William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
FMES,
Nikuombe jaribu kuficha hasira zako kwa Lowassa. Haki na Uhuru wa mimi kumuunga mkono LOWASSA akitangaza NIA, na KUTEULIWA na chama changu ni haki yangu ya Kikatiba kama ilivyokuwa haki yako mwaka 2005 kumuunga mkono Mzee Malecela.
Nikuombe uheshimu haki yangu ya kutoa maoni yangu kama wewe ulivyotoa maoni yako ukitaka wagombea wajitokeze..
Leo mimi nimejitokeza openly na kusema ninachokiamini sijaongelea suala la whether Lowassa ana tuhuma ama hapana, tukianza kufukua tuhuma hata mzee wako ana tuhuma za kupokea fedha za EPA kupitia Jeetu Patel lakini hakuna aliekutuhumu kwa wewe kumuunga Mkono 2005 na pale Morogoro zilipoporwa na wezi wakati mama Anne Malecela akizileta kugawia wapiga kura.
Leo hapa nimesema ninachokiamin, come out sema kama Lowassa hana sifa niliyotaja then utakuwa na hoja ukinipa sababu za yeye kutokuwa na uwezo wa kuchapa kazi na ukajenga hoja nitakuelewa,
Tusipige porojo eti Lowassa alimfata Rais na kubembeleza, go and ask Mr. Malecela and he will give u the facts ambazo wengi hawapendi kusikia. Kama Lowassa anahusika na Richmond apelekwe mahakamani, hakuna anayemtetea na wala hilo halina mjadala; mahakama itaamua, kama Lowassa ni mwizi basi ni udhaifu wa mamlaka kutowakamata wezi na kuwapeleka mahakamani. Kama una ushahidi peleka katika authority uje hapa utueleze umepeleka ushahidi wa wizi wa Lowassa na hata mimi nitakuona hero! Tujadili facts mkuu, tusiingilie uhuru wa mtu kuchagua. Nimesema wazi kama chama kitamteua nitampigia kura na nimetoa sababu yangu, na si Lowassa pekee, same applies kwa CDM, wakisimamisha mgombea hawezi kuwa mkamilifu wa kila kitu lakini kila mmoja atahakikisha anampigia kura.
FMES na Wana JF,
Tusipoteze muda mwingi kujadili LOWASSA, huyu kama ana madhambi yake mamlaka husika zitachukua hatua zinazostahili. Nchi yetu ina bahati mbaya tumekumbwa na ugonjwa wa unaoitwa ‘LOWASSA', tujadili issues za maendeleo.
Nikutoe shaka juu ya jambo moja: Ssina historia ya kuficha wala kutafuna maneno katika jambo ninaloliamini, kama wewe ulifanya kazi ya kutafuta ushahidi juu ya mkataba mbovu wa Richmond, nikupe hongera ulitekeleza wajibu wako kama RAIA mwema. Kama utaongelea UADILIFU, wewe mwenyewe ni zao la UKOSEFU wa UADILIFU wa Viongozi wetu. Suala la RICHMOND ni udhaifu wa mfumo wetu, jambo ambalo mpaka leo linatugharimu kama Taifa. Tumelalamika, tumetuhumu, tumekosoa lakini hatujajadili ufumbuzi wa tatizo lililoleta RICHMOND. Leo ni mwaka wa sita bado tatizo lipo lakini bado tunajadili RICHMOND na LOWASSA.
FMES, don't fool people here, tunafahamu why unakuwa na hasira when it comes to LOWASSA. Ni tatizo la familia yenu na ni makovu ya 2005. Nimalize kwa kusema LOWASSA akiteuliwa na kupitishwa na chama nitamuunga mkono asipoteuliwa na asipopitishwa na chama pia nitaheshimu na kufanya maamuzi kutokana na wakati na mazingira ya wakati huo, hiyo ni imani yangu. Mimi nimesema msimamo wangu na kwa jina langu, wewe come out and sema msimamo wako. Kila mmoja wetu atakuwa na maamuzi yake tuyaheshimu, akini kwa sasa tujadili masuala ya NCHI yetu na tutimize wajibu wetu. Wewe binafsi huna moral authority kuongelea uadilifu bcs your background inaonyesha, lakini hatukuangalii kwa Background yako tunakuangalia wewe na unachosema kwa sasa.
