Uzinduzi wa Studio mpya za Azam Media

Uzinduzi wa Studio mpya za Azam Media

Kwa studio kama iyo hao watangazaji sasa inabidi wakajifunze kwa wenzao wa citizen ya kenya wanavyojiachia kwa kutangaza na lugha sahihi . Sio hapa watangazaji hawajui hata kutofautisha R NA L yani huwa inakera sana..ukiangalia news citizen yani unasikia raha kwa kiswahili chao sahihi

mkuu citizen unaingalia kupitia kisambuzi gani? mara ya mwisho kuiona ilikuwa lini?
 
Kwa studio kama iyo hao watangazaji sasa inabidi wakajifunze kwa wenzao wa citizen ya kenya wanavyojiachia kwa kutangaza na lugha sahihi . Sio hapa watangazaji hawajui hata kutofautisha R NA L yani huwa inakera sana..ukiangalia news citizen yani unasikia raha kwa kiswahili chao sahihi


Kwa E.Africa mimi naona citizen ndo television bora kwa watangazaji mahili wa habari. Ila jana kaimu Mtendaji Mkuu wa Azam Media bwana T. Mhando alisema kua pamoja na uzinduzi wa studio mpya wametenga kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya mafuzo ya watumishi wao.
 
mkuu citizen unaingalia kupitia kisambuzi gani? mara ya mwisho kuiona ilikuwa lini?


Sasa hivi wamesitisha mwatangazo mpaka hapo watakapokua na kisimbuzi chao, waligoma baada ya mitambo ya analojia kuzimwa. Wapo katika mchakato wa kuzindua kisimbuzi chao mda si mrefu, sina uhakika kama baada ya kuja na kisimbuzi chao watapatikana tena kwenye visimbuzi vingine.
 
Lakini JK alitakiwa awe Kahama Shinyanga kwenye maafa ya mafuriko ambako watu zaidi ya 40 wamekufa na madhara mengine makubwa. Hiyo kazi ya kufungua studio angemwachia makamu au kama ni lazima iwe yeye basiingeahirishwa. Kama ingekuwa ni wakati wa msiba wa Komba angeacha kwenda msibani na kwenda kufungua studio. Waliokufa Shinyanga nao ni watanzania kama Komba. Aende akasukume harakati za matibau na misaada kwa waathirika. Asije akatukumbusha ya Mwinyi wakati ule watoto wa Shauritanga walipoteketea kwa moto yeye aliendelea kutembelea kiwanda cha bia kana kwamba hakuna balaa lililotokea. Malalamiko yalipotokea ikaelezwa eti ratiba ilikuwa imepangwa. hata hivyo hoja ikawa je kama siku hiyo angekufa mwanae au mkewe angeendelea na ratiba ya kutembelea kiwanda cha bia? Hivyo hata hili la JK kwenda kuzindua studio badala ya kwenda kwenye maafa wasitwmbie habari ya ratiba. Ameishia kutuma salam za rambi rambi tu redioni. Haitoshi aende field
 
mkuu citizen unaingalia kupitia kisambuzi gani? mara ya mwisho kuiona ilikuwa lini?

Nilidhani ni TV yangu ndo imegoma kuonesha citizen, hivi imepatwa na nini ile TV?

Hongereni sana Azam Media, Hongera Bakhresa...kitu HD sio kama wakenya na Zuku yao
 
Unazidi kujichanganya yeye kama mfanya biashara kama angekua haajiri kwa mujibu wa sifa(angalia post yako #11 ) angefiakje hapo. Huyu mtu ameanza biashara zake tokea miaka ya sabini na kipindi chote hicho amekua akiajili kulingana na mahitaji yake na ndo chachu ya mafanikio yake.

Ninachopingana nawe ni kuwa kwa kuwa ni mfanya bisahara basi anaweza kufanya chochote anachotaka si kweli. Ila naamini ni mtu anayekubali ushauri na ni makini kataika biashara yake. Na sisis wadau wake tutakapoona amekosea hatuzuiwi kuongea. kama kweli amekuwa anatumia kigezo cha dini kuajiri amekosea. Kwa sababu hata wafanyabisahsara haramu hufanikiwa piwa hiyo haiondoi haki yetu ya kukosoa.
 
Hapa tbc ccm hawatii mguu pamoja na lile gari la msaada walilopewa na China.hongera ssb
 
Nimependa studio zao zipo kisasa zaidi hongereni Azam media
 
kwa wale wapenz wa citizen habari njema ni kwamba iko hewani kuanzia jana saa moja usiku, wamesha achia matangazo yao!
 
Rais Kikwete muda huu amezindua Studio za kisasa za Azam TV,TBC na machengachenga yao na watangazaji wasiojua lugha ya taifa wakafie huko na li-CCM lao!
 
SSB businesses are turning into a conglomerate...
 
Ninachopingana nawe ni kuwa kwa kuwa ni mfanya bisahara basi anaweza kufanya chochote anachotaka si kweli. Ila naamini ni mtu anayekubali ushauri na ni makini kataika biashara yake. Na sisis wadau wake tutakapoona amekosea hatuzuiwi kuongea. kama kweli amekuwa anatumia kigezo cha dini kuajiri amekosea. Kwa sababu hata wafanyabisahsara haramu hufanikiwa piwa hiyo haiondoi haki yetu ya kukosoa.


Hili umelitoa wapi? au kuzunguka kote huko ulikua unataka kuongeela hilo? Nadhani ungejiongeza kidogo kwenye ufahamu wa wafanya biashara. Wao kipaumbele chao kikubwa ni faida hayo dini hayawahusu. Kuna watu walikua wnasema kua Bakhresa haweza kukopa mikopo yenye riba kwa sababu imani yake hairuhusu kula wala kutoa riba, na wengine wkaja na tuhuma kama zako. Wabongo tuko busy tunasema kua anaajili kwa kigezo cha dini wakati huo huo watu wanatoka kenya wanakuja kuchukua ajira kiulani. Kama huamini nenda uone idadi ya wakenya waliopo na uliza ni dini gani, sisi tuko busy na maneneo wenzetu wanatoka mbali wanakuja kuchangamkia fursa.
 
Asante mkuu nilikuwa na-miss live stream nikiwa nje ya Tanzania,hivi sasa naona naona live nini yanatokea Tanzania

Asante Bakharesa haya ndio maendeleo tunayoyataka,ITV,TBC wameshindwa kutangaza Live stream nikitu cha kushangaza sana.....

AZAM Media Flash Page
 
Aubona haulizi kuwa dr dau ameajiri wAkristo wangapi
nilidhani utauliza nssf kuna wakristo wangapi, jaribu kufatilia nssf ina waislam wangapi na wakristo wangapi.
ulishawaza kwanini tanzania woman bank kwanini waislam hawajiliwi?
 
hili studio lazima tido atafute watangazaji wa nguvu, akina Jeff Koinage, Larry King, sio hawa wenye makengeza na vithembe. Vipindi vya kiingereza atafute mzungu kama Al-Jazeera.
 
Hivi huyu Barharesa anaweza kuongea kweli
Mbona amekaa kizezeta namna hiyo Au ni mgonjwa?
 
Back
Top Bottom