Uwekezaji wa UTT liquid Fund faida yake mbona ni tofauti na uhalisia wanaousema

Gotze Giyani

Senior Member
Feb 28, 2022
121
180
Habari wadau poleni na majukumu ya taifa lisiloeleweka kama sio lenye jana janja nyingi na yote ni kutokana na watanzania wengi kutokujali.

Tuachane na hayo niliwai kusoma uzi mmoja huku jamii forums nikavutiwa nao nikajitaidi kufuatilia na kuuelewa zaidi basi nikaamua kuwekeza UTT amis mfuko wa Liquid fund ni miezi kama 9 hivi na wanasema kwa mwezi ni asilimia mpaka 1 ila mbona ni tofauti mfano unaweza kuwa na milioni 5 kwa mwezi faidi hapo ilitakiwa iwe 50000 kuendelea ila unaweza ishia 45000 hivi wana calculate vipi wakati thamani ya kipande aijashuka.

Kama ujui kaa kimya sitaki matusi na ujuaji wa kijinga wadau mnaojua kuhusu huu mfuko na wakaribisha mnieleweshe maana naona kama ni uwekezaji kichaa hata kama ela ni nyingi faida ni ndogo.
 
Wapigie
Chagua mkoa uliopo kama mkoa wako aupo piga makao makuu DAR.
Screenshot_20220923-231958_OneDrive.jpg
 
Habari wadau poleni na majukumu ya taifa lisiloeleweka kama sio lenye jana janja nyingi na yote ni kutokana na watanzania wengi kutokujal...
Hiyo asilimia moja huwa wanaipata kwa kujumuisha faida iliyopatikana kwa kipindi cha mwaka mzima gawanya kwa 12. Kwa hiyo ukifuatilia kila mwezi utaona kuna upishano. Mfano mwezi wa nane faida ilikua 0.9731% na mwezi Septemba mpaka tarehe 29/09/2022 faida ni 1.1636%
 
Hiyo 1% ni kwa mwaka mzima. Km una iyo 5mln utapata 5mln×1%=500k kwa mwaka mzima, ina maana kwa wastani kwa kila mwezi utapata 500k÷12=41,666.666666667 sawa na 1,388.8888888889 kwa kila siku. inasaidia kutunza thamani ya pesa yako tofauti km ungeweka iyo pesa benki.
 
Hiyo 1% ni kwa mwaka mzima. Km una iyo 5mln utapata 5mln×1%=500k kwa mwaka mzima, ina maana kwa wastani kwa kila mwezi utapata 500k÷12=41,666.666666667 sawa na 1,388.8888888889 kwa kila siku. inasaidia kutunza thamani ya pesa yako tofauti km ungeweka iyo pesa benki.
Benki ina interest kubwa, ukiweka savings. Pia jaribu benki ya posta. hao matapeli tu.
 
Hiyo asilimia moja huwa wanaipata kwa kujumuisha faida iliyopatikana kwa kipindi cha mwaka mzima gawanya kwa 12. Kwa hiyo ukifuatilia kila mwezi utaona kuna upishano. Mfano mwezi wa nane faida ilikua 0.9731% na mwezi Septemba mpaka tarehe 29/09/2022 faida ni 1.1636%
Hizo faida au hasara zinatokana na nini??

#MaendeleoHayanaChama
 
Hiyo 1% ni kwa mwaka mzima. Km una iyo 5mln utapata 5mln×1%=500k kwa mwaka mzima, ina maana kwa wastani kwa kila mwezi utapata 500k÷12=41,666.666666667 sawa na 1,388.8888888889 kwa kila siku. inasaidia kutunza thamani ya pesa yako tofauti km ungeweka iyo pesa benki.
5m x 1% = 500k? ??? Hesabu za wapi hizi?
 
Back
Top Bottom