Utumwa mpya ndani ya Kanisa

Am christian, i believe in Jesus and i believe in his miracles na nina amini wako wachungaji na maaskofu ambao kweli wana mcha Mungu na wanapokuombea kweli unapata uponyaji au kufungulia, ila tatizo unaloliona sasahivi kwanza si la kushangaza mana hata kwenye biblia takatifu ilishaandika kwamba nyakati za mwisho manabii wengi wa uongo watakuja na wataangamiza watu wengi sana, na pili the problem isn't them (hao manabii) bali waumini, watu hawamtafuti Mungu bali wanatafuta VITU, wamemgeuza Mungu kama mnganga wa kienyeji mtu anataka aendelee na maisha yake ya dhambi kama kawaida at the same time anatafuta baraka kutoka kwa Mungu ndo hao wanakimbilia kwa hao manabii wanaohubiri magari na nyumba na kuwa milionea sijui laana za ukoo yani wanaishia kudanganywa zaidi na kufanywa mazezeta zaidi. Na ndo mana unakuta mtu anakwambia ameokoka ila matendo yake utabaki mdomo wazi, mtu anakwambia ameokoka alivyovaa tena kanisani achia mbali mtaani hutaamini, ukimwambia anakwambia usimletee ulokole wa kizamani, na wachungaji wao wako kimya tu, sasa huwa najiuliza biblia ya zamani ni ipi na ya sasa ni ipi wanayotumia wao, watu wanazini humo makanisani kama hawana akili nzuri yani hata ile hofu ya Mungu ndani yao hakuna lakini ndo hao hao wanakwambia tumeokoka, hizo nyimbo za sikuhizi sasa ndo uuuuwi sometime unazima hadi radio hizo video ndo kabisaaaaa utachefukwa kiukweli kwenye gospel ni heri usikilize tu audio video nyingi zinakera alafu unaambiwa waimbaji wameokoka. Mungu atusaidie
 
Ndio maana mimi niliamua kuacha kwenda kanisani kwa ajili ya mambo kama. Haya niliona sisi washirika ndo mitaji ya wachungaji mitume na manabii.. Kanisa ni mimi mwenyewe hekalu ni roho yangu na. Mwili wangu baaada ya Yesu kunifia msalabani aliondoa kiambaza au ukuta uliokuwepo umezuia Mawasiliano yangu na Mungu ila now najiachia mimi mwenyewe kwa Mungu wangu alieniumba moja kwa moja na ananisikia vizuri sio kuibiwa na kutapeliwa na hawa wahuni wajanja wanajiitwa watumishi wa Mungu.
 
Aahaa kumbe. Bahati nzuri nimejitahidi sana kutoingia ndani zaidi kidini. Hakuna kitu sipendi kama kuingia kwenye ufollower wa manabii na mitume wanaoibuka kila kukicha
Yaani umpatie sadaka iliyonona na inayouuma (yaani kubwa karibu kuzidi uwezo wako), zaka, mavuno, malimbuko, matendo ya huruma kwa maana ya kuweka 'hazina mbinguni'. Kwa nini yeye aitumie hapa duniani badala ya mbinguni pia?
 
"Mtu huna kazi, huna biashara wala wazo la biashara, huna ujuzi, huna elimu, lakini kila siku unashinda kanisani kumsikiliza Mchungaji anayesema kesho utakua milionea na wewe unasema "Baba napokea/Dady I receive". Huu ni utani"

Mkuu huo si utani, ni upuuzi kiwango cha lami ya ya mambele na siyo bongo.
 
Ndefu mno
Hapana, tujifunze kusoma neno kwa neno hapo ndipo tutakwenda sawa. Tujitahidi maana kutosoma neno kwa neno unaweza kuza mara paaap umeteuliwa nenda kawakilishe kusini mkataba wa kununua bombadia. Between the line wanasema faida ya miaka 20 itakuwa ya wenye kampuni. Mara paaap tumekuja kufuata faida yetu ya miaka 20, sasa hapo sijui utakuwa umetusidia au umeshatuingiza cha kike. Kisa mkataba unamakaratasi ya VOLUME kubwa
 
NB: Makala hii inazungumzia baadhi ya makanisa ya kilokole sio yote.Dont generalize.Yapo makanisa ya kilokole yenye misingi bora, lakini mengine yamejaa upotoshaji. Haya ndio yaliyozungumzwa hapa.Nakuunga mkono kwenye umaliaziaji NA umesahau kuwa pia yapo makanisa ya kikatoliki na kiluteri siku hizi ambayo nayo kuna kupanda mbegu....
 
Mtu huna kazi, huna biashara wala wazo la biashara, huna ujuzi, huna elimu, lakini kila siku unashinda kanisani kumsikiliza Mchungaji anayesema kesho utakua milionea na wewe unasema "Baba napokea/Dady I receive".
 
Back
Top Bottom