Duke Tachez
JF-Expert Member
- Mar 28, 2018
- 5,441
- 4,093
Katika kupita mitandaoni nimeona taarifa inasema bahati bukuku ameachana na mumewe, pia juzi tu niliona video florah mbasha anasema kwamba kuna vifungu kwenye biblia vinaruhusu mwanamke kuolewa mara mbili na kwa bahati mbaya Sana hakuvitaja vifungu hivyo, akasema huyo mume wake mpya amemzidi kwa mwezi mmoja wakati amemzidi miaka mingi tu, Sasa kuna mstari kwenye biblia unasema alichokiunganisha Mungu mwana damu asikitenganishe, jamani wataalam wa maandiko binafsi nahitaji elimu hapa maana navyojua ndoa za kikristo marufuku kuachana au sijaelewa