Vatican: Je ‘Ubalozi’ unaeleweka?

ByaseL

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
2,225
247
http://changamoto.co.tz/index.php?o...nbyZvcHRpb249Y29tX2NvbnRlbnQmSXRlbWlkPTE1NA==Tuesday, 10 February 2009 http://changamoto.co.tz/index.php?v...t&print=1&page=&option=com_content&Itemid=154 http://changamoto.co.tz/index.php?v...ango&format=pdf&option=com_content&Itemid=154


VATICAN City State au kwa kifupi Vatican ni nchi yalipo makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani. Kesho inatimiza miaka 80 ya uhuru iliyoupata kutoka Italy.

Makala hii inatumia fursa hii kufafanua kilichozoeleka kuitwa ”Ubalozi wa Vatican”. Mwisho tutaona kuwa kumbe hawa si mabalozi wa Vatican. Je ni mabalozi wa nini? Nakushauri msomaji tuwe pamoja hadi mwisho.
Si ajabu kukutana na swali kuwa ni nini maslahi ya Ubalozi wa ‘Vatican’ hapa nchini wakati ni nchi ya kidini yaani Kanisa Katoliki.
Je, ni kweli Wakatoliki hatuulizi swali hili? Kwamba muuliza swali akificha jina basi tusidhani kwamba ni mkatoliki?

Hapana. Balozi wa ‘Vatican’ nchini Australia, Askofu Mkuu Charles Daniel Balvo anasimulia kwenye Sheria za Kanisa zinazohusu wawakilishi wa Papa ndani ya kitabu kiitwacho New Commentary on the Code of Canon Law kilichotolewa mwaka 2003 kwa ushirikiano wa Beal, Corriden na Green.
Ameeleza kwamba wakati wa Mtaguso (Vatican II) maaskofu walitaka ufafanuzi zaidi kuhusu kazi za mabalozi hawa baadhi wakipendekeza kuwa mpango wa kuendelea kuwa na mabalozi hauendi na wakati, hivyo ufutwe {Ukurasa. 491, aya ya sita}.

Mtaguso ni mkutano wa maaskofu wote duniani. Hapa nchini, Placidus Gervasius Nkalanga, Askofu Mstaafu wa Bukoba ndiye aliye hai aliyekuwa tayari ni askofu wakati wa Mtaguso. Kipindi hicho alikuwa ni Askofu Msaidizi wa Bukoba wakati Jimbo hilo likiongozwa na Laurian Kadinali Rugambwa.

Kanisa Katoliki ni dhehebu pekee ambalo makao yake makuu ni nchi (Sovereign territory). Kiongozi wa Kanisa (Papa) ndiye Mkuu wa nchi hiyo. Tujikumbushe nchi hiyo ilivyozaliwa.

Kanisa halikumiliki mali wala ardhi, hadi ilipofika mwaka 321BK umiliki uliruhusiwa. Wapo waliotoa majengo na ardhi kuwa mali ya Kanisa. Mnamo karne ya 16 Papa alipewa hata maeneo ambayo ni nchi azitawale. Nchi hizo zilizoitwa Papal States zilienea katikati ya Italy na mbili ndani ya Ufaransa yaani Venaissin na Avignon.

Dunia ilibadilika, Marekani ikajitawala (1776) na mapinduzi Ufaransa yalifuata miaka 15 baadaye. Mapinduzi hayo yaliteka zile Papal State mbili kuzifanya zisiwe tena miliki ya Papa.

Baada ya Ufaransa, huko Italy lilianza vuguvugu la kuunganisha tawala za Italy kuwa tawala moja. Papal States zilitekwa na hadi mwaka 1860 zilishamezwa na Italy mpya kasoro eneo la Roma alimoishi Papa.
Mwaka 1861 Italy mpya iliitangaza Roma kuwa Mji Mkuu na kuuteka Septemba 20, 1870. Hii ndiyo siku iliyofuta Papal States zilizodumu kwa karne kadhaa na mwaka uliofuata, Italy ilimtaka Papa kuwa chini ya mamlaka yake, japo haikumzuia kuteua mabalozi wanaomuwakilisha duniani.
Ilishindikana Papa kuwa chini ya Italy ikabidi abaki ndani ya eneo la Vatican yeye na waliomrithi wakijulikana kama mfungwa ndani ya Vatican. Hali ilibaki hivyo kwa miaka 60.

