afu kibaya zaidi wanaamini wenzao wana dhambi then wao pekee ndo wenye haki mbele za Mungu.......wamesahau kwamba tunahesabiwa haki kwa neema kwa njia ya imani.
Tatizo lenu mnabagua ila Mungu habagui...na mibaraka ya ndoa Mungu anatoa kwa wote na mbinguni wataenda watu wa aina zoteSisi sio kama mafarisayo
Ungefafanua maana ya ng'mbe kuanguka Shimoni. Kuitunza sabato ni Amri si ombi.
Wasabato tupo wengi sana. Ni tamaa tu zinapeleka watu nje.
Hata Samson alioa nje, alichokutana nacho nawe unakijua
Mibaraka NdioTatizo lenu mnabagua ila Mungu habagui...na mibaraka ya ndoa Mungu anatoa kwa wote na mbinguni wataenda watu wa aina zote
Mrejesho, mkuu vipi huko kimetokea Nini?Leo ni mara ya kwanza kuingia kwenye hili jukwaa wadau, nategemea ushauri wa maana juu ya hili jambo.
Iko hivi kuna kijana wangu anaomba ushauri kuhusu tatizo linalomsumbua yeye ni mkristo wa dhehebu la KKKT na ana mchumba wake ni msabato, sasa mda unazidi kwenda kijana anataka kufunga ndoa.
Kijana akatoa wazo kwa binti kwamba ndoa inatakiwa ifungwe kanisani KKKT na baada ya ndoa binti ataendelea na dhehebu la kisabato.
Sasa binti amegoma kabisa, binti nae kasema hawezi kufunga ndoa KKKT anataka ndoa ifungwe kanisani sabato na baada ya ndoa kamruhusu kijana aendelee na dhehebu la KKKT.
Sasa ubishano upo kwenye wapi ndoa ifungwe kati ya Kanisani KKKT au sabato, na imefika hatua kwamba endapo mmoja atakataa kukubali mawazo ya mwenzie wanasema bora mahusiano yaishe.
Sasa wadau mnaushauri gani ili kuweza kuwanusuru huyu kijana pamoja na huyo mchumba wake.
Nimewashauri kuhusu ndoa ya kiserikali, ila wote hawako tayari kwa ndoa ya kufungwa serikalini.
Je mnamshauri nini huyu kijana na mchumba wake ili waweze kufanikisha mipango yao ya kufunga ndoa pamoja?
Watakua walitemana hao.. Mimi aliwahi kuwepo m TAG mtoto wa Pastor akaniambia lazima uhamie nikamu intertain alainike ila akagoma nikapiga chini faster nikaja nikapata mtu anaenisikiliza kwa kila kitu alikua TAG akahamia kkkt nikaamua kutulia nae... Nilijiambia siwez endeshwa na mwanamke maisha yangu yoteMrejesho, mkuu vipi huko kimetokea Nini?
Ilishawahi mkuta ndugu yangu hii duu wasabato wanamisimamo mikali mkuu! Lakini br aliamua kufanya maamuzi ya kiume ya kuvunja mahusiano na kuangalia mambo mengine.Leo ni mara ya kwanza kuingia kwenye hili jukwaa wadau, nategemea ushauri wa maana juu ya hili jambo.
Iko hivi kuna kijana wangu anaomba ushauri kuhusu tatizo linalomsumbua yeye ni mkristo wa dhehebu la KKKT na ana mchumba wake ni msabato, sasa mda unazidi kwenda kijana anataka kufunga ndoa.
Kijana akatoa wazo kwa binti kwamba ndoa inatakiwa ifungwe kanisani KKKT na baada ya ndoa binti ataendelea na dhehebu la kisabato.
Sasa binti amegoma kabisa, binti nae kasema hawezi kufunga ndoa KKKT anataka ndoa ifungwe kanisani sabato na baada ya ndoa kamruhusu kijana aendelee na dhehebu la KKKT. Sasa ubishano upo kwenye wapi ndoa ifungwe kati ya Kanisani KKKT au sabato, na imefika hatua kwamba endapo mmoja atakataa kukubali mawazo ya mwenzie wanasema bora mahusiano yaishe.
Sasa wadau mnaushauri gani ili kuweza kuwanusuru huyu kijana pamoja na huyo mchumba wake.
Nimewashauri kuhusu ndoa ya kiserikali, ila wote hawako tayari kwa ndoa ya kufungwa serikalini.
Je, mnamshauri nini huyu kijana na mchumba wake ili waweze kufanikisha mipango yao ya kufunga ndoa pamoja?
Usumbufu wao si ndo huo we unaona ni jambo la kawaida kwa mwanamke kushikilia msimamo wa kutaka mwanaume akafungie ndoa kwenye kanisa la mwanamke!Unajua ishu ni kwamba nahitaji kujua usumbufu wa wasabato ili nipate picha kamili?