Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mie ningepewa dakika 2 tu za kukaa naye .............ngoja nisiseme, nina hasira naye.
Mh. Jakaya Kikwete, CCM kujivua gamba, suala lisiwe kujisafisha tu bali kuleta maendeleo kwa wananchi
*Kama ni kweli kauli yako kuhusu kujivua gamba kama nyoka ulimaanisha CCM ni kama nyoka, ujumbe huo
utakuwa na maana kuwa tumeshang'atwa sana na nyoka (CCM) huyu na sasa utakuwa umetambua kile
kinacholalamikiwa muda mrefu na wananchi kuhusu IPTL, Deep Green, Meremeta, Richmond/DOWANS, EPA na
mengine kibao. Hivyo gamba jipya litusaidie kumwona nyoka huyo hata kama atajificha gizani.
*Kama kweli wewe na Chama Cha Mapinduzi mna nia ya dhati kujivua gamba na kuwatumikia wananchi,
mnapaswa muanze sasa kuwekeza katika kuhakikisha kunakuwepo uwiano sawa kwenye mgawanyo wa rasilimali
ili kwenda sawa na kaulimbiu yako ya Maisha bora kwa kila Mtanzania.
*Najua unalewa kuwa asilimia kubwa ya wananchi wa Tanzania wanaishi vijijini kwa kutegemea jembe la mkono,
kipato wanachopata kutokana na kilimo cha aina hiyo hakiwasaidii kukidhi mahitaji yao muhimu ya kila siku. Ile kauli
ya mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe ingekuwa na ukweli, wananchi wa Tanzania wangekuwa matajiri.
*Rais, wananchi wanalalamika kuwa wakija mijini hali bado ni ngumu wakati nyinyi tuliowapa dhamana ya kuweka
mazingira hayo mmelala usingizi na kufikiria jinsi ya kutengeneza mikataba feki ili mchote fungu mnaloliona lipo 'idle' .
*Ni wakati sasa uelewe kuwa Watanzania siyo wavivu kama unavyofikiria, uchumi siyo kutoa takwimu tu bali
kuwawezesha Watanzania kuwa na matumaini ya kuuza mazao yao kwa wakati kutoka mashambani. Kwa hiyo kujivua
gamba kwa chama chako kusiishie kwenye kubadilisha uongozi tu, unapaswa uyaone haya na kuyatekeleza kivitendo.
Naomba kuwasilisha...
Mh. Jakaya Kikwete, CCM kujivua gamba, suala lisiwe kujisafisha tu bali kuleta maendeleo kwa wananchi
*Kama ni kweli kauli yako kuhusu kujivua gamba kama nyoka ulimaanisha CCM ni kama nyoka, ujumbe huo
utakuwa na maana kuwa tumeshang'atwa sana na nyoka (CCM) huyu na sasa utakuwa umetambua kile
kinacholalamikiwa muda mrefu na wananchi kuhusu IPTL, Deep Green, Meremeta, Richmond/DOWANS, EPA na
mengine kibao. Hivyo gamba jipya litusaidie kumwona nyoka huyo hata kama atajificha gizani.
*Kama kweli wewe na Chama Cha Mapinduzi mna nia ya dhati kujivua gamba na kuwatumikia wananchi,
mnapaswa muanze sasa kuwekeza katika kuhakikisha kunakuwepo uwiano sawa kwenye mgawanyo wa rasilimali
ili kwenda sawa na kaulimbiu yako ya "Maisha bora kwa kila Mtanzania".
*Najua unaleewa kuwa asilimia kubwa ya wananchi wa Tanzania wanaishi vijijini kwa kutegemea jembe la mkono,
kipato wanachopata kutokana na kilimo cha aina hiyo hakiwasaidii kukidhi mahitaji yao muhimu ya kila siku. Ile kauli
ya mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe ingekuwa na ukweli, wananchi wa Tanzania wangekuwa matajiri.
*Rais, wananchi wanalalamika kuwa wakija mijini hali bado ni ngumu wakati nyinyi tuliowapa dhamana ya kuweka
mazingira hayo mmelala usingizi na kufikiria jinsi ya kutengeneza mikataba feki ili mchote fungu mnaloliona lipo 'idle' .
*Ni wakati sasa uelewe kuwa Watanzania siyo wavivu kama unavyofikiria, uchumi siyo kutoa takwimu tu bali
kuwawezesha Watanzania kuwa na matumaini ya kuuza mazao yao kwa wakati kutoka mashambani. Kwa hiyo kujivua
gamba kwa chama chako kusiishie kwenye kubadilisha uongozi tu, unapaswa uyaone haya na kuyatekeleza kivitendo.
Naomba kuwasilisha...
Maneno yote haya na alivyo mvivu na kila*a sidhani kama atakusikiliza!!