Hatimaye Februari 11, 1929 makubaliano yalifikiwa kwa jina la Mkataba wa Lateran. Eneo la Vatican likageuzwa kuwa nchi inayojitegemea (sovereign territory) chini ya Kanisa Katoliki.

Vatican ni nchi ndogo iliyozungukwa na jiji la Roma. Mpaka wa Tanzania unazidi kilomita 4,247 wakati unaoizunguka Vatican haufiki kilomita nne. Jijini Mwanza safari ya kutoka Benki Kuu hadi Mkuyuni inazidi ya kuizunguka Vatican.

Dar es Salaam kwenye barabara ya Morogoro, safari ya Fire au Zimamoto hadi daraja la Manzese pia ni zaidi ya kuizunguka Vatican.
Si rahisi kuuelewa ubalozi kwa sababu tu kuna nchi ya ”Vatican”. Ni lazima kujua taasisi iitwacho Holy See.

Sheria ya Kanisa inaifafanua ”Holy See” kwamba ”Holy See” ni Papa na idara zote za Roman Curia katika kuendesha Kanisa zima duniani (Can. 361).
Tayari tuna ufafanuzi kuhusu Vatican kama nchi na Holy See kama kikundi cha viongozi. Inawezekana kufafanua ubalozi katika hatua hii. Lakini pia tujadili hali inayoitwa Sovereignty. Sina hakika UHURU ndiyo tafsiri fasaha kwa neno hili.

Nadharia za Sovereignty zinakubaliana kwamba ni hali ya kuwa na mamlaka ya mwisho kuendesha serikali, nchi au watu. Mihimili kama serikali (executive), bunge(legislative) na mahakama (judiciary) hugawana uhuru huu wa ndani (Internal sovereignty). Majimbo ya Marekani yana uhuru huu wa ndani ambapo si lazima yafanane uendeshaji.
Uhuru wa kimataifa (External sovereignty) ni hali ya kutambulika na mataifa mengine pia kukidhi vigezo vya sheria za kimataifa (International laws).

Uhuru huu (Sovereignty) unaviweka wapi vyombo viwili, nchi ya Vatican na kingine kikiwa Holy See?
Vatican ina ardhi kama Tanzania japo ni ndogo. Tanzania ina haki ya kuweka mabalozi nchi za nje. Haki hii inaenda kwa Vatican City pia. Ni wazi ubalozi wao yabidi uitwe ”Ubalozi wa Vatican” (Vatican Embassy) na si vinginevyo.

Jambo la msingi kutambua ni kwamba, Holy See ndiyo inayosimamia mahusiano ya kidiplomasia kwa mujibu wa sheria za kimataifa, pia kupokea na kutuma mabalozi na wala si Vatican City State. Hivyo kuanzia sasa halitatumika tena neno “Ubalozi wa “Vatican” badala yake neno “Holy See” litatawala makala hii.

Ni haki kudadisi kwa nini Vatican isitoe mabalozi, jukumu hilo lifanywe na Holy See. Turejee neno Sovereignty tukiiangalia Holy See, uongozi wa Kanisa tangu kale. Papa au Holy See wameteua wawakilishi tangu karne ya nne.

Holy See imetambulika bila kuingiliwa kabla ya karne ya 16. Tumeona ilivyopata nchi zake, yaani Papal States. Ilipokuzwa dhana ya uhuru (Sovereign State), Holy See iliendelea kutambulika tayari ikiwa na Papal States. Ferdinando Cardinal d'Adda amekuwa balozi wa Papa (Holy See) nchini Uingereza Machi 03, 1687.

Kuepusha magomvi, mwaka 1815, Ulaya walikubaliana kuipitia upya ramani ya bara hilo katika mkutano wa Vienna (Congress of Vienna-1815). Kifungu (article) cha nne cha maamuzi kilimpa Nuncio au mwakilishi wa Papa (Holy See) hadhi kubwa ya kidiplomasia (dean) katika nchi anayopelekwa.
Papal States zilipofutwa na Italy (1870-1928), mapapa hawakuwa tena na nchi. Wala Vatican walimoishi haikuwa nchi. Kipindi chote hicho (miaka 60), Holy See imeendelea kutambuliwa uhuru wake (Sovereignty) na kupokelewa mabalozi wake walioteuliwa na Papa.

