Tusilete siasa kwenye mambo ya msingi.
Mengi hapa ameingiaje?
Yani nyie ndio miaka yote mnatudanganya kua Makampuni ya IPP yanaongoza kwa kukwepa kodi kumbe mlikua mnayapigavita kwa jinsi yanavyofichua uovu wenu na marafiki zenu.
Yule mama ametamka mwenyewe live kuwa Amepokea msg kutoka kwa Prof.Muhongo.
Wewe unafikiri yule mama kwa madaraka na nafasi aliyo nayo hana namba za simu za Prof. Muhongo?
Na kwa nini huoni kuwa Muhongo anajua jambo hilo wakati Mafuta yanayopita pale yako chini ya wizara yake!?
Tangu lini Mengi akaingia kwenye baraza la mawaziri na kujua kuwa waziri mkuu amekwazwa na kufungwa kwa miaka mitano kwa flow meter kule bandarini na kupanga ziara ya kushtukiza ili abaini yanayotokea?
Mengi aliijuaje hiyo ziara ya kustukiza ili aweze kumhujumu Prof.Muhongo?
Wewe huoni na iko dhahiri kuwa landa Prof alikua anataka kumsaidia Mwizarubi ili asishtukizwe na Waziri mkuu na hali ikawa ni mbaya zaidi?
Na pia kwa nini tusiomlaumu Prof. Kwa kutoa siri za utendaji wa serikali?
Kama ni kweli hiyo msg imetoka kwa Prof.Muhongo, atakua na tofauti gani na askari polisi anayetoa siri za utendaji kwa wahalifu ili wasikamatwe?
Na ndugu yangu usije ukamwamini mwanasiasa yoyote kuwa yeye ni mwema kwa sababu ya Elimu yake.
Ikiwa ni hivyo basi wasomi wote wataenda peponi.
Binadamu wote wanahulka ya ubinafsi na hawaridhiki na walicho nacho hata akisoma vipi na ndio maana hata Prof. Muhongo hakuridhika na elimu aliyokuwa nayo mpaka akaamua kusoma mpaka kuwa profesa. Muhongo ni binadamu kama binamu wengine. Huwezi kusema kila analofanya jema ndio la kwake lakini baya anasingiziwa!!! Humtendei haki Mengi kwani hata yeye anayo mema na mabaya yake !
Hata hivyo unapotumikia umma ni lazima ufanye kazi kwa kufuata sheria na unapofanya fyongo basi unapaswa kuwekwa pembeni.
Hapa ndio tutakapo mkumbuka Mh. sana Bernad Membe kwa kuweka wazi kuwa ni rahisi kwa rais kumwajibisha mtu ambaye hakumchagua lakini pia ni vigumu sana kumwajibisha mtu ambaye umemchagua na kumpa madeaka.