Uwezo wa vifaa vya kijeshi vya Mmarekani kutazamwa upya?

KISIWAGA

JF-Expert Member
Oct 22, 2015
8,024
16,490
Hivi inawezekana vipi makombora dhaifu ya Muiran yaweze kupenya mifumo imara ya ulinzi wa anga ya Marekani bila kukumbana na kizuizi chochote.

Kama hili limewezekana basi siku za taifa teule hapo mashariki ya kati zitakuwa zinahesabika.

Kwa yanayoendelea huko Mashariki ya Mbali, ni wazi vita inanukia.

Wasiwasi wangu kwa Marekani anaweza kupata aibu kubwa sana baada ya hii vita kama itatoka.

Hata wao walivyoanza kwa tambo za bwana Trump na vitisho vyake ni wazi anataka kucheza vita ya maneno baada ya kutambua adui yake jinsi alivyo.

Alijaribu kutafuta uasi ndani ya Irani akakosa,
Akajaribu vikwazo akashindwa,
Vitisho akashindwa pia,
Kupenyeza inteligencia yake, lakinI mara nyingi walikamatwa hata kabla ya kuanza.
Hata zile ndege zisizo onekana mawinguni ziligundulika hara bila kutegemea.
Akaona asogeze vikosi vingi karibu na nchi ya Irani. Navyo vinaonekana na madhaifu huku Wairaq waliokaribu wakimkata juzi juzi na kuamuru aondoe jeshi lake haraka.

Saudia Arabia ndipo anapopategemea tu ambao nao wameishia kujidhalilisha tu kwa kuwapa nafasi Wamarekani katika ardhi yao.

Mmarekani alimpiga Afghanistan kwa msaada wa waasi, ilimpiga Sadam kwa msaada wa waasi. Iran wapo very strong ktk umoja wao kamwe hawakumruhusu marekan awagawe.

Hii vita naona mrusi na mchina watovyojidai kukaa mbali huku wakiyafanya yao chini kwa chini ili kumbamiza mmarekan kwa mgongo wa Iran.

Kwa Syria, marekani alifyata baada ya kuwaona Warusi na Waturuki wakitanua misuli. Akaamua kulazimisha uasi. lakini kafeli, akizidisha uasi na huku warusi wanawafyeka kwa mgongo wa Assad na mpaka sasa kashindwa kuwatumia hao ISIS, hata hao ISIS wa iraq naona ameanza kuwalinda kwa kuwaamishia makazi yao.

Marekani kamwe asidhani atatawala milele hii dunia huku akiwafanyia unyama wengine, ndo anazidi kujizalishia maadui wapya ambao soon wataja kumlambisha mchanga.

Nimeanza kwa kusema Iran siyo taifa la kubezwa Mmarekani, mwenyewe analifahamu! Hivyo hawezi kwenda akashambulia kiholela kwani anajua huyu siyo mtu wa mchezo na pia anajua Mashariki ya Kati patabana kwa Marekani.

Fikiria Syiria kumembana Iraq kumebana, Pakistan juzi ndiyo kafanya mazungumzo kulikuwa kumebana kinoma na kule ndiko chimbuko la ugaidi. Afghanstan kumebana hadi akawatoa wanajeshi wake baada yakuona wanauawa akawa anatoa misaada ya kijeshi kwa NATO na safari hii nato imesema haitaki kujihusisha na ujinga uliofanywa na marekani!

Fikiria Angel Mikhael anaenda kukutana Putin kuna mipango mingi sana Marekani hawezi kuthubutu hata hivyo kwa sasa Trump atakuwa katika vikao na washauri w anchi katika maswala ya kivita, pia kumbuka ukipiga Iran ni kuwa umewasha Israel hivyo yote haya yanaangaliwa kwa mapana.

Hivyo kwangu naona ni propaganda za kisiasa Trump akitafuta kuungwa mkono na washirika wake ili aanze chokochoko.
 
Hivi inawezaekana vipi makombora dhaifu ya muiran yaweze kupenya mifumo imara ya ulinzi wa anga ya marekani bila kukumbana na kizuizi chochote

Kama hili limewezekana basi siku za taifa teule hapo mashariki ya kati zitakuwa zinahesabika
Kama ndio hivyo mbona Iran hakuzuia zile roketi zilizomdondosha Soremayne? Jibu waliviziana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani mashambulizi hayo yamefanyika kwenye base za jeshi la US ndani ya ardhi ya Marekani au kwenye base za jeshi la US ndani ya ardhi ya Iraq?

Nijuavyo mimi anga la Marekani liko protected zaidi ukilinganisha na anga la Iraq. Hao Iran wako kama ni wakali waambie washambulie ardhi ya Marekani yenyewe waone kama wataweza.
 
