Utitiri wa viongozi serikali una tija gani kwa Taifa?

Darren2019

JF-Expert Member
Nov 23, 2019
1,112
2,379
Nimejaribu kufikiri ni kwanini asilimia kubwa ya fedha za serikali znaishia kwenye matumizi ya kawaida, mojawapo ya sababu niliyoona ni uwepo wa utitiri wa viongozi wengi kwenye ngazi za juu hasa kuanzia wilayani na ukizingatia hawa wanahudumiwa siyo tu mishahara mikubwa bali kuna magari/mafuta, nyumba/malazi, posho za hapa na pale plus ubadhirifu huko maofisini n.k

Ukiangalia wilayani kuna wakuu wa wilaya, wakurugenzi, makatibu tawala, wenyeviti wa halmashauri n.k

Mkoani, kuna wakuu wa mikoa, wakurugenzi wa majiji sijui, makatibu tawala, mameya n.k
Ukiangalia majukumu ya hao viongozi yanafanana fanana sana.

Bungeni ndio vile mipesa mingi isiyoendana na ufanisi wa kazi, mbunge mmoja alipwe 12M kwa mwezi, apewe mkopo wa gari 90M, apewe mafuta lita 1000 kila mwezi, apewe pensheni 250M ndani ya miaka mitano, hapo bado wana kamati mbalimbali huko bungeni, uje uweke wakurugenzi wa mashirika na taasisi mbalimbali za serikali, wenyeviti wa bodi na tume mbalimbali.
Wizarani mawaziri na manaibu wao, makatibu wakuu n.k, hivi kuna haja gani ya kuwa na waziri, naibu waziri na katibu mkuu? Na wizara nyingne zina hadi naibu katibu mkuu kwanini tusiwe na mawazIri wataalam ambao pia watakuwa watendaji?

Kwa utitiri huu wa viongozi kwa nchi maskini km Tanzania tutegemee 90% ya bajeti kuishia kwenye matumizi ya kawaida ya kuendesha serikali. JPM aliwahi kuahidi kupunguza ukubwa wa serikali ila alipofika ikulu kumbukumbu zake zikawa zimeliwa na mchwa, ndo kwanza akaanzisha na wizara mpya ambayo hata waziri muhusika hajui majukumu yake...
Enewei...
Tuliambiwa tukilaumu tutoe na pendekezo, kwangu mimi nafikiri hapa ni Katiba mpya tu, labda itasaidia .
 
Miaka kumi ijayo roboti moja litakuwa likihudumia mkoa mzima, miwili hata zaidi, hivyo wacha wale za mwisho mwisho. Teknologia itawaumbua!
 
Bado tuna muda tujitaidi kupata Katiba.
IMG_20210620_101928.jpg


Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
 
Ndiyo maana JPM aliamua kuongoza nchi yeye tu na PM wake kwa miezi mitatu, na maendeleo makubwa sana yakaonekana tena ndani ya muda mfupi. Anyways, lakini ajira hampendi tena nyie mapomonda wa bara!???
 
Nafikiri huu ni mfumo ambao tumeurithi kutoka kwa wakoloni sasa kwa kuwa uwezo wetu wa kufikiria ni mdogo ndio maana tunaendelea na hiyo mifumo hadi leo

Inatakuwa kuwe ni kitengo cha kufanya review na kutoa mapendekezo ya structure ya utawala wa serikali iweje hichi kitengo kinaweza kikawa chini ya bunge au chuo kikuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiangalia huko maofisini hakuna wanachofanya, juzi halmashauri wamepewa kazi ndogo tu ya kuingiza watumishi wanaopandishwa vyeo kwenye mfumo wamepata tabu hadi wakaongezwa muda na vitisho vya kutosha.
 
