Uwepo au kutokuwepo kwa kitu ni jambo moja na maelezo yenye contradiction ni jambo lengine,kutokuwepo kwa kitu si kwamba ndio sababu ya kuwepo maelezo yenye contradiction kiasi cha tutumie hizo contradictions kama jibu la kuwa hicho kitu hakipo. Kwahiyo kama wewe unajua hakuna Mungu basi ueleze ni vp hakuyupo na kuleta hoja ya contradiction kwa sababu yawezekana kuna hujaelewa vizuri.
Unaelewa kwamba swali nililokuuliza hujajibu na kama unajibu kitu sijakuuliza.
Narudia.
1. Inawezekana kitu kikawepo, kikawa cha kweli, ila maelezo yake yakawa na contradiction, kwa sababu hatujaelewa tu kilivyo kweli.
2. Inawezekana kitu kikawa hakipo, habari z akuwapo kwake zikawa uongo, maelezo ya kuwapo kwake yakawa na contradiction kutokana na kwamba habari ni za uongo.
Hapo tumeona kitu cha kweli kinaweza kuwa na maelezo ya contradiction, na kitu cha uongo kinaweza kuwa na maelezo ya contradiction.
Mpaka hapo nimesha accommodate main point yako kwamba, si lazima maelezo yenye contradiction yaoneshe kitu ni uongo/ hakipo.
Kwa hivyo tusibishane kuhusu point hii, kwa sababu hakuna cha kubishania, wote tushaikubali, huna haja ya kuitaja tena.
Uitaje tena kwa nini wakati wote tushakubaliana?
Sasa, baada ya kukubaliana hivyo, tuendeleze mjadala.
Ukiona sehemu jambo lina maelezo yenye contradiction, utajuaje contradiction hiyo inatokana na jambo kuwa la uongo/ halipo au jambo lipo, ni la ukweli, contradiction inaonekana kuwapo kwa kuwa hatujaelewa kitu tu?
Hujajibu swali hili.
Unarudia mambo ambayo hatujabishana.
Badala ya kujibu tulipohitilafiana ili tupatengeneze, kwenye mjadala, unajibu pasipo na mjadala!