Pia mwaka 1961 Umoja wa Mataifa ulitoa makubaliano mapya ya kidiplomasia (Vienna Convention on Diplomatic Relations of 1961). Wawakilishi wa Papa wametajwa kwenye vifungu 14(1)(a) na 16(3). Balozi za Holy See huitwa Apostolic Nunciature of the Holy See.

Kuzaliwa kwa Vatican kuliiongezea Holy See chombo kingine huru (Sovereign) kwa vigezo vya kimataifa. Holy See ina umri wa karne nyingi. Vatican ndiyo kwanza inafikisha miaka 80. Hivyo, Holy See ni mzoefu mzuri duniani kwa masuala ya ubalozi kama si mmoja wa waanzilishi. Uhusiano wake (Nunciature) nchini Iraq ulianza Disemba 17, 1832 na Askofu Mkuu Henri-Marie Amanton akiwa mwanzilishi katika hadhi ya Apostolic Delegate. Holy See duniani ina ubalozi kwenye nchi 173, baadhi ni Iran, Yemen, Sudan, Morocco, Brazil n.k.

Holy See ina mahusiano maalum kwa Palestina na Russia. Pia ina mahusiano ya kibalozi na taasisi isiyo na nchi, lakini inatambulika huru iitwayo Sovereign Military Order of Malta (SMOM).
Vatican na Holy See ni vitu viwili tofauti vilivyo huru. Holy See imeteua mabalozi karne nyingi na imeendelea hivyo hata baada ya kuzaliwa Vatican City State.

Kwa uhuru (Sovereignty) uliopo Holy See na Vatican City State kila moja zaweza kutoa pasi za kusafiri (passport). Udogo wa Vatican na shughuli za Holy See havileti mazingira ya utoaji pasi mara kwa mara. Inapotokea, Holy See hutoa pasi maalum (Diplomatic passport).

Vatican City kama nchi yaweza kutoa pasi za kawaida (normal passports) japo yaelekea hilo limekabidhiwa kwa Holy See pia. Mahujaji kwenda Vatican hupata viza ya Italy kwenye ubalozi wa Italy.

Vatican City haijatangaza utaratibu wa kuteua mabalozi wakati utaratibu wa Holy See umo kwenye sheria za Kanisa, mabalozi wakiwa aina ya wawakilishi wa Papa au Papal Legates (Can. 363-367).
Hivyo ni vigumu kuhoji kwa nini nchi iwe na ubalozi wa Holy See. Yapo mawazo yanayofananisha kwa kuuliza ‘Mbona tuna ubalozi wa Vatican ambayo ni nchi ya kidini’?

Jibu la kwanza ni kwamba, hakuna ubalozi wa Vatican ila kuna ubalozi wa Holy See. Jibu la pili linahitaji msaada wetu tulio wakatoliki. Hata Vatican na Holy See zisitambuliwe kimataifa, bado mwakilishi huyu (Nuncio) anahitajika penye wakatoliki (Can. 362).
Nafasi yake kwa wakatoliki haitaathirika na kutotambuliwa huko. Masuala yetu atayafikisha kwa Papa kama kawaida. Itakayopotea ni hadhi yake ya kiubalozi tu.

Yeye ni sehemu ya utaratibu wa Kanisa. Nchi kuikubali hali yake ya kibalozi si suala la wakatoliki wala watanzania. Ni suala la Umoja wa Mataifa chini ya mkataba wa Vienna wa mwaka 1961.

Hivyo, swali hili halina tija kuwauliza wakatoliki au viongozi wa nchi ya Tanzania. Swali hili mahala pake ni Umoja wa Mataifa unaoweza kulijadili kwa uthabiti wa hoja itakavyojengwa.
Kila la heri Vatican City State kufikisha miaka themanini.

Source: ChangaMoto
 
Nadhani swali limejibiwa na makala. Ni Holy See na siyo Vatican City State.
 
Kwani Katiba ya Tanzania inaruhusu kitu kama hichi? Nahitaji kuelimishwa si vyenginevyo!


Ngekewa, ByaseL si kwamba anaileta hii thread kama ni mara ya kwanza. Mimi naamini nilielimika ilipokuja hii thread kwa mara ya kwanza mwaka jana

Ni moja ya makala za Joseph Misango kwenye TANZANIA DAIMA. Inaelekea kuwa ilitoka pia kwenye CHANGAMOTO.

Ninakumegea elimu ifuatayo na wewe uimege zaidi na zaidi.

Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 ndiyo uliowatambua mabalozi hawa ambao nyinyi mnawaita wa Vatican wakati ni wa Holy See.

