Uzito wa Zitto, Wepesi wa Hoja kwa Suala zito

Mchambuzi

JF-Expert Member
Aug 24, 2007
4,850
9,405
Suala la Zitto kutangaza nia yake kuwania Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema Uchaguzi Mkuu Ujao wa mwaka 2015, limepokewa kwa hisia na tafsiri mbalimbali ndani ya Jamii; Pamoja na mgawanyiko huu wa hisia na tafsiri, mgawanyiko mkubwa upo katika kambi kuu mbili; Kambi ya Kwanza ni ile inayo muunga Mkono Zitto kwa uamuzi huu, wakiwepo viongozi kadhaa ndani ya Chadema; Kambi ya Pili ni ile inayo mpinga Zitto kwa uamuzi huu, akiwemo Mwasisi wa Chadema, Mzee Edwin Mtei;

Mgawanyiko wa kambi hizi kubwa, unatoa picha moja kubwa kwamba: Zitto ni Mgombea mwenye Uzito Mkubwa; Lakini pamoja na Uzito Huu Wa Zitto katika suala husika, Uzito uliopelekea Jamii kugawanyika katika kambi hizi kubwa mbili, bado hoja zinazotolewa na kambi zote – ama za kumpinga au za kumuunga mkono Zitto katika uamuzi wake huu mzito, badala ya kutawaliwa na uzito wa hoja, zinatawaliwa na wepesi wa hoja;

Tukianza na Upande wa Kwanza wa Hoja:

Upande huu ni ule unao mpinga Zitto; Wepesi wa hoja za kambi hii katika suala hili Zito linalohusu Urais wa Nchi ni kwamba, hoja hizi hazinukuu, na wala hazitoi mrejeo wowote kwa UMMA, kuelimisha iwapo Uamuzi Mzito wa Zitto unakiuka KANUNI zozote za Chadema; Wepesi huu wa hoja unapelekea maswali makuu matano kwa kambi hii, inayopinga Uamuzi wa Zitto; JE:

  1. Pingamizi hii inatokana na Zitto kukiuka Kanuni Yoyote Ya Chadema KIKATIBA?
  2. Kama Jibu ni NDIO, Zitto Amekiuka Kanuni ipi?
  3. Adhabu ya Kukiuka Kanuni Hii Ya Kikatiba ni ipi?
  4. Maamuzi Juu ya Adhabu hiyo hufanywa na Kikao Kipi?
  5. Kwanini Zitto Anapingwa Barabarani na Vibarazani Badala ya Ndani Ya Kikao Hiki?

Tukihamia Kwenye Upande wa Pili wa Hoja:

Upande huu ni ule unaomuunga mkono Zitto; Wepesi wa hoja za kambi hii kwa suala hili Zito linalohusu Urais wa Nchi ni kwamba, hoja hizi haziakisi matarajio na matamanio ya wananchi walio wengi katika Tanzania ya leo, hasa kuelekea mwaka 2015; Wepesi huu wa hoja unapelekea maswali makuu manne kwa kambi inayo unga Mkono Uamuzi wa Zitto; JE:


  1. Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Suala La Mfumo Wa Muungano?
  2. Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Mfumo wa Uchumi Wa Nchi, ambapo kwa upande mmoja, wapiga kura wengi ni wale Waliosalitiwa na Ujamaa, na kwa upande wa Pili, Wagombea Urais kutoka Vyama Vyote Vya Siasa Wanaendesha Maisha Yao Kiliberali na Kibepari?
  3. Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Miiko ya Uongozi, Hasa Suala La Rushwa?
  4. Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Katiba Mpya, hasa nini kiwemo na nini kisiwemo, pamoja na mkakati wake wa kusimamia na kuyalinda hayo?

