Uteuzi wa Makamba kama Waziri wa Nishati na aliyofanya alipoteuliwa umenifanya niwakataze watoto wangu kuchukua masomo ya Sayansi

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Kuna mengi yalisemwa kuhusu January kuteuliwa kuwa waziri wa nishati, mojawapo likiwa ni kwamba kulikuwa na msukumo fulani kutoka kwa wazee kwa mama kumpa January wizara hiyo nyeti kama chaguo lake.

Sasa kwangu mimi hilo nililiona lina walakini sana. Sina tatizo na Makamba kuwa waziri, lakini kwa nini wizara ya Nishati ambayo ni nyeti sana? Kwa nini tusiwe na waziri katika wizara hii ambae ana ufahamu angalau na mambo ya sera na utawala katika mambo ya nishati? Hakuna Mtanzania ambae angefaa zaidi sana ya Makamba?

Nikasema ngoja nimpe kinachoitwa the benefit of doubt, kwamba mtu ambae hana kabisa background ya energy policy na management atuongozee hii wizara. Kama nilistaajabishwa na uteuzi wake, nilipata na mshituko na yale aliyofanya mara tu baada ya kuteuliwa. Alibadilisha watendaji nyeti wote wa juu katika wizara hii!

Nikauliza ndugu zangu walio karibu na jikoni - kulikoni? Wengi wakasema hataki kufanya kazi na wateule wa Magufuli. Nikauliza hawataki wale wasio na sifa ambao labda Magufuli aliwateua kwa ukabila na urafiki? Nikaambiwa hapana, wote tu.

Sikuamini. Nikamchukulia Dr. Tito Mwinuka ambae alikuwa Mkurugenzi wa Tanesco, ambae nae January alitaka aondoke. Nikaangalia background yake na kuona Mwinuka ni mtu alikuwa kipanga sana kimasomo. Alisoma PCM, akasomea uhandisi pale UDSM na kufaulu vizuri sana hadi kubakizwa kama lecturer. Akaendelea kupanda hadi kuteuliwa kuwa Mkurugenizi wa Tanesco.

Nilishituka hata zaidi kusikia nani atam-replace Dr. Mwinuka - mtu aliesimamia kampuni ya television channel! Nikajiuliza, hivi tuna tatizo gani? Kweli tunafikiri mtu akifanikiwa kusambaza DSTV nchini atafanikiwa kuongoza Tanesco zaidi sana ya mtu kama Dr. Mwinuka? Siamini. Ngoja muda uni prove wrong.

Sasa nilipofikiria kwamba upande wa pili tuna January, ambae alisomea masomo ya kiingereza na historia sijui, na akaja kuwa mwandishi wa hotuba za Kikwete, na kutokana na ukaribu wake na Kikwete na kuwa mtoto wa Makamba akawa waziri. Leo hii huyu ndio anasema simtaki Mwinuka, aondolewe pale Tanesco. Yaani vijana wa UDSM watakuambia nguini ana dictate injinia aondolewe katika kazi ya uinjinia kwa sababu nyepesi sana!

NIkasikitika sana. Ndipo nikakumbuka ule mtazamo kwamba watu wa masomo ya sayansi wanafanya kazi kubwa sana katika maisha yao ya shule, lakini katika maisha wanakuja kuamuliwa mambo na hao waliowaita manguini au hata wale vilaza wa darasani walioamua kuingia kwenye siasa kwa kuwa hawakua na kitu kingine cha kufanya!

Hebu niambieni labda sioni. Tumepata mafanikio yepi katika utendaji wa wizara ya nishati tangu uteuzi hu wa Samia? Mambo yanazidi kuharibika kila siku katika kipindi hiki kigumu ambacho tunahitaji sana wizara hii iongozwe na mtu mwenye utaalamu wa juu wa sera na utawala katika masuaala ya nishati. Sio mzoefu wa kuandika hotuba. Mama usisubiri mambo yaharibike kabisa.

Nadhani dunia inahitaji mapinduzi ya wasomi wa science na teknolojia na kuondokana na kuamuliwa mambo ya kiufundi na watu ambao hawastahili kufanya maamui katika nyanja hizo!

Nikawaambia wanangu, epukeni kozi ngumu za sayansi. Someni historia na kiingereza mje kuwa waandishi wa hotuba za maraisi na mawaziri hata wa nishati au sayansi na teknolojia!
 
Makamba ni dhaifu, hujamuonea, ndio ukweli wenyewe huo, majibu ambayo amekuwa akiyatoa kuhusu utendaji kwenye wizara yake yanathibitisha hilo.

Majibu kama niueni, au kama shida ni uwaziri wangu, au Urais wa Samia, yanamuonesha alivyo empty kichwani, anaifikiria zaidi nafasi aliyopo badala ya utendaji wake wizarani hapo.

