Vibaka kuzunguka Ikulu, Usalama upo?

Vibaka kuzunguka Ikulu, Usalama upo?

mada kama hizi aliziletaga sana pididy last year, pididy alikuwa anadai watu wanaliwa hadi......
 
hivi humu si wapo wafanyakazi wa wizara ya mambo ya ndani tunawaomba wafikishe kwa kova hii taarifa
 
Kumekuwa na ujambazi was kutumia visu namapanga!!majuzi shemejio alinipigia nikamchukue ifm!!nilipopita oceanaroad nikakuta MTU anaporwa pikipiki walipoona nasimama wakakimbilia upande was bfoward!!nkawatonya jamaa walinzi nikarudinao nikakuta jamaa wamemkata mkono awezikuendesha tukapiga ukunga wakajaa watu tukasubiri defender wakambeba!! Maisha borakwa kilamtz!bado was Amboni awajafika loh wakivuka KWAHERI PWANI KARIBU DSM LOH SHIDAA



Vijana 6 wamekamatwa usiku huu baada ya kuhusika na wizi kwa kumtishia muuza sigara na karanga maeneo ya Ocean Road kuelekea BOT.

Vijana hawa walimtishia huyu muuzaji sigara akiwa na pakiti kumi za sigara na karanga zisizozidi za sh5000!

Baada ya kuoneshwa panga na kisu aliwakabidhi mzigo na kutishiwa kuuawa kama atapiga kelele!

Kijana akajificha sehemu alipoona pikpiki akaomba msaada wakaenda kuwasubiria maeneo ya KFC!

Hapo ndipo kijana akishirikiana na walinzi wengine waliokuwa wakiwasubiri kwa hamu wakapiga ukunga wa wezi!!

Wazee wa CRDB wakamaliza kazi yao huku waungwana wanawarushia mawe vichwani.

Nimeacha wanasubiri defender kuwachukua !!

Samahani dini yangu hairuhusu kupiga picha za wenye damu, ningewawekea!

Muwe makini area hiyo usiku kuanzia saa moja!



Sea View, Ocean Road na Viwanja vya Golf Gymkhanna Club:
Maeneo haya kuna vibaka hatari sana ambao hushambulia kwa kikundi na kupora mali zote na kukuacha ukiwa majeruhi. Maeneo haya yametulia sana na yanaonekana ni salama sana kwani yako jirani na ikulu, lakini hayana usalama wowote na ni hatari kabisa.
Usipite maeneo hayo kwa miguu mida ya kuanzia saa kumi na mbili na nusu giza likiwa linaingi, maana utakumbwa na dhahama.




Polisi wanayajua maeneo yote hatari kwa raia, lakini haiboreshi ulinzi maeneo hayo na wala haiwatahadharishi wananchi.
 
2ywviuv.jpg
[/IMG]
vnk0n6.jpg
[/IMG]
t9bn1u.jpg
[/IMG]
 
Hilo eneo limelalamikiwa sana .....Polisi hawachukui hatua ....
 
Ni rahisi sana kuwakamata wezi sehemu kama izo kama itafanyika ambush ya kweli sema kila kitu kimekua siasa ndio shida..
 
hii nchi nayo ina raha,kuna vitu ukiwa nnje lazima uvimiss, yani oneway ya ikulu na katikati ya jiji vibaka had mchana,zamani ocean road majira ya saa 11 jion,tayar kunavibaka wanapora sana na giza linavyozidi ndo hatari baharini kote wezi tuu wamejaa, ss sie tumeona na tunapajua huyo asiyejua? watu wanaumia sana,nimeish maeneo hayo kweli ni changamoto huwez tembea maeneo ya posta kuanzia saa 2 usiku,hasa maeneo yasiyo na msongamano wa watu.
 
ni huyo huyo keekweeteteten ndiyo anayafuga hayo majambazi
 
Haya pia yapo kati ya njia panda ya kinondoni na Salenda bridge...

Usisimame hata kwa lolote.... Kuna jamaa alisimama kujisaidia pale kwenye kituo cha kuendea posta, walipotokea akakimbia, jamaa walimchomeka bisibisi mgongoni!
 
Hii ni aibu kubwa, police wako busy na kampeni
 
Jeshi letu la polisi lisifumbie macho uhalifu huu, waweke mtego wawanase hao wahalifu.
cc. Nyanda Dindai
 
KULE NI JEHANAMU WATAKUUA...

Polisi tusaidieni!
Ni mita ngapi kutoka ikulu ya nchi!?
Polisi labda wako kwenye maandalizi ya kusimamia uchaguzi nadhani wakimaliza hilo watahamia hilo eneo kudhibiti hali ya mambo. Sina uhakika hadi wakati huo watakuwa wameathirika raia wema wangapi!

 
Back
Top Bottom