Ni matumaini yangu kwamba, majibu kwa maswali haya yatasaidia kambi hizi kuu mbili kuja na hoja nzito ama Kumpinga, au Kumuunga Mkono Zitto Katika nia yake ya kuwania Urais wa Tanzania, 2015, badala ya kuendelea kutawaliwa na Wepesi wa hoja katika suala hili Zito;

Mbali ya Zitto, hata huko mbeleni tujitahidi kupima wagombea wengine wote kutoka vyama vyote kwa mwendo huu, kwani kwa kufanya hivyo, tutahamia katika ushindani wa siasa wenye tija kwa wananchi kwa maana ya kwamba - SIASA ZA MASUALA - ZINAZOLINGANISHA MASUALA NA WATU (WAGOMBEA) badala ya SIASA ZA WATU (WAGOMBEA) - ZINAZOLINGANISHA WATU NA WATU (WAGOMBEA), kama ilivyo sasa;
 
Mchambuzi hoja ya watu kumpinga Zitto zipo hivi;

Ielelweke kuwa Zitto hajavunja kanuni yoyote ya chama au katiba ya CDM kutangaza kugombea urais 2015. Tatizo linakuja, hajafanya "proper timing" ya yeye kutangaza suala hilo. Leo ni 2012, mpaka 2015 bado safari ni ndefu sana upepo wa kisiasa unaweza kuvuma vyovyote.

In connection to that, CCM inateswa na mzimu wa urahisi 2015. Sasa kitendo cha yeye kutangaza hilo maana yake hajajifunza makosa ya CCM kukesha kulumbana, kuhujumiana n.k kwa sababu ya urais tu!!!!! Sasa kwa nini yeye asijifunze kutoka kwa wapinzani CCM?????

Mimi ningeomba Zitto aelewe mpaka sasa CDM haijasema itamsimamisha nani kwa sababu inajua kazi kubwa iliyopo mbele yake ya kuchanga karata yake vizuri katika kipindi kilichobaki ili 2015 mambo yaende kama ndoto zao zilivyo yaani kushika dola.

Nijuavyo Zitto ni mjuvi sana na si kwamba haya tusemayo hayajui ila sielewi ni kwa nini anafanya hivi. Namtahadharisha asidhani CCM tayari imeshindwa 2015 kiasi cha kung'ang'ania au kugombea urais kiasi hicho.

Namuombea kwa Mungu ampe uhai na hekima ili KUDRA ya Mwenyezi Mungu ifanye kazi.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi hoja ya watu kumpinga Zitto zipo hivi;

Ielelweke kuwa Zitto hajavunja kanuni yoyote ya chama au katiba ya CDM kutangaza kugombea urais 2015. Tatizo linakuja, hajafanya "proper timing" ya yeye kutangaza suala hilo. Leo ni 2012, mpaka 2015 bado safari ni ndefu sana upepo wa kisiasa unaweza kuvuma vyovyote.
Kwa upande huu unaompinga, Zitto akifanya timing mbaya si ni kheri kwa kambi hii? Au maana yako ni kwamba wangependelea agombee lakini asubiri kwanza? Kwa Zitto, nini faida za kusuburi na nini faida za kuwahi, iwapo kichama, hasa kikatiba, hakuna muda maalum wa kuruhusu wanachama na viongozi kutanganza nia?

In connection to that, CCM inateswa na mzimu wa urahisi 2015. Sasa kitendo cha yeye kutangaza hilo maana yake hajajifunza makosa ya CCM kukesha kulumbana, kuhujumiana n.k kwa sababu ya urais tu!!!!! Sasa kwa nini yeye asijifunze kutoka kwa wapinzani CCM?????
Wapo wanaojenga hoja kwamba Dr. Slaa angetangazwa mapema pengine angeweza kushinda; tukiacha hoja ya uchakachuaji wa kura pembeni kwa sasa, nini mtazamo wako juu ya hili?

Mimi ningeomba Zitto aelewe mpaka sasa CDM haijasema itamsimamisha nani kwa sababu inajua kazi kubwa iliyopo mbele yake ya kuchanga karata yake vizuri katika kipindi kilichobaki ili 2015 mambo yaende kama ndoto zao zilivyo yaani kushika dola.

Hili kwahiyo ni suala la common sense ambalo hali hitaji kanuni, hivyo Zitto hana common sense?

Nijuavyo Zitto ni mjuvi sana na si kwamba haya tusemayo hayajui ila sielewi ni kwa nini anafanya hivi. Namtahadharisha asidhani CCM tayari imeshindwa 2015 kiasi cha kung'ang'ania au kugombea urais kiasi hicho.