Hili taifa tumeshaona mara nyingi elimu haina umuhimu sana, mifano miwili ya matukio ya hivi karibuni imethibitisha hayo.

- Uteuzi wa wagombea wa bunge la Afrika Mashariki.

- Utenguzi wa Mulamula akiwa waziri wa mambo ya nje.

Kilicho na umuhimu kwetu ni kujipendekeza, kujuana, nk ndio sifa kuu za mteuliwa kuwa kiongozi.
 
Huku kijijini akina mama waliopewa mitingi ya gesi ya kupikia wapo wanasubiri "ofa" nyingine!
 
Una hoja nzur Sana,
Ila uwasilishaji wako Ni mbovu Sana,
Kuanzisha Uzi ukikosoa huku unadhihaki na kutukana wengine hii haikubaliki
Ukweli huwa unaumiza mara nyingine, au labda useme dhihaka iko wapi hapo, nguini? Maoni yangu ni kwamba wizara ya nishati ni wizara nyeti inayotakiwa kuongozwa na waziri anaeelewa mabo ya sera na utawala wa nishati, hasa katika kipindi hiki kigumu. Sasa kama mama Samia anaona tofauti sawa, leti time prove me wrong, it it hasnt.
 
Makamba Januari amewekwa pale ili Msoga team wamalizie kile ambacho walikuwa wamebakiza.
Baada ya Janabi kuwasafishia njia.

Bwawa la JNHP licheleweshwe kwa maksudi ili wapate fursa ya kuingia mikataba ya kinyonyaji yenye kuwanufaisha na 20% zao,kama ilivyotokea na inavyoendelea.

Kuna mikataba mingi imeingiwa ambayo huko mbeleni itakuja kuwa Scandals tupu.

Aliwaondoa wataalamu husika kwanza,ili waweze kuamua mambo yao bila vikwazo.

Kumbuka Kikwete ndie alimfuata Samia kumtoa Chumbani kumleta ukumbini Chimwaga Dodoma kumtambulisha kwenye CCM/CC kwamba ndie mgombea mwenza wa JPM.

Leo hii Janabi amepewa promotion ya kuwa mkurugenzi wa Muhimbili.

Baada ya kutoka kutubu na kuungama dhambi zao yeye na Kikwete huko Mecca.

Mama yupo autopilot pale,mshika usukani anajulikana.

Angalia Ardhi unamtoa Lukuvi unapeleka Msoga team,sababu tu,Lukuvi asingekubali ufisadi wao.

Tanzania maudhi ni Mengi hata ukiangalia movie gani Duniani...bado utaendea kuudhika ukiwa ukumbini.
 
Umenikumbusha mbali baba yangu yangu aliwahi kuniambia sisi tuliosoma masomo magumu tunalipwa mshahara mdogo kulinganisha na wengine na alinisapoti Bila shida Mwanangu kasome HGL
NB:: MLIOKALILI ENDELEENI NA EMOJI ZENU ZA MISHANGAO NA VICHEKO THIS IS ME NA MIMI NI MIMI SIO WEWE
 
Una hoja nzur Sana,
Ila uwasilishaji wako Ni mbovu Sana,
Kuanzisha Uzi ukikosoa huku unadhihaki na kutukana wengine hii haikubaliki hata kdg
Watalaotukanwa wamestahili matusi,na watakapongezwa wamestahili pongezi hizo.
 
Umenikumbusha mbali baba yangu yangu aliwahi kuniambia sisi tuliosoma masomo magumu tunalipwa mshahara mdogo kulinganisha na wengine na alinisapoti Bila shida Mwanangu kasome HGL
Hiyo ndio reality katika nchi yetu mkuu. Waache wapambane na HGL waje kuwa wanasheria na kazi nyingine. Masomo ya sayansi hayalipi katika nchi hii.
 
Makamba anafanya mambo ya kijinga sana hapo wizarani
Tatizo ni kwamba approach yake sio ya mtu mwenye uelewa wa sera na utawala wa mambo ya nishati. Anatumia uzoefu. Lakini sasa, sometimes uzoefu lazima uendani na ufahamu wa kiutawala na sera katika fani fulani.
 
Tatizo kubwa ni katiba, ilitakiwa mawaziri wawe confirmed na bunge. Huenda Makamba asingeteuliwa au hata kama angeteuliwa asingepita kwenye "check" ya bunge.
 
Kituko zaidi ni kwamba mkurugenzi wa TANESCO ameletwa na Makamba kutoka Multichoice!
Yaani nimesahau kusema huo ulikuwa mshituko wangu mwingine, ngoja niongeze nanshukuru kwa kunikumbusha Mkuu!
 
Back
Top Bottom