Pia mwaka 1961 Umoja wa Mataifa ulitoa makubaliano mapya ya kidiplomasia (Vienna Convention on Diplomatic Relations of 1961). Wawakilishi wa Papa wametajwa kwenye vifungu 14(1)(a) na 16(3). Balozi za Holy See huitwa Apostolic Nunciature of the Holy See.!

Siku hizi mambo ya internet ni hadharani huna haja ya kuwanyenyekea Foreign Afairs kuupata mkataba huu. Hebu tuusome mkataba huu unaopatikana kwa ku-click hapa. Na utaona vifungu 14(1) na 16(3) vinasema hivi:

****************
Article 14:

1.Heads of mission are divided into three classes, namely:
(a) That of ambassadors or nuncios accredited to Heads of State, and other heads of mission of
equivalent rank;

(b) That of envoys, ministers and internuncios accredited to Heads of State;

(c) That of chargés d'affaires accredited to Ministers for Foreign Affairs.

****************
Article 16 (3):

This article is without prejudice to any practice accepted by the receiving State regarding the precedence of the representative of the Holy See.

****************

Nadhani hadi hapo ni elimu kamili.

Utaona kwamba mkataba huu ni wa wanachama wote wa Umoja wa Mataifa (UN). Hivyo Tanzania ilijiunga na UN na ikauridhia mkataba huu kama yalivyoridhia mataifa yote duniani bila taifa lolote kupinga hata nukta.

Hivyo katiba ya Tanzania inautambaua Umoja wa Mataifa na hivyo inaukubali mkataba huu.

Siku UN itakapoacha kuwatambua mabalozi hawa (nuncios) basi ndipo Tanzania itapata nguvu kutowatambua hawa mabalozi wa Holy See.

Vinginevyo kama Tanzania haiwataki basi jengeni hoja kwenye UN kwamba mabalozi hawa ni kero na ule mkataba wa Vienna ubatilishwe.

Mkishindwa, basi Tanzania hamlazimiki kuwa mwanachama wa UN. Jiondoeni kwenye Umoja wa Mataifa muende kivyenuvyenu ili muondokane na mabalozi hawa mnaodhani ni wa Vaitcan kumbe ni wa Holy See.

Mabalozi ambao hawaonekani jambo geni isipokuwa Tanzania ambako kila kitu ni jambo geni tangu waraka hadi mabalozi na sijui ni nini tena kitaonekana kigeni.
 
Hapa Kwetu tuna mwakilishi gani kati ya vyombo viwili hivi?

Unaweza pia kusoma hii ili kupanua uelewa:

Diplomatic missions of the Holy See

This is a list of diplomatic missions of the Holy See. Since the fifth century, long before the founding of the Vatican City State in 1929, papal envoys (now known as nuncios) have represented the Holy See to foreign potentates. Additionally, papal representatives known not as nuncios but as apostolic delegates ensure contact between the Holy See and the Catholic Church in countries that do not have diplomatic relations with the Holy See.

At present, there is one residential apostolic delegate, for Jerusalem and Palestine, as well as non-residential ones for seven countries (Botswana, Brunei, Burma, Laos, Malaysia, Mauritania, Somalia) and for the territories and countries without diplomatic relations in three regions (Arabian Peninsula, the Caribbean, the Pacific Ocean).

Vietnam is also listed in the Annuario Pontificio as having an apostolic delegation, but the post of apostolic delegate has been vacant for several decades. In keeping with the "one China" policy, no representative, whether nuncio or apostolic delegate, is appointed for mainland China, since the Holy See is represented in Taipei by an apostolic nunciature, headed not by a nuncio, but only by a chargé d'affaires. Many countries, such as the United States, for which apostolic delegates were once appointed, now have nuncios.

As well as the countries mentioned above as having apostolic delegations, Afghanistan, Bhutan, People's Republic of China, North Korea, Oman, Saudi Arabia and Tuvalu do not have diplomatic relations with the Holy See.

In most respects the status of the diplomatic missions of the Holy See are identical with those of other countries, with the exception of the nomenclature: apostolic nuncios have ambassadorial rank and apostolic nunciatures are ranked as embassies.

However, in most countries of central and western Europe and of southern and central America, as well as in a few countries elsewhere, the nuncio is granted precedence over other ambassadors and is dean of the diplomatic corps from the moment he presents his credentials. The Holy See, which does not issue visas, does not have consulates.