Iwapo ana sifa hizi unazompa, basi ni dhahiri pia ana uwezo mkubwa wa kufanya COST-BENEFIT ANALYSIS, amelikamilisha hilo, na ameona kuna umuhimu wa kuchukua maamuzi aliyochukua;

Namuombea kwa Mungu ampe uhai na hekima ili KUDRA ya Mwenyezi Mungu ifanye kazi.
Amina.
 
Huyu Zitto amewalipa bei gani? Manake kutwa kuchwa mnamjadili!! Hebu subirini 2mzike kamanda balo kwanza hiki ni kipindi cha majonzi makubwa kwa Taifa!!
 
Mchambuzi umetoa ufafanuzi mzuri, nadhani ni wakati muafaka wa Zitto kuweka misimamo yake hadharani juu ya masuala nyeti kama muungano nk ili watu wajue amesimama wapi.
 
mchambuzi umetoa ufafanuzi mzuri, nadhani ni wakati muafaka wa zito kuweka misimamo yake hadharani juu ya masuala nyeti kama muungano nk ili watu wajue amesimama wapi.

Upo sahihi Peri, kwani vile vile itatusaidia kuingia katika Siasa za kujadili MASUALA KWA KULINGANISHA NA WATU badala ya Siasa za WATU KWA KULINGANISHA NA WATU; Hii ndio nia ya uzi wangu huu;
 
Kwa upande huu unaompinga, Zitto akifanya timing mbaya si ni kheri kwa kambi hii? Au maana yako ni kwamba wangependelea agombee lakini asubiri kwanza? Kwa Zitto, nini faida za kusuburi na nini faida za kuwahi, iwapo kichama, hasa kikatiba, hakuna muda maalum wa kuruhusu wanachama na viongozi kutanganza nia?

Au maana yako ni kwamba wangependelea agombee lakini asubiri kwanza? Hiyo ndiyo maana yangu. Kwa nini????

Tunaangalia impact ya yeye kutangaza au kukaa kimya ndani ya chama. Ni wazi kutangaza kumeibua malumbano ambayo siyo ya msingi na yanaweza kuondoa unit iliyojengwa muda mrefu sana. Kwa mantiki hiyo, angeweka nia yake kama kawaida na kuweka mtandao wake kwa ajili ya ushindani pindi muda ukifika. Vile vile kwake binafsi, anakuwa ametangaza vita kubwa unnecessarily, mfano unaweza kuundiwa makashfa mengi yasiyo ya msingi na kumuundia usumbufu usio wa lazima kujibia vitu ambavyo vinatoka na "dirty game in politics"


Dr. Slaa anaamika zaidi chamani zaidi kwa kuwa amekuwa yupo wazi zaidi misimamo yake kuliko Zitto. Kiasi fulani Zitto amekuwa mtata na amekuwa hajali hilo na kiasi fulani kuhisiwa kuwa huenda ni chaguo la CCM katika kipindi hiki ambacho upinzani umekuwa ukikuwa kwa kasi na kujenga nadharia CCM lolote linaweza kutokea.

Mtazamo wangu, kama Dr. Slaa akitangaza kugombea uraisi litakuwa ni kosa kubwa sana kwa kuwa hautakuwa ni wakati muafaka. Ningeomba katika hilo, CDM wajifunze kwa Lowassa, kila mtu anajua Lowasa anautaka urais lakini yeye hajawahi kukiri hilo au kutangaza hadharani badala yake anafanyia kazi nia yake chamani na kisha baadae kwa wapiga kura mambo yakinyooka.


Pamoja na yote hayo, COST - BENEFIT ANALYSIS unayoisemea haijafanya vizuri vya kutosha, labda hapa angeruhusu mlango wa ushauri ili aone nini cha kufanya. Lakini kwa uzoefu wangu, Zitto ni mgumu wa kushaurika hasa kutokana na sifa aliyojijengea, labda anaona amemaliza kila kitu.
 
Zitto is nothing but a mere traitor undermining his Party in favour of his masters if anything he deserves no such a prominent coverage every now and again.
Soon or later we shall see where he belongs
 
Ungetaka kuwa fair kwenye mada yako,ungeitaja na kambi ya magamba inayomuunga mkono.

