Jon Moss– Sunderland
Mwamuzi, Jon Moss ni mmoja kati ya wale wenye heshima kubwa wanaochezesha Ligi Kuu England. Mwamuzi huyo ameripotiwa kuwa shabiki wa Sunderland. Alizaliwa Oktoba 18, 1970 katika mji wa Sunderland na ndio maana haishangazi kuona akiwa shabiki wa timu hiyo. Kwenye Ligi Kuu England alijiunga mwaka 2011 na moja ya mechi zake kubwa alizowahi kuchezesha ni ile fainali ya Kombe la FA mwaka 2015, wakati Arsenal walipoichapa Aston Villa 4-0.