Apostolic delegates and their missions do not have diplomatic status.

In countries where that is permitted, the apostolic nunciature is sometimes, though rarely, located outside the capital, perhaps in towns with particularly important religious connections, such as the village of Rabat in Malta where Saint Paul's grotto exists, and Harissa in Lebanon where Maronite, Greek Orthodox and Melkite Greek Catholic Church authorities are located.

In other countries that is not permitted: when India opened diplomatic relations with the Holy See, what until that moment was an apostolic delegation moved from Bangalore to the capital, New Delhi; and in Australia the mission moved from Sydney to Canberra.

Listed below are the Holy See's apostolic nunciatures, apostolic delegations, and observer or representative missions to international governmental organizations — such as the United Nations, the Council of Europe and the Arab League — with the names of the head officials in the Annuario Pontificio.

Europe
Apostolic Nunciature in Tirana, Albania
Apostolic Nunciature in Berlin
Apostolic Nunciature in Paris
Apostolic Nunciature in Prague Albania
Tirana (Apostolic Nunciature)

Austria
Vienna (Apostolic Nunciature)

Belarus
Minsk (Apostolic Nunciature)

Belgium
Brussels (Apostolic Nunciature)

Bosnia and Herzegovina
Sarajevo (Apostolic Nunciature)

Bulgaria
Sofia (Apostolic Nunciature)

Croatia
Zagreb (Apostolic Nunciature)

Cyprus
Nicosia (Apostolic Nunciature)

Czech Republic
Prague (Apostolic Nunciature)

France
Paris (Apostolic Nunciature)
Strasbourg (Office)

Georgia
Tbilisi (Apostolic Nunciature)

Germany
Berlin (Apostolic Nunciature)

Greece
Athens (Apostolic Nunciature)

Hungary
Budapest (Apostolic Nunciature)

Ireland
Dublin (Apostolic Nunciature)

Italy
Rome (Apostolic Nunciature)

Lithuania
Vilnius (Apostolic Nunciature)

Malta
Rabat (Apostolic Nunciature)

Netherlands
The Hague (Apostolic Nunciature)

Poland
Warsaw (Apostolic Nunciature)

Portugal
Lisbon (Apostolic Nunciature)

Romania
Bucharest (Apostolic Nunciature)

Russia
Moscow (Apostolic Nunciature)

San Marino
San Marino (Apostolic Nunciature)

Serbia
Belgrade (Apostolic Nunciature)

Slovakia
Bratislava (Apostolic Nunciature)

Slovenia
Ljubljana (Apostolic Nunciature)

Spain
Madrid (Apostolic Nunciature)

Sweden
Stockholm (Apostolic Nunciature)

Switzerland
Berne (Apostolic Nunciature)

Ukraine
Kiev (Apostolic Nunciature)

United Kingdom
London (Apostolic Nunciature)

Uzbekistan
Tashkent (Apostolic Nunciature)

North America
Apostolic Nunciature in Ottawa Canada
Ottawa (Apostolic Nunciature)

Costa Rica
San José (Apostolic Nunciature)

Cuba
Havana (Apostolic Nunciature)

Dominican Republic
Santo Domingo (Apostolic Nunciature)

El Salvador
San Salvador (Apostolic Nunciature)

Guatemala
Guatemala City (Apostolic Nunciature)

Haiti
Port au Prince (Apostolic Nunciature)

Honduras
Tegucigalpa (Apostolic Nunciature)

Mexico
Mexico City (Apostolic Nunciature)

Nicaragua
Managua (Apostolic Nunciature)

Panama
Panama City (Apostolic Nunciature)

Trinidad and Tobago
Port of Spain (Apostolic Nunciature)

United States
Washington DC (Apostolic Nunciature)

South America
Apostolic Nunciature in Brasília
Apostolic Nunciature in Buenos Aires Argentina
Buenos Aires (Apostolic Nunciature)

Bolivia
La Paz (Apostolic Nunciature)

Brazil
Brasília (Apostolic Nunciature)

Chile
Santiago (Apostolic Nunciature)

Colombia
Bogotá (Apostolic Nunciature)

Ecuador
Quito (Apostolic Nunciature)

Paraguay
Asunción (Apostolic Nunciature)

Peru
Lima (Apostolic Nunciature)

Uruguay
Montevideo (Apostolic Nunciature)