Hoja nzuri lakini kwa vile hii ni hatua ya awali ambayo inahusisha mchakato na siasa za ndani za chama, sikuona sababu ya kufanya hivyo kwani mwisho wa siku, uamuzi wa kumsimamisha au kutomsimamishwa utafanywa na Chadema, sio CCM, NCCR, CUF, CCK, au vyama vingine vya Siasa;
 
Hoja nzuri lakini kwa vile hii ni hatua ya awali ambayo inahusisha mchakato na siasa za ndani za chama, sikuona sababu ya kufanya hivyo kwani mwisho wa siku, uamuzi wa kumsimamisha au kutomsimamishwa utafanywa na Chadema, sio CCM, NCCR, CUF, CCK, au vyama vingine vya Siasa;
Kwahiyo hatuna haja ya kuzihusisha hoja za nyie wana CCM? Si tunazungumzia wepesi vs uzito wa hoja? Hilo tu lingekufanya useme tuzungumzie hoja zote bila kujali vyama.

Kwasababu sasa una imply kwamba matatizo haya ni ya ndani ya chama, where as kuna wanaoamini kuwa yameanzia nje ya chama ie magamba. Na ndiyo maana nikasema ili mjadala "uwe fair, ungeinclude na wale wanaomsapoti ama kumpinga,walioko ccm,ama cuf ukipenda.

Just ushauri.
 
Kwahiyo hatuna haja ya kuzihusisha hoja za nyie wana ccm?Si tunazungumzia wepesi vs uzito wa hoja?Hilo tu lingekufanya useme tuzungumzie hoja zote bila kujali vyama.

Kwasababu sasa una imply kwamba matatizo haya ni ya ndani ya chama,where as kuna wanaoamini kuwa yameanzia nje ya chama ie magamba.Na ndiyo maana nikasema ili mjadala "uwe fair,unge include na wale wanaomsapoti ama kumpinga,walioko ccm,ama cuf ukipenda. Just ushauri.

Hoja ya kumpinga mgombea wa chama chochote kutangaza nia itakuwa ni hoja nzito iwapo tu ni suala la KIKANUNI/KATIBA; Hoja ya kumuunga mgombea itakuwa ni hoja nzito iwapo tu inahusisha msimamo wake vis a vis matarajio na matumaini ya wananchi walio wengi; Nje ha hapo, mjadala huu utaenda kinyume na kilichokusudiwa, na isitoshe, uliyoyazungumza yameshajadiliwa sana elsewhere;
 
Hoja ya kumpinga mgombea wa chama chochote kutangaza nia itakuwa ni hoja nzito iwapo tu ni suala la KIKANUNI/KATIBA; Hoja ya kumuunga mgombea itakuwa ni hoja nzito iwapo tu inahusisha msimamo wake vis a vis matarajio na matumaini ya wananchi walio wengi; Nje ha hapo, mjadala huu utaenda kinyume na kilichokusudiwa, na isitoshe, uliyoyazungumza yameshajadiliwa sana elsewhere;


Mkuu Mchambuzi unaongelea vitu ambavyo najua wewe unaelewa ila kwa sababu labda ambazo haziko wazi, unachokoza watu tu ili waseme!

Naomba nikupe mifano kidogo....

Mwaka 2000, Mh. Nchimbi (akiwa mwenyekiti wa UVCCM) alisimama jukwaani akasema kuwa mtu atakayempinga Mkapa kuomba kipindi cha pili watampopoa mawe.

Na Malecela wakati huo akiwa makamu wa mwenyekiti wa CCM akasema kuwa hawaturuhusu mtu kumpinga Mkapa...Shibuda alijaribu ila watu wote walijua kuwa alikuwa anafanya usanii....

Na kutokana na misimamo hiyo, Mkapa hakupingwa tofauti na ilivyokuwa 1995 au kwa JK 2005 ambapo watu kibao walichukua fomu kugombea urais kupitia CCM....Je kuna KANUNI yoyote ya CCM inayowazuia watu kumchallenge rais anayetaka kugombea kipindi cha pili?

