Ifike mahala sasa, tusikubali viongozi wetu ambao wanajitoa kufanya kazi kwa moyo mmoja wachafuliwe kirahisi rahisi hivi.
tumeshuhudia tabia hii imeshamiri kwa kasi kubwa sana mara baada ya hayati JPM kuaga dunia!! hili halikubaliki na wala lisifumbiwe macho, tumeona maneno na kashifa nyingi zikitolewa kwa viongozi wetu wajuu, tuhuma za kizushi, majungu na fitina, hii si sawa.
mamlaka zinazo husika chukueni hatua, kwa nini mnaachilia watu wanachafuliwa tu, kutokana na chuki binafsi!!
kazi aliyo ifanya DPP ni ngumu sana ambayo hata angekuwa mtu yoyote yule lazima upate maadui wengi tu, ni sawa na kazi ya Ujaji au Uhakimu kamwe huwezi kupendwa na watu wote lazima wapo wengi watakuchukia kutokana na aina ya kazi yako kuwa huwezi kuwaridhisha watu wote na haswa kama unamsimamo na unasimamia sheria kikamilifu.
Biswalo ni mtu alijitolea kufanya kazi zake kwa uaminifu wa hali ya juu na kutokana na uadilifu wake wapo ambao walitaka kumtoa kwenye msimamo na walishindwa, sasa nadhani ndio wakati wao wa kupiga majungu na kumfitini ilimradi achafuke ili wapate ushindi.
kamwe Rais wetu asiingie kwenye mtengo na kuwasikiliza watu wenye chuki zao binafsi.
tumeshuhudia tabia hii imeshamiri kwa kasi kubwa sana mara baada ya hayati JPM kuaga dunia!! hili halikubaliki na wala lisifumbiwe macho, tumeona maneno na kashifa nyingi zikitolewa kwa viongozi wetu wajuu, tuhuma za kizushi, majungu na fitina, hii si sawa.
mamlaka zinazo husika chukueni hatua, kwa nini mnaachilia watu wanachafuliwa tu, kutokana na chuki binafsi!!
kazi aliyo ifanya DPP ni ngumu sana ambayo hata angekuwa mtu yoyote yule lazima upate maadui wengi tu, ni sawa na kazi ya Ujaji au Uhakimu kamwe huwezi kupendwa na watu wote lazima wapo wengi watakuchukia kutokana na aina ya kazi yako kuwa huwezi kuwaridhisha watu wote na haswa kama unamsimamo na unasimamia sheria kikamilifu.
Biswalo ni mtu alijitolea kufanya kazi zake kwa uaminifu wa hali ya juu na kutokana na uadilifu wake wapo ambao walitaka kumtoa kwenye msimamo na walishindwa, sasa nadhani ndio wakati wao wa kupiga majungu na kumfitini ilimradi achafuke ili wapate ushindi.
kamwe Rais wetu asiingie kwenye mtengo na kuwasikiliza watu wenye chuki zao binafsi.