Hussein
Mheshimiwa Bashe: ninaomba sana nisaidie kujibu huu ujumbe wako kwa sababu no question unaelekezwa kwangu zaidi kuliko uliyetaka kumtumia, na ninaomba sana nikuaminishe kwamba mimi ninasimamia taifa kwanza na sio majungu na hadithi hadithi za mitaani.
1. Sikufahamu sana, lakini kwa maneno uliyoanza nayo umenipa wasi wasi sana na uwezo wako wa uongozi wa juu na hata kufikia kuwa ndiye mkusanyaji wa mawazo ya wananchi on UV-CCM: Hela za EPA zilikuwa ni hela za Mtandao ambao Malecela alikuwa ni their number one enemy, nitakuamini kwamba unasema ukweli iwapo utaonyesha karatasi yoyote ile iliyosainiwa na Malecela kuchukua hela kutoka BOT on the behalf of CCM.
- Unaropoka ropoka kuhusu Mama Kilango na kuvamiwa na majambazi pale Mvomero, hapa ndipo nimekutoa heshima kabisaa kwamba huna maana kabisaa kwa hili taifa, Mama kilango alikuwa akitokea kwangu hapa New York kuchukua malighafi zake za biashara zake, kwenye maduka yake ya Dar na Dodoma, ni kawaida yake kila anapofika huko kugawanya bidha zake kati ya dula lake la Dar na zingine husafiri nazo kwende kwenye duka lake la Dodoma, kwenye lile alikuwa amebeba masanduku ya nguo za biashara na kwenye pochi yake alikuwa na Shillingi laki mbili tu, na hata kwenye kesi mahakamani wale majambazi walikiri kwamba ndizo hela walizozikuta kwenye pochi waliyokimbia nayo, masanduku yalikuwa ni mazito sana yaliwashinda kabisa kukimbia nayo wakayaacha pale pale, sasa unasema Shiilingi laki mbili ndio zinaweza kununua urais wa Tanzania mwaka 2005!
- Halafu kwa taarifa yako kesho yake hawa majambazi walimvamia Makongoro Nyerere na kumpora kila kitu vipi na yeye alikuwa anagawa hela za rushwa wa Urais?
- Una maana Mvomero ndio wanaamua Rais wa Tanzania awe nani kwamba Mama kilango na Makongoro walikwenda kugawa hela pale? ha! ha! ha!
2. Malecela facts na Lowassa ni kwamba wabunge wanne walipokwenda Chamwino kumuona Rais kuhusu kumuokoa Lowassa na Uwaziri Mkuu, Makamba, Ameir, na Kingunge walimtetea Lowassa ni Malecela peke yake aliyegoma kwamba ni lazima aondoke, yes hilo aliniambia, asingeweza kuniambia uongo ambao haukufanyika! Mimi simchukii Lowasaa as a person lakini nina tatizo sana na kazi zake akiwa Waziri mkuu, hasa ninapoona taifa letu linalipa mabillioni ya pesa kwa Umeme ambao haupo nina haki zote za kukemea aliyetufikisha hapo kama ulivyoona kwenye ile topic niliyoianzisha jana ya kujivua.
- Unasema wewe matatizo ya Richmond hayakuhusu maana ni mapungufu ya mamlaka zetu kwa kutokumchukulia hatua and you want to be a leader wa hili taifa?
well, nilitaka kugusa haya tu mkuu sana, ninaamini Mkulu FMES naye atakujibu kama ulivyomu-address kwenye ujumbe wako, karibu sana mkuu, nothing personal ila NI TAIFA KWANZA!
William @ NYC, USA.