Bilal alijaribu kumchallenge Karume kwenye kipindi cha pili, kwa nini CCM hawakurudisha jina lake?

Baada ya kusema hayo, naomba nikueleze kuwa kila jamii au kikundi kinakuwa na norms zake na hizi huwezi kukuta zimeandikwa popote.

Ndo maana kule kwetu, mtoto akijamba wakati wa chakula mbele ya watu wazima, zawadi yake ni kwenzi kichwani ili next time ajifunze kuwa na adabu watu wanapokuwa mezani!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mchambuzi unaongelea vitu ambavyo najua wewe unaelewa ila kwa sababu labda ambazo haziko wazi, unachokoza watu tu ili waseme!

Naomba nikupe mifano kidogo....

Mwaka 2000, Mh. Nchimbi (akiwa mwenyekiti wa UVCCM) alisimama jukwaani akasema kuwa mtu atakayempinga Mkapa kuomba kipindi cha pili watampopoa mawe.

Na Malecela wakati huo akiwa makamu wa mwenyekiti wa CCM akasema kuwa hawaturuhusu mtu kumpinga Mkapa...Shibuda alijaribu ila watu wote walijua kuwa alikuwa anafanya usanii....

Na kutokana na misimamo hiyo, Mkapa hakupingwa tofauti na ilivyokuwa 1995 au kwa JK 2005 ambapo watu kibao walichukua fomu kugombea urais kupitia CCM....Je kuna KANUNI yoyote ya CCM inayowazuia watu kumchallenge rais anayetaka kugombea kipindi cha pili?

Bilal alijaribu kumchallenge Karume kwenye kipindi cha pili, kwa nini CCM hawakurudisha jina lake?

Baada ya kusema hayo, naomba nikueleze kuwa kila jamii au kikundi kinakuwa na norms zake na hizi huwezi kukuta zimeandikwa popote.

Ndo maana kule kwetu, mtoto akijamba wakati wa chakula mbele ya watu wazima, zawadi yake ni kwenzi kichwani ili next time ajifunze kuwa na adabu watu wanapokuwa mezani!!

Kwa kweli sijakuelewa; Unaweza ukafananisha Masuala ya Mkapa na Bilal na hili la Zitto kwa lugha nyepesi na ya moja kwa moja ili nikusome vizuri? Vinginevyo natazama hoja za kumpinga na Kumuunga Mkono Zitto kwa Kanuni, Katiba na Msimamo wake katika masuala yanayogusa wananchi walio wengi; Hii itasaidia kwanza, kuwa fair kwake, pili kubaini nguvu ya candidature yake ndani ya chama na tatu, kuweza baini uwezekano wake wa kukubalika na kuwa na mvuto kwa wapiga kura wengi iwapo atasimamishwa na chama chake cha Chadema;

Mada yangu hailengi kumjadili mtu kwa kumlinganisha na mtu bali mtu kwa kumlinganisha na masuala yenye maslahi kwa wapiga kura;
 
Kwa kweli sijakuelewa; Unaweza ukafananisha Masuala ya Mkapa na Bilal na hili la Zitto kwa lugha nyepesi na ya moja kwa moja ili nikusome vizuri? Vinginevyo natazama hoja za kumpinga Zitto kwa Kanuni, Katiba na Msimamo wake katika masuala yanayogusa wananchi walio wengi; Hii itasaidia kubaini nguvu ya candidature yake ndani ya chama na vile vile uwezo wa kukubalika na wapiga kura wengi iwapo atasimamishwa; Mada yangu hailengi kumjadili mtu kwa kumlinganisha na mtu bali mtu kwa kumlinganisha na masuala yenye maslahi kwa wapiga kura;

Mimi sijamlinganisha Zitto na mtu yeyote...ila nimejaribu kukupa mifano ambayo inaonesha kuwa siyo kila kitu kinachofanywa na jamii kiwe kimefafanuliwa katika kanuni za kwenye vitabu.

Na pia nikahitimisha kwa kukueleza kuwa lazima jamii iwe na norms ambazo zinaelekeza timing ya kufanya mambo...Huwezi kuwaacha watoto wakajamba jamba hovyo wakati wa chakula.