HAKUNA KOMBORA LA IRAN LIMETUA MAREKANI..UKIACHILIA MBALI JAPAN WALIPOVAMIA HAWAII (WWII)
HAKUNA KOMBORA LA NCHI NYINGENE LIMETUA MAREKANI! ILA YANATUA KWENYE VITUO VYAO HUKO IRAQ,AFGHANISTAN NK...
Hivi unafikiri maadui zake hawajui kua ameliwekea ulinzi anga lake!
anajua ndo mana walishaumiza akili kutengeneza makombora ya kuzama huko.Kiduku alimambia huyo Mmarekani ana kombora akilituma linatua hapo New york.Pia tambua kuna kitu inaitwa nyuklia.Hii hakuna wakuizuia na ndo man anatapatapa watu wasitengeneze silaha za nyuklia huku ye akiwa nazo.Uzuri hao watubado wakaendelea kutengeneza bila kumuhofu chochote maana wanamjua anavyopenda uonevu.

By the way huyo USA hakuna vita kawai imaliza zaid ya kuacha vikundi vya anavyoita vya kigaidi vikiendelea kumuulia raia wake kila kona.Usalama wa raia wa USA dunia nzim umekua mdogo sana na ndo mana hawataki vita wakijua fika vita haiishagi kamwe.


Ukinipiga basi kizazi changu kitalipiza.Kwa mtindo huu usalama wa Mmarekawa utaendelea kua mashakani popote alipo.
 
Kwa yanayoendelea huko Mashariki ya Mbali, ni wazi vita inanukia.

Wasiwasi wangu kwa Marekani anaweza kupata aibu kubwa sana baada ya hii vita kama itatoka.

Hata wao walivyoanza kwa tambo za bwana Trump na vitisho vyake ni wazi anataka kucheza vita ya maneno baada ya kutambua adui yake jinsi alivyo.

Alijaribu kutafuta uasi ndani ya Irani akakosa,
Akajaribu vikwazo akashindwa,
Vitisho akashindwa pia,
Kupenyeza inteligencia yake, lakinI mara nyingi walikamatwa hata kabla ya kuanza.
Hata zile ndege zisizo onekana mawinguni ziligundulika hara bila kutegemea.
Akaona asogeze vikosi vingi karibu na nchi ya Irani. Navyo vinaonekana na madhaifu huku Wairaq waliokaribu wakimkata juzi juzi na kuamuru aondoe jeshi lake haraka.

Saudia Arabia ndipo anapopategemea tu ambao nao wameishia kujidhalilisha tu kwa kuwapa nafasi Wamarekani katika ardhi yao.

Mmarekani alimpiga Afghanistan kwa msaada wa waasi, ilimpiga Sadam kwa msaada wa waasi. Iran wapo very strong ktk umoja wao kamwe hawakumruhusu marekan awagawe.

Hii vita naona mrusi na mchina watovyojidai kukaa mbali huku wakiyafanya yao chini kwa chini ili kumbamiza mmarekan kwa mgongo wa Iran.

Kwa Syria, marekani alifyata baada ya kuwaona Warusi na Waturuki wakitanua misuli. Akaamua kulazimisha uasi. lakini kafeli, akizidisha uasi na huku warusi wanawafyeka kwa mgongo wa Assad na mpaka sasa kashindwa kuwatumia hao ISIS, hata hao ISIS wa iraq naona ameanza kuwalinda kwa kuwaamishia makazi yao.

Marekani kamwe asidhani atatawala milele hii dunia huku akiwafanyia unyama wengine, ndo anazidi kujizalishia maadui wapya ambao soon wataja kumlambisha mchanga.
 
Kwani mashambulizi hayo yamefanyika kwenye base za jeshi la US ndani ya ardhi ya Marekani au kwenye base za jeshi la US ndani ya ardhi ya Iraq?

Nijuavyo mimi anga la Marekani liko protected zaidi ukilinganisha na anga la Iraq. Hao Iran wako kama ni wakali waambie washambulie ardhi ya Marekani yenyewe waone kama wataweza.
Wewe unaongea nini mbona base za Urusi nchini Syria zilikuwa zinazuia makombora yanayorushwa kwake. Yaani unataka kusema anga la Marekani tu ndo limelindwa, kwani ni mifumo ipi tofauti na THAAD na mingine ileile iliyopo kwenye base za ndani ya U.S na nje ya nchi. Na ndo mifumo hiyo iliyoshindwa kuzuia makombora yaliyorushwa kwenye miundombinu ya mafuta kule Saudi Arabia.
 
HAKUNA KOMBORA LA IRAN LIMETUA MAREKANI..UKIACHILIA MBALI JAPAN WALIPOVAMIA HAWAII (WWII)
HAKUNA KOMBORA LA NCHI NYINGENE LIMETUA MAREKANI! ILA YANATUA KWENYE VITUO VYAO HUKO IRAQ,AFGHANISTAN NK...
Kambi zote kubwa za marekani wameweka mifumo ya kujilinda kumbuka wanawanajeshi 60,000 mashariki ya Kati Iraq wapo 6,000 .ambayo inatia shaka uwezo.kumbuka Saudi Arabia wanatumia mifumo ya kisasa ya USA lakini ilishindwa kuzuia shanbulio kwenye kiwanda kikumbwa kabisa duniani Cha kusafisha mafuta la wa houthi wa yemeni ambao washirika wa irani.drone za kienyeji zilipenya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom