GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 63,061
- 126,626
Lakini JK alitakiwa awe Kahama Shinyanga kwenye maafa ya mafuriko ambako watu zaidi ya 40 wamekufa na madhara mengine makubwa. Hiyo kazi ya kufungua studio angemwachia makamu au kama ni lazima iwe yeye basiingeahirishwa. Kama ingekuwa ni wakati wa msiba wa Komba angeacha kwenda msibani na kwenda kufungua studio. Waliokufa Shinyanga nao ni watanzania kama Komba. Aende akasukume harakati za matibau na misaada kwa waathirika. Asije akatukumbusha ya Mwinyi wakati ule watoto wa Shauritanga walipoteketea kwa moto yeye aliendelea kutembelea kiwanda cha bia kana kwamba hakuna balaa lililotokea. Malalamiko yalipotokea ikaelezwa eti ratiba ilikuwa imepangwa. hata hivyo hoja ikawa je kama siku hiyo angekufa mwanae au mkewe angeendelea na ratiba ya kutembelea kiwanda cha bia? Hivyo hata hili la JK kwenda kuzindua studio badala ya kwenda kwenye maafa wasitwmbie habari ya ratiba. Ameishia kutuma salam za rambi rambi tu redioni. Haitoshi aende field
Umesahau Kuwa Yeye Ni Mr. Popularity Na Prestige?