Utata mwanamke kujinyonga polisi

Utata mwanamke kujinyonga polisi

Kikawaida polisi post mburahati haiwezi kukosa watuhumiwa wengine,na huwa wanawake hawachanganywi na wanaume. Huyo walishindwana tu labda aligoma kuwapa mzigo
 
Dah...ni ujinga tu kujiua kwa sababu ya madeni….wakati mtu unaweza kuishi kwa figo moja bila tatizo lolote...Kule Iran ambako figo zinauzwa kihalali….figo moja bei yake ni kati ya shilingi milioni 120 hadi 300 kutokana na ubora ...halafu wewe unajiua...unafukiwa na figo zako
Kama ameweza kujisalimisha mwenyewe polisi, kwa ujasili huo je uoga wa ku jinyonga ameutoa wapi! Na je mazingira ya sero unaweza vipi kujinyonga?

Sero inarindea mda wote, Sasa je walishindwa vipi kuzuia tukio.

Polosi wameua mama wa watu! Tunadanganya tu hapa .
 
Kwani sikuhizi kila mahabusu na chumba chake?..🙉🙉
 
Lugumi Akamatwe na Kuhukumiwa Mara Moja. Mhe. Kikwete alipanga kuweka CCTV kwenye vituo vyote vya polisi.
 
Hii nchi tutarudi kwenye mambo ya kurogana.

Kule Njombe kuna kitu wanaita " TEGO".......ni balaa hiyo kitu bwashee!
Jamii yoyote inayozidiwa na hali ya umasikini, kinachofuata ni kulogana tu, kwani , mambo yanapokuwa hayaendi vizuri, lazima atafutwe mchawi, na awamu hii mtu usimchezee kabisa .
 
Kama ameweza kujisalimisha mwenyewe polisi, kwa ujasili huo je uoga wa ku jinyonga ameutoa wapi! Na je mazingira ya sero unaweza vipi kujinyonga?

Sero inarindea mda wote, Sasa je walishindwa vipi kuzuia tukio.

Polosi wameua mama wa watu! Tunadanganya tu hapa .

RIP Tapeli afisa feki, ulikuwa unachafua taasisi na Maisha yako yalileta vilio kwa wengine. Familia ihangaike kulipa madeni na kufuta kesi.
 
Kama aliweza kufika hadi kituo cha POLISI basi alikuwa anao uwezo wa kujinyonga akiwa nyumbani kwake, kwanini hakujinyongea nyumbani ambapo alikuwa huru kabisa kufanya hilo na jingine bila ya kuonwa na yeyote kwani shida yake si ilikuwa ni kujitoa uhai, Maswali kama haya ndio yanayosababisha kuwe na utata katika tukio hili. Polisi mtoe majibu nyoofu hasa kwenye eneo la Hospitali maana kwa mujibu wa taarifa hapo ukiisoma vizuri, ni kwamba ndugu walipofika Polisi waliambiwa kuwa wamechelewa kupeleka chai kwaiyo wapeleke saa 5. walipofika hiyo saa 5 wakaambiwa yupo Muhimbili alijaribu kujinyonga, walipofika Muhimbili wameambiwa amefikishwa na Polisi saa 5 akiwa kashakufa . sasa wale waliosema mrudi saa 5 na hawa waliompeleka Muhimbili saa 5 ni watu tofauti?
 
RIP Tapeli afisa feki, ulikuwa unachafua taasisi na Maisha yako yalileta vilio kwa wengine. Familia ihangaike kulipa madeni na kufuta kesi.
Alikuwa anajifanya ofisa wa nini?
 
RIP Tapeli afisa feki, ulikuwa unachafua taasisi na Maisha yako yalileta vilio kwa wengine. Familia ihangaike kulipa madeni na kufuta kesi.
Umeeleweka vizuri sana.

Bado nashindwa amini kifo hiki inawezekana Ni mchongo wa polisi na mama huyu ili kumaliza kesi

Life goes on!!!
 
Kajisalimisha ili akajinyonge mahabusu hii chai ya moto sana
 
Dah...ni ujinga tu kujiua kwa sababu ya madeni….wakati mtu unaweza kuishi kwa figo moja bila tatizo lolote...Kule Iran ambako figo zinauzwa kihalali….figo moja bei yake ni kati ya shilingi milioni 120 hadi 300 kutokana na ubora ...halafu wewe unajiua...unafukiwa na figo zako 🤣 🤣🤭
Kwa hiyo unatushauri twende Iran tukauze figo zetu? Ila kumbuka ukija na fedha nyingi kiasi hicho utaishia pale JNIA na kuwekwa ndani kisa unatakatisha fedha. Kesi hiyo haina dhamana.
 
yaani ajipeleke mwenyewe kituoni alafu ajinyonge si angejinyonga mtaani huku

kwa mawazo yangu kuna ma 2
1.polisi wanahusika na kifo chake

2.mahojiano yalijaa vitisho sana hadi kumfanya ajinyonge ila hili ni asilimia 2
 
MASWALI YA KUJIULIZA.

1. Ilitokea bahati mbaya gani mpaka akawa peke yake mahabusu ? Hili jambo gumu sana

2. Aliwekwa kituoni kwa makosa yepi ??

3. Mchakato wote wa kujinyonga polisi walikuwa wapi ??

4. Kwa nini apelekwe kituoni usiku wa saa 5:27 wakati polisi walikuwa mbali ya kituo wakati wote wa kujinyonga hiyo saa 5:27 walitokea wapi ?

5. Nguo aliyojinyongea ina uimara kiasi gani na ni ya aina gani ??

6. Polisi wana mamraka ya kuua mahabusu ??


NCHI HII SA HIVI WOTE TUMEKUWA WATUMWA KWENYE NCHI YETU WENYEWE.
Avatar yako na ulichokiandika haviendani. Kijani si inabidi u praise mwanzo mwisho?😲 Liwe baya liwe zuri. Au akili zishatuingia baada ya uchaguz?!
 
MASWALI YA KUJIULIZA.

1. Ilitokea bahati mbaya gani mpaka akawa peke yake mahabusu ? Hili jambo gumu sana

2. Aliwekwa kituoni kwa makosa yepi ??

3. Mchakato wote wa kujinyonga polisi walikuwa wapi ??

4. Kwa nini apelekwe kituoni usiku wa saa 5:27 wakati polisi walikuwa mbali ya kituo wakati wote wa kujinyonga hiyo saa 5:27 walitokea wapi ?

5. Nguo aliyojinyongea ina uimara kiasi gani na ni ya aina gani ??

6. Polisi wana mamraka ya kuua mahabusu ??


NCHI HII SA HIVI WOTE TUMEKUWA WATUMWA KWENYE NCHI YETU WENYEWE.
. Upande mmoja alijifunga kwenye shingo na kujinyonga, ule upande mwingine aliufunga wapi?
Kwenye zile nondo za vidirisha vidogo vya juu vya mahabusu?
Alifikaje Kyle juu na kufunga fundo?
Alipandaje Kyle juu na kufunga fundo?
Ilikuwaje ghafla akawa peke take mahabusu had I akaweza kuyafanya yote hayo bila MTU kumuona?
Hivi Tanzania sasa imekuwa Kweli Kisiwa cha Amani kiasi kwamba kwa Sikukuu kama hii Mahabusu inaweza kuwa na Mfungwa Mmoja tu ambaye anaweza kujinyonga kwa nafasi bila kubughudhiwa na MTU?

Kuna Maswali mengi ya kawaida kabisa yanahitaji majibu hapo...!
 
Back
Top Bottom