Ndoa za kikristo hazifati maandiko ya kwenye biblia, zinafata sheria za viongozi wa makanisa

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Hizi ndoa za kikristo zimefikia mahala sasa tunaweza kuziita ndoa za kisheria kwasababu watu wanaona mahakamani kuna unafuu kuliko kufata sheria za ndoa za kikristo.

Usijidanganye kizazi hiki kwamba mke mwema anashushwa na Bwana, mwanamke unaweza kumchunguza mwaka mzima mkiwa kwenye uchumba na ukaona ndiyo hapa nimepata "Wife material".

Muoe sasa uone timbwili lake na makucha aliyoficha, hutakosa kuona rangi yoyote. Kiburi kitaanza kwa jeuri ya ndoa akiona kwamba wote mpo sawa, maana sheria za viongozi wa kanisa zimekubana ugandane naye mpaka kifo na huruhusiwi kuoa mke mwengine.

Maandiko yapo wazi kabisa huwezi kumuacha mpaka kifo ama afanye uashareti nje ya ndoa, lakini hakuna sehemu wamekataza kuongeza mke! Kuhusu kuoa wake wawili hapa ndipo tulipoingizwa cha kike hasa kwetu Waafrika.

Watu wanakuja na utetezi wa mistari ile ya kila mwanaume awe na "Mke wake", hivi nitoe mfano tu mtu ana wake watatu;

~ Mke wa kwanza sio "Mke wake"?
~ Mke wa pili sio "Mke wake"?
~ Mke wa tatu sio "Mke wake"?

Hata kwa mwanaume mwenye mke moja, naye huyo moja ni mke wake.

Yesu pia aliongelea tu kuhusu kutoa talaka hakuzungumzia chochote kuhusu kukataza kuongeza mke. Wakati huo aliokuwepo kulikuwa na wa Israel wengi tu wenye mke zaidi ya mmoja kama mababu zao akina Musa walioleta Amri 10 za Mungu.

Kuna hii hoja nyingine ya "Mwili moja" inatafsiriwa vibaya ili kuendana na sheria za viongozi wa makanisa wanaobana mwanaume asioe mke wa ziada.

Mwanaume ni mwili moja na kila mwanamke ataekutana nae kimwili, iwe ni kwenye ndoa yenye baraka zake Mungu ama nje ya ndoa akiwa na malaya. Kwahiyo pale mwanaume anapokuwa mwili moja na mke wake bado haiondoi kwake kuwa mwili moja na wake wengine.

Hata sisi wanadamu tupo zaidi ya bilioni lakini Mungu yupo moja ila kila anaeungana roho yake, Mungu hutengeneza roho moja. Ndivyo ilivyo hivi kwa wanawake wengi wakiolewa na mwanaume moja, kila mmoja wao huwa ni mwili mmoja na mme moja. Siongei maneno matupu bila maandiko ya biblia 1-wakorintho 6:16;

"Au hamjui ya kuwa hata yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja, Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye."

Madhara yake siku hizi wakristo wengi hawana muda na sheria za viongozi wa makanisa wanakimbilia kuyamaliza mahakamani ili kuoa mke mwengine.

kumbana mwanaume kuwa na mke moja matokeo yake ndiyo haya tunayoyaona michepuko imekuwa kawaida sana siku hizi.
 
Si uoe wake wengi ?Kwani umefungwa kamba ?
Hadi sasa sijaona kanisa linalofata maandiko kama yalivyo kwenye biblia, sheria zinazofatwa ni za viongozi wa makanisa zikiwemo sheria za utesaji za kulazimisha mapadre wasifanye sex maisha yao yote, ndizo hizi sheria iliwafanya kina Dokta slaa wakimbie upadri, waliobaki ndio hawa wengi wenye watoto wa siri mitaani na lundo la kesi za kulawiti watoto wa kiume
 
Hizo Ndoa za kikristo zimefikia mahala sasa tunaweza kuziita ndoa za kisheria kwasababu watu wanaona mahakamani kuna unafuu kuliko kufata Sheria za ndoa za kikristo.