Venezuela
Caracas (Apostolic Nunciature)



Africa
Algeria
Algiers (Apostolic Nunciature)

Angola
Luanda (Apostolic Nunciature)

Benin
Cotonou (Apostolic Nunciature)

Burundi
Bujumbura (Apostolic Nunciature)

Cameroon
Yaounde (Apostolic Nunciature)

Central African Republic
Bangui (Apostolic Nunciature)

Chad
N'Djamena (Apostolic Nunciature)

Republic of the Congo
Brazzaville (Apostolic Nunciature)

Democratic Republic of the Congo
Kinshasa (Apostolic Nunciature)

Côte d'Ivoire
Abidjan (Apostolic Nunciature)

Egypt
Cairo (Apostolic Nunciature)

Ethiopia
Addis Ababa (Apostolic Nunciature)

Gabon
Libreville (Apostolic Nunciature)

Ghana
Accra (Apostolic Nunciature)

Guinea
Conakry (Apostolic Nunciature)

Kenya
Nairobi (Apostolic Nunciature)

Madagascar
Antananarivo (Apostolic Nunciature)

Morocco
Rabat (Apostolic Nunciature)

Mozambique
Maputo (Apostolic Nunciature)

Nigeria
Abuja (Apostolic Nunciature)

Rwanda
Kigali (Apostolic Nunciature)

Senegal
Dakar (Apostolic Nunciature)

South Africa
Pretoria (Apostolic Nunciature)

Sudan
Khartoum (Apostolic Nunciature)

Tanzania
Dar Es Salaam (Apostolic Nunciature)

Uganda
Kampala (Apostolic Nunciature)

Zambia
Lusaka (Apostolic Nunciature)

Zimbabwe
Harare (Apostolic Nunciature)

Middle East
Iran
Tehran (Apostolic Nunciature)

Iraq
Baghdad (Apostolic Nunciature)

Israel
Tel Aviv (Apostolic Nunciature)

Jordan
Amman (Apostolic Nunciature)

Kuwait
Kuwait City (Apostolic Nunciature)

Lebanon
Harissa (Apostolic Nunciature)

Palestinian Authority
Jerusalem (Apostolic Delegation)

Syria
Damascus (Apostolic Nunciature)

Turkey
Ankara (Apostolic Nunciature)

Asia
Bangladesh
Dhaka (Apostolic Nunciature)

Republic of China (Taiwan)
Taipei (Apostolic Nunciature)

India
New Delhi (Apostolic Nunciature)

Indonesia
Jakarta (Apostolic Nunciature)

Japan
Tokyo (Apostolic Nunciature)

Kazakhstan
Astana (Apostolic Nunciature)

Kyrgyzstan
Bishkek (Apostolic Nunciature)

South Korea
Seoul (Apostolic Nunciature)

Pakistan
Islamabad (Apostolic Nunciature)

Philippines
Manila (Apostolic Nunciature))

Singapore
Singapore (Apostolic Nunciature)

Sri Lanka
Colombo (Apostolic Nunciature)

Thailand
Bangkok (Apostolic Nunciature)

Oceania
Apostolic Nunciature in Canberra Australia
Canberra (Apostolic Nunciature)

New Zealand
Wellington (Apostolic Nunciature)

Papua New Guinea
Port Moresby (Apostolic Nunciature)

http://en.wikipedia.org/wiki/List_of_diplomatic_missions_of_the_Holy_See
 
Iran
Tehran (Apostolic Nunciature)

Kama Iran wana Balozi wa Papa ( Sijui niko sahihi?), Sehemu ambako ni moja kati jamii ya watu walio karibu zaidi na Allah sasa Kelele za nini Tanzania?
 
Kama Iran wana Balozi wa Papa ( Sijui niko sahihi?), Sehemu ambako ni moja kati jamii ya watu walio karibu zaidi na Allah sasa Kelele za nini Tanzania?

Mimi naona uko sahihi kusema Ubalozi wa Papa. Hawa watanzania wanaopiga kelele ndio walewale ninaowaweka katika kundi la kuona kila kitu ni kigeni kwani nchi za kiislamu kwelikweli husikii hata nukta ya kelele zile.

Huko hawapigi kelele kwani hata nyaraka zikiandikwa hutawasikia. Tatizo ni ushamba wa wanaodhani mambo haya ni mageni kumbe wao ndiyo wageni katika exposure ya mambo ya dunia hii.
 
Back
Top Bottom