Hayo mambo ya kujadili uwezo wa mgombea mnayataka kwa CHADEMA ila siyo kwa CCM...?? Au unasemaje wewe??
 
Mimi sijamlinganisha Zitto na mtu yeyote...ila nimejaribu kukupa mifano ambayo inaonesha kuwa siyo kila kitu kinachofanywa na jamii kiwe kimefafanuliwa katika kanuni za kwenye vitabu.

Na pia nikahitimisha kwa kukueleza kuwa lazima jamii iwe na norms ambazo zinaelekeza timing ya kufanya mambo...Huwezi kuwaacha watoto wakajamba jamba hovyo wakati wa chakula.

Niseme tu kwamba mimi sina ufahamu iwapo katika demokrasia ya kiliberali ambayo ndio tunaifuata, suala la timing katika suala tunalojadili, linakuwa treated vipi, hasa ikizingatiwa kwamba hakuna a universal approach katika suala hili, hata katika mfumo unwritten...; ndio maana narudi kwenye Kanuni;

Hayo mambo ya kujadili uwezo wa mgombea mnayataka kwa CHADEMA ila siyo kwa CCM...au unasemaje wewe??
Kama ukiamua kunisoma vizuri, mada yangu hailengi kumjadili MTU kwa Kumfananisha na MTU, bali MTU na Masuala, kwanza ya ndani KIKANUNI na KIKATIBA na vile vile kwa nje, Msimamo wake dhidi ya MASUALA ambayo yanazunguka maisha ya wananchi wa leo;

Vinginevyo Siasa za timing katika ugombea Urais, zilizaliwa CCM, na inanishangaza kwanini Chadema wanaiga utamaduni huu na sina uhakika kama una manufaa; Ningeomba unielimishe zaidi juu ya hili;
 
Kwa sababu zinatawaliwa na hoja zenye wepesi katika suala zito;

Mchambuzi,Tutamjadili Zitto Kabwe kugombea urais wa Tanzania atakapofikisha umri ambao kikatiba unamruhusu, kwa sasa katiba haimruhusu Zitto Kabwe kugombea urais kwa vile yuko chini ya umri wa miaka 40. Hata 2015 kama kifungu cha katiba kuhusu umri wa kugombea urais Tanzania usipofanyiwa marekebisho bado hatakuwa na nafasi hiyo.

Bora Zitto na wanamwunga mkono wangehangaikia Katiba mpya kufanyiwa marekebisha badala ya kuhangaikia kitu ambacho kikatiba ni ukiukwaji.

Hiyo ni hoja nzito ambayo inagusa Katiba ya nchi kuhusu umri wa mgombea Urais
 
Mchambuzi,Tutamjadili Zitto Kabwe kugombea urais wa Tanzania atakapofikisha umri ambao kikatiba unamruhusu, kwa sasa katiba haimruhusu Zitto Kabwe kugombea urais kwa vile yuko chini ya umri wa miaka 40. Hata 2015 kama kifungu cha katiba kuhusu umri wa kugombea urais Tanzania usipofanyiwa marekebisho bado hatakuwa na nafasi hiyo.

Bora Zitto na wanamwunga mkono wangehangaikia Katiba mpya kufanyiwa marekebisha badala ya kuhangaikia kitu ambacho kikatiba ni ukiukwaji.

Hiyo ni hoja nzito ambayo inagusa Katiba ya nchi kuhusu umri wa mgombea Urais

Upo sahihi, hii ni hoja nzito, sio hoja nyepesi; Pengine ana matarajio kwamba kigezo hiki kitatenguliwa ndani ya katiba mpya, lakini kama ulivyosema, hadi ifikie huko, as we stand, Zitto hawezi kuwa Rais wa Tanzania kwa vile Katiba haimruhusu kutokana na suala la ugombea; Lakini swali langu linalofuata kwako ni je, pingamizi ndani ya chama chake zinatokana na Chadema pia kuheshimu kigezo kilichopo ndani ya katiba ya nchi? Au kuna lingine Kikanuni na Kikatiba?
 
Back
Top Bottom