Usijidanganye kizazi hiki kwamba mke mwema anashushwa na Bwana, Mwanamke unaweza kumchunguza mwaka mzima mkiwa kwenye uchumba na ukaona Yes! Hapa nimepata wife material, Muoe Sasa uone timbwili lake na makucha aliyoficha, hutakosa kuona rangi yoyote, Kiburi kitaanza Kwa jeuri ya ndoa akiona kwamba wote mpo sawa Sasa.

ukienda kuanza kufatilia divorce kanisa linakwambia ulikula kiapo cha kuachana nae mpaka kifo ama uje na ushahidi wa mwenzako ni muashareti, Yani kuleta tu huo ushahidi ni kukiri wazi umechapiwa!! aibu ilioje hii kwa mwanaume! kwanini yasiishe kimya kimya tu, Mbaya zaidi huwezi kutoa talaja hata kama nyumbani hakuna amani, Kuna vipigo, mwenzako ni mchawi, hapendi ndugu zako, n.k hizi sababu kanisa hazizitambui,,, ndio ujinga huu unaofanya wakristo wengi kwenda kuyamaliza mahakamani na hata kuhonga honga wajinasue.

Kuhusu kuona wake wawili napo hapa ni kukaza mafuvu tu hasa kwetu waafrika

Watu wanakuja na utetezi wa mistari Ile ya Kila mwanaume awe na "mke wake", hivi nitoe mfano tu mtu ana wake watu,

mke wa kwanza sio "mke wake"?
mke wa pili sio "mke wake" ?
mke wa tatu sio "mke wake"?

Hata Kwa mwanaume mwenye mke moja nae huyo moja ni mke wake.

Pia tukija Kwa Yesu aliongelea tu kuhusu pale inapobidi umpe talaka mke na Wala hakuzungumzia chochote kuhusu kukataza kuoa mke zaidi ya Moja, wakati huo aliokuwepo kulikiwa na wa Israel wengi tu wenye mke zaidi ya moja kama mababu zao kina Musa walioleta amri 10 za Mungu.

Madhara yake siku hizi wakristo wengi hawana muda na sheria za viongozi wa makanisa wanakimbilia kuyamaliza mahakamani.

kumbana mwanaume kuwa na mke moja matokeo yake ndio haya tunayoyaona michepuko imekuwa kawaida sana siku hizi
Nimejizuia tu lakini unastahili tusi! Waislamu wanaoruhusiwa kuoa wanawake hadi 4 hawana michepuko?
 
Ndoa ya kikristo inabidi ifate maandiko ya kwenye biblia na sio sheria za viongozi wa makanisa.
Kwani mkuu umefungishwa ndoa ambayo haijafuata maandiko? Maana ndoa zetu maandiko yanasema utaachana na wazazi na utaambatana na mume/mke, maandiko yanaagiza mwanaume kumpenda mke na mke kumuheshimu mume, kama maagizo hayo yakivunjwa automatically ndoa inakua haijatendewa haki
 
Wewe umeamua kuwa mkaidi basi kuwa mkaidi kivyako acha kujifanya mjuaji kuliko neno la Mungu.

Soon utakuwa umekufa na hili neno utaliacha.
 
Nimejizuia tu lakini unastahili tusi! Waislamu wanaoruhusiwa kuoa wanawake hadi 4 hawana michepuko?
Ishu ni kwamba muislamu anaweza kuongeza mke lakini mkristo anachoweza kuongeza ni mchepuko tu
 
Mleta mada ruksa kuoa hata wake 10 shida iko wapi tuache sisi tunaozitii sheria za viongozi wetu wa dini badala ya biblia.
Nimefurahi kujua kwamba wapo wakristo mnaofata viongozi badala ya maandiko, mtapuliziwa sana dawa za mbu kuamini kwamba zinatoa mapepo
1665077923671.png
 
Back
Top Bottom