuwa kuna baraka zao kwenye huu uhalifu pale
 
hii inatisha kwa kweli.. kuna kipindi cha nyuma ndugu yangu alikuwa napita ilikuwa saa 1830 jioni askari wakamsimamisha wakamwambia arudi pambeach akkapande basi maana pale sio salama pana vibaka wengi sasa akawauliza ikiwa mnajua kuna vibaka kwanini msiwashuhulikie kama askari wenyewe mnawaopgopa vibaka sie raia tufanyaje yule askari akamwambia mie ndio nakuambia sasa kama unalete ubishi yakikupa yakukupata usije kutulilia. nIlijiuliza maswali mengi sikupata jibu

wiki iliopita kuna doria ya maaskari walikuwa wanazunguka mitaa ile kuanzia mwazo wa daraja hadi pale ubalozi wa urusi kumbe hii yote ni nguvu ya soda.

Kuna swali huwa najiuiza hivi ule ulinzi ulikuwapo kipindi kile cha awamu ya 2 uko wapi pale darajani?? ama tumrudishe mzee ruksa madarakani atusaidie kuimarisha ulinzi??
 
wewe hujiulizi hawa majambazi wanapata wapi silaha za kushambulia mawindo yao? jibu unalo.

Polisi wana maslahi madogo hivyo ni rahisi kushawishika kufanya faulo mbaya ktk kazi zake ilhali apate chochote cha kukeep familia yake inayoishi ktk jokofu (jumba la mabati kota)
 
Ipo wazi kuwa Polisi pale Selender Bridge wanapata gawio la nguvu toka kwa wale vibaka.
 
Tatizo sio wazungu.
Tatizo ni polisi walioshindwa kudhibiti uhalifu.
Je kutoka kituoni hadi darajani panahitaji petroli ya kuweka kwenye gari?


Obvious tatizo liko kwa polisi, maana hata wakisimama tu pale nje they could see the whole scenario!!
 
hii inatisha kwa kweli.. kuna kipindi cha nyuma ndugu yangu alikuwa napita ilikuwa saa 1830 jioni askari wakamsimamisha wakamwambia arudi pambeach akkapande basi maana pale sio salama pana vibaka wengi sasa akawauliza ikiwa mnajua kuna vibaka kwanini msiwashuhulikie kama askari wenyewe mnawaopgopa vibaka sie raia tufanyaje yule askari akamwambia mie ndio nakuambia sasa kama unalete ubishi yakikupa yakukupata usije kutulilia. nIlijiuliza maswali mengi sikupata jibu

wiki iliopita kuna doria ya maaskari walikuwa wanazunguka mitaa ile kuanzia mwazo wa daraja hadi pale ubalozi wa urusi kumbe hii yote ni nguvu ya soda.

Kuna swali huwa najiuiza hivi ule ulinzi ulikuwapo kipindi kile cha awamu ya 2 uko wapi pale darajani?? ama tumrudishe mzee ruksa madarakani atusaidie kuimarisha ulinzi??

kumbe wameridhia hii hali eeh
vibaka wamejipatia baraka kwa polisi....

hapo ndipo huwasukuma raia kujichukulia hatua mkononi
 
POLISI jamii ndivyo ilivyo
maana hata vibaka ni sehemu jamii na polisi wanadumisha udugu na jamii yote bila madhara.

Unategemea nini kwa askari ambaye alijiunga na jeshi baada ya kuona hana pass marks nzuri za kuendelea mbele kimasomo?
Tatizo ni namna recruitment za kujiunga na polisi zinavyoendeshwa na siyo namna wanavyofanya kazi. Wanaajiri ndugu zao et all na utakuta hawana lolote zaidi ya utendaji wa KIMAPOKEO na si wa kwenda na mabadiliko ya tabia-watu.

Tuwape motisha askari wetu kwa kuwaandalia semina mbalimbali za kukuza uelewa wao ktk masuala ya kiteknolojia na kujitambua..... Najua CCM watapinga hili kwa manufaa yao
 
jamaaa was tall enough kwa hiyo vibaka walimdandia kama wanarukia mapera vile
polisi wa pale wanajua 'wat goes on'.....sasa sijui kwa nini hawachukui hatua madhubuti!!!

hiyo kweli inaweza kutufanya tuhisi kuwa kuna baraka zao kwenye huu uhalifu pale
eeeeeh,ndio inavyokuwa,kumtia roba TALL iko kazi.
 
Tatizo sio wazungu.
Tatizo ni polisi walioshindwa kudhibiti uhalifu.
Je kutoka kituoni hadi darajani panahitaji petroli ya kuweka kwenye gari?[/QUOTE]

Mkuu, umenifurahisha sana!!
 
wewe hujiulizi hawa majambazi wanapata wapi silaha za kushambulia mawindo yao? jibu unalo.

Polisi wana maslahi madogo hivyo ni rahisi kushawishika kufanya faulo mbaya ktk kazi zake ilhali apate chochote cha kukeep familia yake inayoishi ktk jokofu (jumba la mabati kota)

Silaha zina sehemu nyingi sana ya kupatikana. Somalia hapako salama na border zetu na Kenya haziko 100% secured. Sasa hizo silaha, tena latest ambazo hata majeshi yetu hayana unadhani zitaacha kupita na kuwafikia walengwa(majambazi). We just need to secure our borders na kuimarisha majeshi yetu. Kuimarisha namaanisha kuwapa kipaumbele kwenye maslahi pamoja na kuwa na jeshi lenye heshima na utii. Jeshi lenye kujali maisha ya raia na mali zao. Na sio jeshi lenye njaa.

Samahani kama nitakuwa nimemkwaza mtu. Ni maoni tu!
 
Inaelekea kweli si salama kwani wakati wa jioni ukipita utakuta polisi wanalinda na wakati mwingine kuna kampuni ya ulinzi kwa hiyo naamini polisi wanafahamuhilo
 
Siku za kituo polisi cha Selander zinahesabika pamoja na zile ghorofa mbili za NHC haswa katika mpango wa kupunguza foleni Jijini lazima kipitiwe!!! Hii ni baada ya Barabara mpya na daraja jipya kuongezwa kutokea Kenyatta Road (Oysterbay) mpaka Ocean Road (Seaview)...
 
Siku za kituo polisi cha Selander zinahesabika pamoja na zile ghorofa mbili za NHC haswa katika mpango wa kupunguza foleni Jijini lazima kipitiwe!!! Hii ni baada ya Barabara mpya na daraja jipya kuongezwa kutokea Kenyatta Road (Oysterbay) mpaka Ocean Road (Seaview)...

mpwazz kwa hiyo hili litasaidaje kupunguza na vibaka kama hali hii na kuna kituo cha apolisi pale pale

au kwa vile zile swamps zitatolewa pale maficho yatakosekana?
 
Back
Top Bottom