Utata wa dhehebu lako katika kufunga ndoa

Utata wa dhehebu lako katika kufunga ndoa

Haulijui fungu la usifunge nira wasioamini???
Pole!
Fuatilia kisa cha Abraham kumtafutia mwanae mke ambaye alikuwa Rebeka process ilikuwaje
Samson alionywaje asifunge nila na watu wa mataifa.
Nenda ufunue mafungu usome, acha uvivu.
Asante, ila sidhani kama na wewe una fahamu vifungu vyote katika biblia
 
kwa msabato hatoboi, msabato ahame sijawahi ona. kuna jamaa yangu alidanganya ahamie usabatoni watampa uchungaji, na ndugu wa mke watamuingiza kwenye system ya watu wasiojulikana.

Mpaka leo tunaongea naona(ga) dish lake limeyumba kidogo kutokana na ahadi alizopewa haijatimia hata moja ila anamini si muda anakuwa mchungaji na mtu wa suti nyeusi
Kama ndio hivyo, basi hii ni hatari
 
Baba ndiyo kichwa cha nyumba

1.Enyi wanawake watiin waume zenu, 2 Enyi waume wapendeni wake zenu

Msabato ni ishu.Kama huyo jamaa hataki kwenda usabato basi aachane na huyo mwanamke .maana msabato kuhama usabato ni sawa na ngamia kuingia tundu la sindano
Aisee kama ndio hivyo, basi hii ni shida sio kidogo
 
Mwambie mwanao atafute mlutheri mwenzake wasabato wanapendaga kujihesabia haki sana! Yaani hiyo ndoa ikifungwa huko mbeleni atapata shida mno.
 
Hapa nyumbani ninaishi na msabato, ni watu wabishi sana kwa asili, hii sumu sijui wanalishwa huko kanisani kwao. Huwa wanaamini wao tu ndio wenye tiketi ya Mbinguni, hakuna msabato utakaemkuta sio mbishi. Huyo binti atamsumbua sana huyo kijana, anashindwa kuelewa mapenzi yako beyond riligious blvs. Huyo kijana afanye maamuzi ila suala la kumconvice huyo binti sio rahisi. Ndani ya ndoa hakutakuwa na utulivu otherwise wamekubaliana kukaa wote upande mmoja. Kama ataendelea kuwa mbishi mwambia amtie pembeni, wadada wazuri na wenye imani thabiti wapo hata huko KKKT kwake.
Asante kwa ushuhuda, pia na ushauri mzuri
 
Kwanini umeamua ku sitisha ndugu?
Kwa Sababu hatuelewani kwa hilo suala la wapi tufunge ndoa
Mosi: anaweza kuwa hataki tu kuolewa na Mimi so akatumia kigezo cha dini kukomalia ishindikane, n.a. ukiamua kukubali ni mwanzo wa kuonyesha udhaifu kwa Tabia za wadada wa kiafrica, ataendelea kukubadilikia kila uchwao.
Pili: Mimi huwa nikiona kitu kinakuwa na dalili za kushindikana, naairisha maana kama anakupenda kweli hawezi kukupinga au ww huwezi kumpinga
Tatu; tukikomaa tukafunge Kwa Dc baada ya ndoa mtasalije? Nani atamfuta nani au kila mtu kivyake, ibada za nyumbani je? Watoto wataenda wapi, mtaonekanaje kwa watoto
Kiujumla ni mwanzo wa mtafaruku, achilia mbali ratiba za ibada na maombi ya usiku sijui kwa walokole na blabla nyingine
 
nkikumbuka walivyotaka kusafir bila visa hata passport sijashangaa sana
Umenikumbusha kile kisa wale wasabato walikaa pale Julias Nyerere airport wiki nzima wakitaka wasafiri bila passport wala nauli.
Halafu walikuwa wanajiita wasabato masalia, sijui hata walikuwa wana maana gani kujiita wasabato masalia?
 
Kwa kukushauri tu, mwambie atafute mtu wa KKKT au dhehebu lolote la Kikristo, Ndoa na Msabato ni pasua kichwa, Msabato hachangamani na Mkristo yoyote, nimeshuhudia mateso makubwa ya ndoa a Msabato na Mkristo (Catholic, KKKT, Mlokole) Kuoa ni mara moja tu na ukikosea ni kila kitu
Wasabato waoane wenyewe kwa wenyewe!
 
Umenikumbusha kile kisa wale wasabato walikaa pale Julias Nyerere airport wiki nzima wakitaka wasafiri bila passport wala nauli.
Halafu walikuwa wanajiita wasabato masalia, sijui hata walikuwa wana maana gani kujiita wasabato masalia?
haaaaaa sasa unazan kwa ubishi ule ndo ndoa itafungika bro
 
Back
Top Bottom