Nimejaribu kufikiri ni kwanini asilimia kubwa ya fedha za serikali znaishia kwenye matumizi ya kawaida, mojawapo ya sababu niliyoona ni uwepo wa utitiri wa viongozi wengi kwenye ngazi za juu hasa kuanzia wilayani na ukizingatia hawa wanahudumiwa siyo tu mishahara mikubwa bali kuna magari/mafuta, nyumba/malazi, posho za hapa na pale plus ubadhirifu huko maofisini n.k

Ukiangalia wilayani kuna wakuu wa wilaya, wakurugenzi, makatibu tawala, wenyeviti wa halmashauri n.k

Mkoani, kuna wakuu wa mikoa, wakurugenzi wa majiji sijui, makatibu tawala, mameya n.k
Ukiangalia majukumu ya hao viongozi yanafanana fanana sana.

Bungeni ndio vile mipesa mingi isiyoendana na ufanisi wa kazi, mbunge mmoja alipwe 12M kwa mwezi, apewe mkopo wa gari 90M, apewe mafuta lita 1000 kila mwezi, apewe pensheni 250M ndani ya miaka mitano, hapo bado wana kamati mbalimbali huko bungeni, uje uweke wakurugenzi wa mashirika na taasisi mbalimbali za serikali, wenyeviti wa bodi na tume mbalimbali.
Wizarani mawaziri na manaibu wao, makatibu wakuu n.k, hivi kuna haja gani ya kuwa na waziri, naibu waziri na katibu mkuu? Na wizara nyingne zina hadi naibu katibu mkuu kwanini tusiwe na mawazIri wataalam ambao pia watakuwa watendaji?

Kwa utitiri huu wa viongozi kwa nchi maskini km Tanzania tutegemee 90% ya bajeti kuishia kwenye matumizi ya kawaida ya kuendesha serikali. JPM aliwahi kuahidi kupunguza ukubwa wa serikali ila alipofika ikulu kumbukumbu zake zikawa zimeliwa na mchwa, ndo kwanza akaanzisha na wizara mpya ambayo hata waziri muhusika hajui majukumu yake...
Enewei...
Tuliambiwa tukilaumu tutoe na pendekezo, kwangu mimi nafikiri hapa ni Katiba mpya tu, labda itasaidia .

Huu ujinga unatakiwa ukomeshwe haraka iwezekanavyo kupitia Katiba Mpya ya Wananchi.

Cheo kama cha Mkuu wa Mkoa na Wilaya, RAS na DAS, Afisa Tarafa, nk kinainufaisha CCM zaidi kuliko Taifa! Mbaya zaidi kila mwezi mabilioni ya pesa za walipa kodi wa nchi hii hutumika kuwalipa hawa makada wa ccm!

Halafu bado tunaongezewa TOZO kwenye simu!
 
Ndiyo maana JPM aliamua kuongoza nchi yeye tu na PM wake kwa miezi mitatu, na maendeleo makubwa sana yakaonekana tena ndani ya muda mfupi. Anyways, lakini ajira hampendi tena nyie mapomonda wa bara!???
Wewe Mataga hutakiwi hata kukosoa chochote! Nyinyi ndiyo wale wale wafuasi wa chama cha kishetani kama ccm.

Tofauti yako na Mataga wengine ni moja tu, wewe unakufa njaa huko kwenu Mchamba wima! huku wenzako wakipata ulaji.
 
Huu ujinga unatakiwa ukomeshwe haraka iwezekanavyo kupitia Katiba Mpya ya Wananchi.

Cheo kama cha Mkuu wa Mkoa na Wilaya, RAS na DAS, Afisa Tarafa, nk kinainufaisha CCM zaidi kuliko Taifa! Mbaya zaidi kila mwezi mabilioni ya pesa za walipa kodi wa nchi hii hutumika kuwalipa hawa makada wa ccm!

Halafu bado tunaongezewa TOZO kwenye simu!
Ni hatari mkuu, sijui huyo Nyerere aliruhusu vipi haya km alikuwa mwadilifu kweli km tunavyomsoma na kuhubiriwa.
 
Back
Top Bottom